Ufisadi nje ya geti la waziri mkuu.....

wimbi la mbele

JF-Expert Member
Jan 4, 2011
647
266
Weekend hii nilikuwa nafanya mzunguko nilitembea kwa gari hadi Oysterbay maeneo ya cocobeach, wakati narudi nikapita njia ambayo kisheria hairuhusiwi namimi sikujua kama hairuhusiwi kupita njia hiyo. Njia hiyo ni ile ya pale anapoishi Waziri Mkuu, askari aliyekuwa amebeba bunduki akanistopisha na kusema niteremke ndani ya gari nikaandike statement na sikuwa mimi peke yangu niliyepita kwa njia hiyo bali wengi tulipita njia hiyo na tukakamatwa.Kila mtu kaomba msamaha lakini hakuna aliyesamehewa, Kumbe nia ya hao askari ni kuomba rushwa ili wakuachie na karibia watu wote tuliopita njia hiyo walitoa rushwa kwa hao askari ndio wote tukaachiwa. Jamani hawa askari wetu mbona njaa itawaua maana inatia aibu sana.


U-turn naomba uipublish hii ili wakae watambue kuwa wanavyofanya sivyo,

Asante,


Mange naomba uifiche email yangu tafadhali.

Omg, this happened to me,nilikuwa natoka Golden Tulip ,si mnajua kile kifoleni cha pale coco beach siku za jumapili,so nikaamua kukata short cut, kumbe ile short cut bwana ni nyumbani kwa waziri mkuu hapo hapo nikasimamishwa na askari waliobeba bunduki, nikajaribu kuwaambia kuwa sikujua na sikuona alama yoyote inayosema kuwa siruhusiwi kutumia barabara hii, kwani walielewa wakaniambia haya geuza twende kituoni, ilibidi niongee nao kiutu uzima ndo wakaniachia nikaondoka.(naogopa kuongea details nsije nkaji incriminate,maana nasikia mpokea rushwa na mtoa rushwa adhabu ni ile ile)LOL…

Really this has to stop especially cos inatokea nyumbani kwa waziri mkuu.

Mange

U Turn Blog
 
Mimi sioni kwa nini unalalamika.Umevunja sheria,kuna kibao kikubwa kinaonyesha usipite pale ni one way.
Pole mkuu kuwa mwangalifu na sheria za barabara.
 
Teh teh teh:) Vijana wa police usiwape mwanya wa kukukuta na hatia/kosa kama hilo!!! Yaani hiyo umewapelekea hela kiulaaaini....

Next time uwe makini!! Punguza sababu za kuombwa rushwa kwa kutovunja sheria hasa za barabarani:)
 
Kuna kibao kinaonyesha njia inaingia upande mmoja tu na hii nafikiri ni kwa sababau za kiusalama. Hata hivyo, watanzania wengi nilikiwemo mimi tumezoea kuendesha vyombo vya moto barabarani bila kuangalia alama za barabarani hata kwa njia ambazo hatuna mazoea nazo. Kimsingi kama njia yoyote hupiti mara kwa mara au haujawahi pita kitu cha kwanza ni kuangalia alama za usalama barabarani.
 
Ili tuweze kupunguza askari wetu kura rushwa tuwe waangalifu kufanya makosa vinginevyo tuwe tayari kulipa gharama za kosa hilo ama kituo cha polisi au kwa polisi mwenyewe kama wewe ni mmoja wa wale wasambaza rushwa kwa askari wetu wenye tamaa ya pesa kama mamba kwenye kina cha maji marefu.
 
Big red round with white line very visible, u can't miss it even at night...h'fu ni kama umekutana na polisi mara ya kwanza, hivyo inaonyesha wewe ni 'learner' na hukujifunzia kwenye shule rasmi....judging from kichwa cha habari na habari yenyewe...
 
Ili tuweze kupunguza askari wetu kura rushwa tuwe waangalifu kufanya makosa vinginevyo tuwe tayari kulipa gharama za kosa hilo ama kituo cha polisi au kwa polisi mwenyewe kama wewe ni mmoja wa wale wasambaza rushwa kwa askari wetu wenye tamaa ya pesa kama mamba kwenye kina cha maji marefu.

hasa ukizingatia kuwa bajeti hii imepandisha 'maximum notification fee' kutoka TZS 20,000/= hadi TZS 200,000/=.
 
Back
Top Bottom