Ufafanuzi wa Waziri Mkuu MAJALIWA na yaliyofanywa na Mhe. Rais kwa watumishi wa Umma Nchini

Jun 4, 2022
68
184
38850454_101.jpg

Ufafanuzi wa kina uliotolewa na Waziri Mkuu kuhusu nyongeza ya Mishahara ya asilimia 23.3 na mambo yaliyofanywa mpaka sasa na Rais Samia kwa watumishi wa umma;

1. Nyongeza ya mshahara kwa asilimia 23.3 kwa watumishi wa umma kulingana na madaraja huku kipaumbele kikiwa kwa wenye mishahara midogo.

2. Kupunguza kodi(PAYE) kwa kuifikisha 8% na kupandisha kiwango cha chini cha kukatwa kodi, suala hili lilipoteza kiwango cha takribani Bilioni 14 ya fedha zilizopaswa kukusanywa na serikali.

3. Katika mifuko ya hifadhi ya jamii kupandisha kiwanga cha malipo ya mkupuo kwa kufikia asilimia 33 kutoka 25% iliyokataliwa na wadau mwaka 2018.

4. Kupandishwa madaraja WATUMISHI laki moja tisini elfu na miatano sitini na mbili~ 190,562 (Kwa wasioelewa, hii imeigharimu Serikali kiasi cha takribani TZS BILIONI 39.6).

5. Taasisi zote zenye uhitaji wa wafanyakazi kupewa vibali vya ajira mpya na kutolewa vibali kwa watumishi walioomba kubadilisha vituo na kwenda kuongeza taaluma kwa mujibu wa taratibu na sheria za utumishi wa umma.

6. Kuanzia Mwezi March 2021 hadi January 2022, Rais Samia amewezesha ulipwaji wa madeni na malimbikizo ya watumishi wa umma wapatao 65,391, madeni yenye thamani ya takribani TZS BILIONI 90.7.

7. Kuondolewa kwa mzigo wa tozo ya 6%(VALUE RETENTION FEE) kwa watumishi waliokuwa wanufaika wa mikopo ya Elimu ya juu (HESLB). Kiwango hiki cha 6% kimekuwa mzigo mzito kwa watumishi hususani vijana wanaotoka Vyuo Vikuu, Rais Samia atakumbukwa sana kwa hili.

8. Kuboreshwa kwa mazingira ya kazi ya watumishi. Hii inatupa hamasa watumishi kutoa huduma bora na kuhakikisha wananchi wanapewa wanachostahiri.

Itoshe kusema kwamba Rais Samia Suluhu Hassan ameweka rekodi ya aina yake kama Mkuu wa nchi anayejali watumishi wa umma. Tumuunge mkono azidi kuijenga Tanzania yetu.

#SisiTumekubali #Kaziinafanyika
 
Rais Samia amefanya mengi makubwa,yaliyowashinda watangulizi wake, tena ndani ya muda mfupi.

Mimi sitamsahau,aishi miaka mingi.
 
Amenisuru kwenye deni la bodi ya mikopo,na daraja nimepanda,namshukuru sana.
Hili la nyongeza linamtia doa,ameongozwa vibaya,ajipange!
 
View attachment 2308396
Ufafanuzi wa kina uliotolewa na Waziri Mkuu kuhusu nyongeza ya Mishahara ya asilimia 23.3 na mambo yaliyofanywa mpaka sasa na Rais Samia kwa watumishi wa umma;

1. Nyongeza ya mshahara kwa asilimia 23.3 kwa watumishi wa umma kulingana na madaraja huku kipaumbele kikiwa kwa wenye mishahara midogo.

2. Kupunguza kodi(PAYE) kwa kuifikisha 8% na kupandisha kiwango cha chini cha kukatwa kodi, suala hili lilipoteza kiwango cha takribani Bilioni 14 ya fedha zilizopaswa kukusanywa na serikali.

3. Katika mifuko ya hifadhi ya jamii kupandisha kiwanga cha malipo ya mkupuo kwa kufikia asilimia 33 kutoka 25% iliyokataliwa na wadau mwaka 2018.

4. Kupandishwa madaraja WATUMISHI laki moja tisini elfu na miatano sitini na mbili~ 190,562 (Kwa wasioelewa, hii imeigharimu Serikali kiasi cha takribani TZS BILIONI 39.6).

5. Taasisi zote zenye uhitaji wa wafanyakazi kupewa vibali vya ajira mpya na kutolewa vibali kwa watumishi walioomba kubadilisha vituo na kwenda kuongeza taaluma kwa mujibu wa taratibu na sheria za utumishi wa umma.

6. Kuanzia Mwezi March 2021 hadi January 2022, Rais Samia amewezesha ulipwaji wa madeni na malimbikizo ya watumishi wa umma wapatao 65,391, madeni yenye thamani ya takribani TZS BILIONI 90.7.

7. Kuondolewa kwa mzigo wa tozo ya 6%(VALUE RETENTION FEE) kwa watumishi waliokuwa wanufaika wa mikopo ya Elimu ya juu (HESLB). Kiwango hiki cha 6% kimekuwa mzigo mzito kwa watumishi hususani vijana wanaotoka Vyuo Vikuu, Rais Samia atakumbukwa sana kwa hili.

8. Kuboreshwa kwa mazingira ya kazi ya watumishi. Hii inatupa hamasa watumishi kutoa huduma bora na kuhakikisha wananchi wanapewa wanachostahiri.

Itoshe kusema kwamba Rais Samia Suluhu Hassan ameweka rekodi ya aina yake kama Mkuu wa nchi anayejali watumishi wa umma. Tumuunge mkono azidi kuijenga Tanzania yetu.

#SisiTumekubali #Kaziinafanyika
huu usanii cjui utaisha lini hapa tanzania.PAYE pamoja na kujigamba imepunguzwa lkn bado ni kubwa mno mfano kama mshahara wako 1,940,000 kodi pekee ni 363,262.21 sasa hapo kuna nafuu gani.bado bima 3%,vyama vya wafanyakazi wanalamba achilia mbalii PSSSF au NSSSF sababu angalau hiyo ni pesa yako.sasa kwa nn hata wa kima cha chini hajapewa hata hiyo 23.23%.wafanyakazi jiondoeni kwenye vyama vya wafanyakazi muanze upya hao viongozi na ccm ni kidole na pete.
 
Back
Top Bottom