Boniphace Kichonge
JF-Expert Member
- Jul 31, 2017
- 1,605
- 1,958
Wapendwa WanaJF
Katika kitabu cha ufunuo 5:1-14 imeweka bayana kuhusu Mungu na kufunua uongo wa ile nadharia inayodai kuwa Baba ndiye Huyo huyo Mwana na kwamba ndiye huyohuyo Roho. Kitabu cha Ufunuo kimeweka Bayana kuwa Baba na Mwana ni wawili tofauti na kwamba sii Mtu Mmoja. Baba sii Mwana na Mwana sii Baba. Baba na Mwana ni nafsi Mbili tofauti zilizo Umoja. Katika Ufu5:1-5 Biblia inamfunua Mungu Baba akiwa ameketi katika Kiti cha Enzi akiwa ameshikilia Kitabu ambacho kimeandikwa ndani na nyuma na kimetiwa Muhuri saba. Katika Kitabu cha Ufu5:6-7 tunamwona Yesu akiwa anawakilishwa na Mwanakondoo aliyechinjwa na kisha akamwendea Mungu Baba, na akakitwaa kile kitabu kilichoko Mkononi mwake na kuvunja Muhuri zake.
Kama Baba ndo huyohuyo Mwana kama baadhi ya watu wanavyo sema haiingii akilini kwamba Baba ameketi kitini pa enzi, halafu huyohuyo ajiendee Mwenyewe na kukitwaa kitabu ambacho kiko katika Mkono ambao ni wa kwake Mwenyewe!!! Lazima Baba na Mwana wawe ni nafsi Mbili tofauti kabisa. Lakini pia Ufunuo sura ya tano inawapinga wale wanaodai kuwa Imetupasa kumwabudu Baba pekee na sii Mwana, na kudai kuwa ni dhambi kumwabudu Mwana. Ufunuo sura ya tano imeweka bayana kuwa Wote Baba na Mwana wanaabudiwa na viumbe vyote vya Mbinguni na kwamba Mwana anayo haki sawa ya Kuabudiwa kama Baba. Yesu kama Mwana wa Mungu, ana haki ya kustahili Ibada na kusujudiwa kama vile Baba yake wa Mbinguni. Biblia yasema hivi: “Na kila kiumbe kilichoko mbinguni na juu ya nchi na chini ya nchi ya juu ya bahari, na vitu vyote vilivyomo ndani yake, nalivisikia, vikisema, Baraka na heshima na utukufu na uweza una yeye aketiye juu ya kiti cha enzi, na yeye Mwana-Kondoo, hata milele na milele. Na wale wenye uhai wanne wakasema, Amina. Na wale wazee wakaanguka, wakasujudu. [Ufu5:13-14]
Katika kitabu cha ufunuo5:6 Kristo amefunuliwa kama Mwanakondoo mwenye Macho saba na macho saba yamefananuliwa kuwa ni Roho saba za Mungu ambazo zimetumwa dunia yote. Kulingana na Kitabu cha Ufunuo Roho Mtakatifu ni Macho ya Mwanakondoo. Macho huwa ni viungo na sehemu ya mnyama hivyo Roho Mtakatifu ni Roho ya Mungu na Roho ya Yesu. Roho Mtakatifu anamilikiwa na Mungu pamoja na Kristo na ambaye hutumwa na Mungu na Kristo dunia yote ili kumwakilisha Mungu na Kristo na kuwafanya Mungu na Kristo waweze kuwepo kila Mahali. Lakini pia tunaona katika kitabu cha Ufunuo kuwa Roho Mtakatifu ni Roho ambayo hutoka kwa Mungu na hutumwa kama mjumbe huru na anayejitegemea mbali na Baba na Mwana. Ingawa Roho sii Mtu mwingine ama Mungu mwingine aliye tofauti na Mungu na Kristo bali ni Roho yao, lakini Mungu anaweza kuituma Roho yake kama Mjumbe huru na ambaye anajitegemea Mwenyewe.
Karibuni kwa maoni
Mbarikiwe sana
Katika kitabu cha ufunuo 5:1-14 imeweka bayana kuhusu Mungu na kufunua uongo wa ile nadharia inayodai kuwa Baba ndiye Huyo huyo Mwana na kwamba ndiye huyohuyo Roho. Kitabu cha Ufunuo kimeweka Bayana kuwa Baba na Mwana ni wawili tofauti na kwamba sii Mtu Mmoja. Baba sii Mwana na Mwana sii Baba. Baba na Mwana ni nafsi Mbili tofauti zilizo Umoja. Katika Ufu5:1-5 Biblia inamfunua Mungu Baba akiwa ameketi katika Kiti cha Enzi akiwa ameshikilia Kitabu ambacho kimeandikwa ndani na nyuma na kimetiwa Muhuri saba. Katika Kitabu cha Ufu5:6-7 tunamwona Yesu akiwa anawakilishwa na Mwanakondoo aliyechinjwa na kisha akamwendea Mungu Baba, na akakitwaa kile kitabu kilichoko Mkononi mwake na kuvunja Muhuri zake.
Kama Baba ndo huyohuyo Mwana kama baadhi ya watu wanavyo sema haiingii akilini kwamba Baba ameketi kitini pa enzi, halafu huyohuyo ajiendee Mwenyewe na kukitwaa kitabu ambacho kiko katika Mkono ambao ni wa kwake Mwenyewe!!! Lazima Baba na Mwana wawe ni nafsi Mbili tofauti kabisa. Lakini pia Ufunuo sura ya tano inawapinga wale wanaodai kuwa Imetupasa kumwabudu Baba pekee na sii Mwana, na kudai kuwa ni dhambi kumwabudu Mwana. Ufunuo sura ya tano imeweka bayana kuwa Wote Baba na Mwana wanaabudiwa na viumbe vyote vya Mbinguni na kwamba Mwana anayo haki sawa ya Kuabudiwa kama Baba. Yesu kama Mwana wa Mungu, ana haki ya kustahili Ibada na kusujudiwa kama vile Baba yake wa Mbinguni. Biblia yasema hivi: “Na kila kiumbe kilichoko mbinguni na juu ya nchi na chini ya nchi ya juu ya bahari, na vitu vyote vilivyomo ndani yake, nalivisikia, vikisema, Baraka na heshima na utukufu na uweza una yeye aketiye juu ya kiti cha enzi, na yeye Mwana-Kondoo, hata milele na milele. Na wale wenye uhai wanne wakasema, Amina. Na wale wazee wakaanguka, wakasujudu. [Ufu5:13-14]
Katika kitabu cha ufunuo5:6 Kristo amefunuliwa kama Mwanakondoo mwenye Macho saba na macho saba yamefananuliwa kuwa ni Roho saba za Mungu ambazo zimetumwa dunia yote. Kulingana na Kitabu cha Ufunuo Roho Mtakatifu ni Macho ya Mwanakondoo. Macho huwa ni viungo na sehemu ya mnyama hivyo Roho Mtakatifu ni Roho ya Mungu na Roho ya Yesu. Roho Mtakatifu anamilikiwa na Mungu pamoja na Kristo na ambaye hutumwa na Mungu na Kristo dunia yote ili kumwakilisha Mungu na Kristo na kuwafanya Mungu na Kristo waweze kuwepo kila Mahali. Lakini pia tunaona katika kitabu cha Ufunuo kuwa Roho Mtakatifu ni Roho ambayo hutoka kwa Mungu na hutumwa kama mjumbe huru na anayejitegemea mbali na Baba na Mwana. Ingawa Roho sii Mtu mwingine ama Mungu mwingine aliye tofauti na Mungu na Kristo bali ni Roho yao, lakini Mungu anaweza kuituma Roho yake kama Mjumbe huru na ambaye anajitegemea Mwenyewe.
Karibuni kwa maoni
Mbarikiwe sana