Droo ya Klabu Bingwa Ulaya kwa msimu wa mwaka 2021-22 inachezeshwa leo huko Instanbul, Uturuki kuanzia majira ya saa 5pm (BST) au saa 1 jioni (Saa za Afrika Mashariki)
Timu 32 zitashiriki katika kupangiwa makundi, 26 zikiwa zimepita moja kwa moja na nyingine 6 zikitokea katika play-offs
Tumu zitapangwa katika makundi 8 yenye timu 4. Upangaji huo utatokana na makundi manne (Pots) yaliyowekwa sasa kabla ya upangaji.
Timu zinazotoka katika nchi moja hazitaweza kukutana katika hatua hii ya makundi
View attachment 1909236
Pot 1 ina jumuisha Bingwa wa UEFA, EUROPA na Bingwa wa kila Ligi katika nchi 6. Pot 2, 3, 4 inajumuisha timu zilizopangwa kutokana na nafasi zao katika viwango vya UEFA