UDSM kunani hapo?

..hayo ya kusoma huku mkifanya vibarua ndio maana kamwe hamvumbui....mtabaki hivyo hivyo....mfano muulize mkuu wako wa nchi PhD yake ya chemistry ameipa heshima gani??...zaidi ya kuiweka kapuni na kuingia kwenye siasa....viongozi wenu bongo wanaojiita wasomi wa Chuo ni reflection tosha ya namna wabongo wanavyotumia elimu zao hovyo.....kwaheri...

 
Huna exposure wewe
Watu wanasoma na kazi wanafanya ili kumudu life, sio UDSM peke yake hata uende Ulaya hilo linafanyika mkuu.

Chuo hakuna msuli wa kukesha kama advanced level

Kule ukiwa vizuri upstairs basi unaweza fanya kazi plus kusoma na hakuna tatizo.
Umalaya ni hulka ya mtu sio kwa sababu ya kusoma chuo
 
...exposure niliyonayo ndio inanifanya nione kuwa udsm ni Chuo feki ukilinganisha na vyuo vingine vya nje..hata ndani ya Africa...mfano nikuulize we unayejiita msomi...nipe list ya patents zilizotoka udsm kwa kipindi cha miaka 10 iliyopita....kama hujui...patents ni hati miliki ya innovation....si tu kwenye science bali hata huko kwenye fine arts unakosema udsm wanajirusha japo ni vichwa....nipe list ya patents....ama hata spin offs angalau tano tu toka udsm kwa kindi tajwa...

...we umesema sina exposure...sasa we graduate wa udsm tetea chuo chako nipe jibu la hayo juu....ili nisiendelee kuwaona nyie watu wa vitu vidogo...zikiwemo siasa vyuoni na starehe..



 
Innovation zipo japo siwezi kukupa na huwezi kuwalaumu wanafunzi wala graduate katika hili kwa 100%
Ukitaka innovation uliza serikali yako kwanini inawakamata innovators wa kitaa? Ndo ujue nchi yako sio rafiki wa innovation usikimbilie kulaumu wanafunzi bure.
 
Kama ungechukua muda wako kidogo kuelewa dhumuni mleta uzi nadhani majibu yako yangekuwa tofauti na ulicho andika.

Sio lazima kubomoa miundombinu iliyopo hapana ila cha msingi ni kutengeneza mazingira ya kuendana na wakati tuliopo.
Makerere ni chuo ambacho kina umri mkubwa kuliko udsm lakini wanaenda na wakata, University of Nairobi hapo jirani ukifika pale unajiskia kweli you are in an academic arena.

Wenzetu wanajaribu ku~keep up with the pace sisi tunabaki nyuma.
We need to do some restructuring of our infrustructures while at the same time maintaining the status quo of our udsm.
 
Nilitegemea baada ya kumponda huyo Jamaa kuwa amekosea kuielezea UDSM basi Wewe mwana UDSM kindakindaki sasa ungetuelezea sisi tusioijua hiyo UDSM yako ili tufahamu mengi juu yake. Otherwise hata Wewe nimekuona ni mpita njia vile vile wa hapo UDSM.
Naam.
Siku zote hakuna kitu kizuri kama kupinga hoja kwa "HOJA ILIYOSHIBA' badala ya kupinga hoja bila maelezo hata ya kuzugia
 
Wewe ni punguani. Sio kujenga mapya tu. Waboreshe hata hayo yaliyopo. Kama hawana pesa wachangishe tufanye harambee ya pesa za rangi za majengo. Acha kujitoa ufahamu. Unapenda kuiangalia picha ya mkuu wa chuo kwenye website au sio? Sasa mtu wa nchi za mbali unamuwekea picha ya nini? Please take a chill pill and relax.
 
Chuo kizima hakina hata wifi, kwa dunia ya leo ya sayansi na teknolojia bila internet ni sawa na bure.
Jordan university college ya hapa morogoro tunaenjoy wi-fi ya bure. Nashangaa UDSM kama hakuna basi ni tatizo.
 
Sasa kama wao wamefanya Sisi inatuhusu nini ? Kila watu na vipaumbele vyao, Makerere na mambo yao, Sisi tunajenga viwanda kenya wapo bize na reli, Uganda wapo bize na besigye
 
Sasa kama wao wamefanya Sisi inatuhusu nini ? Kila watu na vipaumbele vyao, Makerere na mambo yao, Sisi tunajenga viwanda kenya wapo bize na reli, Uganda wapo bize na besigye
Tunajenga viwanda....!?
Toka tulivyo ambiwa sasa tunataka Tanzania ya viwanda tumefika wapi?

Well ni kweli kila nchi ina vipaumbele vyake lakini pia usisahau kwamba vyuo vikuu ndio chimbuko la maendeleo au mawazo ya maendeleo (THINK TANKS) ndio maana kipindi cha Mwalimu Nyerere alipenda sana kwenda hapo mlimani kuzungumza na kubalishana mawazo na wanazuoni.

Sio kwamba alikuwa anajiskia tu kwenda huko ila alijua kwa kufanya hivyo atapata mawazo endelevu.
So niseme tu kwamba hivyo viwanda tunavyo vihitaji sana wataalamu wake watatoka kwenye vyuo vyetu ikiwemo udsm ili kukuza ajira za ndani.

Otherwise unapotegemea kuwa utajenga viwanda bila ya wataalamu wako wa ndani kwa kushindwa kuweka mazingira ya vyuo sawa utakuwa unawatengenezea watu/wataalam wa nje nafasi za ajira na sio watu wako.

Hivyo badala ya kuwa Tanzania ya viwanda tutajikuta tunakuwa Tanzania ya vi~wonder.
 
..huna hoja....
 
...alafu utashangaa vyuo hivi vyenye angalau ujaribu kwenye science & tech ndio vinavyofungiwa kila kukicha....huko udsm wanaojiita ma genius hatuoni products zaidi ya blah blah... Wanakaririshana mitihani wanamaliza na vyeti vizuri huku kichwani hamna kitu zaidi ya siasa.... Pathetic...


Jordan university college ya hapa morogoro tunaenjoy wi-fi ya bure. Nashangaa UDSM kama hakuna basi ni tatizo.
 
Wakati mwingine huwa nawashangaa watu wengine, mtu anafikili akisoma chuo flani basi kikikosolewa au kushauriwa anakuja juu kama vile chuo hicho ni cha baba yake. vyuo vyote vya serikali vinaendeshwa kwa kodi za watanzania wote hivyo kila mtu ana haki ya kushauri na kukosoa pale anapoona mambo hayaendi sawa. Ukweli utabaki kuwa vyuo vyetu vimebaki tu na majina lakini kitaaluma viko nyuma sana. Siku kadhaa zilizopita nilikuwa naongea na mhadhiri mmoja wa chuo hicho (UDSM) na mjadala wetu ulikuwa ni juuu ya matumizi ya technolojia katika chuo hicho. Nilishangaa kusikia kwamba katika karne hii kuna wanafunzi wanasoma na kuhitimu masters za hesabu bila kutumia soft ware package hata moja. kizazi hiki kuna wahadhiri bado wanataka mtu afanye hesabu kwa peni na karatasi? Nkashangaa ananiambia kuwa kuna watu pale kwenye mathematics departiment wanapinga wanafunzi wa kusoma programming. hivi ulimwengu huu bado watu wanafikili matumizi ya computer ni kuangalizia? eti inamsaidia mwanafunzi kufanya maswali?. Huu ni utani kabisa. Tumekwenda vyuo vya watu tukaishia kuonekana vilaza kwasababu tulisoma mambo mengi yaliyopitwa na wakati. Inakuhitaji kuwa na akili finyu kufikili kwamba tunachopewa kwenye hivi vyuo vyetu kama kinaweza kutusaidia kujikomboa. Bado tuna vyuo ambavyo wahadhiri ni miungu watu, huwezi kumchalenge professor labda kama unataka udisco. Basi tu acha tuendelee kupeana moyo eti tuna vyuo vikuu lakini ukweli ni kwamba tuko nyuma ya wakati.
 
Magufuli anabadilisha UDSM bavicha wanamponda
 
mkuu hayo ulosema sawa ila na camera yako inachangia mkuu
 
Alafu pia na huu utaratibu na ukiritimba Masters programmes wanafunzi with no reasons wanasota miaka mitatu plus, wakati Vyuo vingi Duniani wanajikita kutoa Masters programmes kwa mwaka mmoja wao wanaona raha kuchelewesha wanafunzi.

Mambo ya ajabu kabisa.
 
Watanzania aise, hawakubali mabadiliko, jamaa ameshauri lkn kupokea ushauri wake ni kazi, tutaendelea kweli namna hii. Maisha ya kitamaduni ya jamii tulizotoka ni shida, ndiyo yanayotuathiri. Chukuweni ushauri kama unafaa!
kila kitu siasa hapo hawakawii kusema we mleta mada huiwezi ccm yetu kaa huko na chadema yako. Sababu kubwa ya kupinga mi zaidi ya hiyo siioni.
 
hawa wakuu wa vyuo vyetu wamesoma elimu ya zamani, elimu zao na mindsets zao zipo outdated, mbaya zaidi wapo rigid hawataki kujiupdate pamoja na kuwa dunia imebadilika sana. Wapo miaka 50 nyuma.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…