Bishop Hiluka
JF-Expert Member
- Aug 12, 2011
- 7,147
- 14,711
* Wakaguzi wabaini ufujaji pesa za miradi
* Mabilioni ya pesa za walipa kodi yayeyuka
* Kashfa kwenye ununuzi wa mashangingi 68
* Wafadhili watishia kuzuia misaada yao
WIZARA ya Maji na Umwagiliaji imekumbwa na kashfa kubwa baada ya ukaguzi maalumu
uliofanywa kwenye miradi ya maji nchi nzima kubaini tuhuma za ufisadi, uzembe wa maofisa
na matumizi mabaya ya mabilioni ya shilingi kwenye wizara hiyo.
Ukaguzi maalumu (special audit) uliofanywa na Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu
za Serikali (CAG) kwenye programu ya maendeleo ya sekta ya maji (2007-2010) umebaini
malipo mengi ya utata kwenye miradi ya maji nchini na matumizi mabaya ya pesa za umma.
Katika moja ya tuhuma hizo za ufisadi, Wizara ya Maji na Umwagiliaji imebainika kutumia zaidi
ya dola za Marekani milioni 39 (takribani shilingi bilioni 63) kwenye mazingira ya utata bila
kuzingatia miradi iliyopo kwenye mpango kazi wa mwaka wa wizara hiyo.
"Shughuli za manunuzi ndani ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji hazifanywi kuendana na mpango
wa manunuzi wa kila mwaka," imesema sehemu hiyo ya ripoti mpya ya CAG kutokana na ukaguzi
uliofanywa Septemba mwaka jana.
Pia ukaguzi huo umebaini kashfa kwenye ununuzi wa mashangingi (Toyota Land Cruiser) yapatayo 68
uliofanyika mwaka 2009 kwa Yen za Japan milioni 235.4 (zaidi ya shilingi bilioni 5) kinyume na utaratibu
rasmi wa manunuzi ndani ya serikali.
Kwa mujibu wa wakaguzi wa ofisi ya CAG, ununuzi huo wa mashangingi bila kufuata taratibu za serikali
umeisababishia wizara hasara ya zaidi ya shilingi milioni 218 kutokana na tofauti ya viwango vya
ubadilishaji wa pesa za kigeni.
Wizara hiyo imebainika kutokuwa na ufuatiliaji wa karibu wa pesa za miradi ya maji zinazopelekwa
nchi nzima kwenye mamlaka za serikali za mitaa na hivyo basi kutojua kama pesa hizo zimetumiwa
kwenye matumizi sahihi ama la.
Wizara hiyo pia imekumbwa na kashfa ya matumizi makubwa ya pesa kwenye miradi mbalimbali ya
maji kuliko gharama halisi za awali zilizokubaliwa kwenye miradi hiyo.
Mifano hiyo ni pamoja na mradi wa ujenzi wa Bwawa la Matwiga ambapo wakati mkataba wa awali
ulisema kuwa mradi utagharimu dola za Marekani 284,693, wizara hiyo iliongeza malipo ya ziada
kwenye mradi huo ya dola 80,615 (wastani wa shilingi milioni 129).
Kwenye mradi wa Mpwapwa na Utete, wizara ilitumia dola za Marekani 32,250 zaidi ya gharama
halisi ya mradi huo kwenye mkataba wa ujenzi ambayo ilikuwa ni $39,600.
Mamlaka ya Maji Safi na Taka ya Moshi nayo ilitumia $947,757.53 (shilingi bilioni 1.5) kuilipa
kampuni ya Seureca Consulting Egineers ya Ufaransa kushirikiana na NETWAS Tanzania Ltd
wakati mkataba na kampuni hiyo ulikuwa ni wa malipo ya $303,375.04 (shilingi milioni 485 tu).
Malipo hayo ya ziada ni sawa na asilimia 212 ya gharama zilikubaliwa awali za mkataba huo.
Wakaguzi wamebaini ukiukwaji mkubwa wa taratibu rasmi za manunuzi, utunzaji wa kumbukumbu
za fedha na ufuatiliaji kwenye miradi mbalimbali ya maji. Hii ni pamoja na kutokuwepo kwa nyaraka
muhimu za malipo, malipo ya pesa nyingi zaidi kuliko zilizokubaliwa kwenye mikataba ya miradi ya maji,
matumizi mabaya ya pesa na kutokuwepo kwa wakaguzi wa ndani.
Baadhi ya matumizi kwenye miradi ya maji nchini inayoratibiwa na wizara hiyo yameonekana kuwa ni
zaidi ya pesa zilizotengwa kwenye bajeti, huku pesa nyingine zikitumiwa kwenye miradi ambayo
haikulengwa kutekelezwa.
"Wizara ya Maji na Umwagiliaji inatakiwa kutengeneza utaratibu mzuri wa kufuatilia na kuweka rekodi
ya pesa zote zinazotumwa kwenye mamlaka za serikali za mitaa," ilisema sehemu ya ripoti hiyo ambayo
KuliKoni imepata nakala yake.
Ofisi ya CAG imetoa maagizo kwa wizara hiyo kuhakikisha kuwa manunuzi yote yanafanywa kulingana
na pesa na miradi iliyowekwa kwenye mipango rasmi ya manunuzi.
Maafisa wa serikali wameiambia Kulikoni kuwa baadhi ya nchi na mashirika ya kimataifa ambayo
yamekuwa yakitoa misaada na mikopo kwenye sekta ya maji hapa nchini yamesitisha misaada yake
kwa Tanzania, huku na mengine yakitishia kuzuia misaada kutokana na tuhuma za ubadhirifu wa pesa
kwenye miradi ya maji.
* Mabilioni ya pesa za walipa kodi yayeyuka
* Kashfa kwenye ununuzi wa mashangingi 68
* Wafadhili watishia kuzuia misaada yao
WIZARA ya Maji na Umwagiliaji imekumbwa na kashfa kubwa baada ya ukaguzi maalumu
uliofanywa kwenye miradi ya maji nchi nzima kubaini tuhuma za ufisadi, uzembe wa maofisa
na matumizi mabaya ya mabilioni ya shilingi kwenye wizara hiyo.
Ukaguzi maalumu (special audit) uliofanywa na Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu
za Serikali (CAG) kwenye programu ya maendeleo ya sekta ya maji (2007-2010) umebaini
malipo mengi ya utata kwenye miradi ya maji nchini na matumizi mabaya ya pesa za umma.
Katika moja ya tuhuma hizo za ufisadi, Wizara ya Maji na Umwagiliaji imebainika kutumia zaidi
ya dola za Marekani milioni 39 (takribani shilingi bilioni 63) kwenye mazingira ya utata bila
kuzingatia miradi iliyopo kwenye mpango kazi wa mwaka wa wizara hiyo.
"Shughuli za manunuzi ndani ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji hazifanywi kuendana na mpango
wa manunuzi wa kila mwaka," imesema sehemu hiyo ya ripoti mpya ya CAG kutokana na ukaguzi
uliofanywa Septemba mwaka jana.
Pia ukaguzi huo umebaini kashfa kwenye ununuzi wa mashangingi (Toyota Land Cruiser) yapatayo 68
uliofanyika mwaka 2009 kwa Yen za Japan milioni 235.4 (zaidi ya shilingi bilioni 5) kinyume na utaratibu
rasmi wa manunuzi ndani ya serikali.
Kwa mujibu wa wakaguzi wa ofisi ya CAG, ununuzi huo wa mashangingi bila kufuata taratibu za serikali
umeisababishia wizara hasara ya zaidi ya shilingi milioni 218 kutokana na tofauti ya viwango vya
ubadilishaji wa pesa za kigeni.
Wizara hiyo imebainika kutokuwa na ufuatiliaji wa karibu wa pesa za miradi ya maji zinazopelekwa
nchi nzima kwenye mamlaka za serikali za mitaa na hivyo basi kutojua kama pesa hizo zimetumiwa
kwenye matumizi sahihi ama la.
Wizara hiyo pia imekumbwa na kashfa ya matumizi makubwa ya pesa kwenye miradi mbalimbali ya
maji kuliko gharama halisi za awali zilizokubaliwa kwenye miradi hiyo.
Mifano hiyo ni pamoja na mradi wa ujenzi wa Bwawa la Matwiga ambapo wakati mkataba wa awali
ulisema kuwa mradi utagharimu dola za Marekani 284,693, wizara hiyo iliongeza malipo ya ziada
kwenye mradi huo ya dola 80,615 (wastani wa shilingi milioni 129).
Kwenye mradi wa Mpwapwa na Utete, wizara ilitumia dola za Marekani 32,250 zaidi ya gharama
halisi ya mradi huo kwenye mkataba wa ujenzi ambayo ilikuwa ni $39,600.
Mamlaka ya Maji Safi na Taka ya Moshi nayo ilitumia $947,757.53 (shilingi bilioni 1.5) kuilipa
kampuni ya Seureca Consulting Egineers ya Ufaransa kushirikiana na NETWAS Tanzania Ltd
wakati mkataba na kampuni hiyo ulikuwa ni wa malipo ya $303,375.04 (shilingi milioni 485 tu).
Malipo hayo ya ziada ni sawa na asilimia 212 ya gharama zilikubaliwa awali za mkataba huo.
Wakaguzi wamebaini ukiukwaji mkubwa wa taratibu rasmi za manunuzi, utunzaji wa kumbukumbu
za fedha na ufuatiliaji kwenye miradi mbalimbali ya maji. Hii ni pamoja na kutokuwepo kwa nyaraka
muhimu za malipo, malipo ya pesa nyingi zaidi kuliko zilizokubaliwa kwenye mikataba ya miradi ya maji,
matumizi mabaya ya pesa na kutokuwepo kwa wakaguzi wa ndani.
Baadhi ya matumizi kwenye miradi ya maji nchini inayoratibiwa na wizara hiyo yameonekana kuwa ni
zaidi ya pesa zilizotengwa kwenye bajeti, huku pesa nyingine zikitumiwa kwenye miradi ambayo
haikulengwa kutekelezwa.
"Wizara ya Maji na Umwagiliaji inatakiwa kutengeneza utaratibu mzuri wa kufuatilia na kuweka rekodi
ya pesa zote zinazotumwa kwenye mamlaka za serikali za mitaa," ilisema sehemu ya ripoti hiyo ambayo
KuliKoni imepata nakala yake.
Ofisi ya CAG imetoa maagizo kwa wizara hiyo kuhakikisha kuwa manunuzi yote yanafanywa kulingana
na pesa na miradi iliyowekwa kwenye mipango rasmi ya manunuzi.
Maafisa wa serikali wameiambia Kulikoni kuwa baadhi ya nchi na mashirika ya kimataifa ambayo
yamekuwa yakitoa misaada na mikopo kwenye sekta ya maji hapa nchini yamesitisha misaada yake
kwa Tanzania, huku na mengine yakitishia kuzuia misaada kutokana na tuhuma za ubadhirifu wa pesa
kwenye miradi ya maji.