UDSM kunani hapo?

Chuo kizima hakina hata wifi, kwa dunia ya leo ya sayansi na teknolojia bila internet ni sawa na bure.
Udbs ipo acha uongo
 
sikatai ukosoaji wako,
website mbovu nakubali, miundombinu ya miaka ya 70 haiwezi kuendana na mahitaji ya sasa hata kidogo.
unapaswa kufahamu idadi ya wanafunzi imeongezeka maradufu ukilinganisha na facilities zilizopo.

Kwa hiyo hatukujua kama idadi itaongezeka seriously?
 

Kinaongoza kwa facilities ama academic results?
 
Ni kweli UDSM tuna madhaifu fulani lakini si kwa kiwango hicho cha mtoa mada hajui kuwa serikali ingewekeza UDSm tu basi yeye leo hii angekuwa na certicate yake / Diploma mana Chuo chake cha UDOM kisingejengwa na matokeo yake ungeishia diploma mana sifa za kusoma UDSM hakuwa nazo
 
Labda upo outdated, naomba link ya hiyo no.13
 
My friend, I am very updated, naomba link ya hiyo no.13.
Forget history!
 
Wapo busy na siasa hapo hakuna anayekuja na mawazo mbadala waache wasubilie teuzi za Mkulu
 
Kitaaluma sahau kimajengo sawa tatizo la udom walicopy everything from Udsm afu strength ya Udsm wanafunzi waliopass sana ndo wanachaguliwa tofauti na udom
Suala sio kusahau, suala is how you maintain your ability and consistently excell
Mimi kama mtanzania napenda kuona vyuo vinachuana kwa ubora wa elimu, nataka kuona UDSM inapewa challenge na SAUT, hapo ndio the sleeping monsters like udsm, sua and the like will realize how things change. Hata ukiwa mwalimu Huwezi kuwa na darasa ambalo mwanafunzi mmoja huwa ni wa kwanza kila mtihani halafu ukajisifu!
 
Bro nimesoma O'leve na A'level kwa ufaulu wa juu kabisa, na A'level nilsoma PCB.
 
Unaweza kuwa na nia nzuri lakini attitude yako ikaharibu. Unaponda kuwa hawana library na maabara huku unawapongeza wachina. Unawezaje kuwapongeza wachina kwa kuijengea UDSM library ya kisasa lakini ukabeza wanaUD kwamba hawana mipango wala hawafanyi juhudi yoyote kuboresha chuo? Hivi wachina walitoka huko kwao wakaenda UD kuwaambia wanawapenda sana hivyo wameamua kuwajengea library? UD ilitambua kabla yako kuwa inahitaji library na maabara za kisasa na iliweka mipango ya kuwa nazo na ikaweka mikakati, ikafanya juhudi ya kutafuta fedha, ikapatikana fursa ya hao wachina. Unampongeza mtekelezaji wa mpango halafu unamponda aliyepanga!

Kuhusu uchafu wa mazingira umewasingizia. Ni kweli chuo si kirembo kivile ila si kichafu. Mazingira yake ya asili yanatunzwa vizuri hata ngedere wanajimwayamwaya. Sitegemei wapotezee kwenye "beautification" hela ambayo hata hivyo haipo wakati kuna changamoto kubwa zaidi zinahitaji fedha. Changamoto ya uchakavu wa miundo mbinu ipo na wanajua ndo maana kuna mabweni hayana wanafunzi ili kupisha ukarabati. Ukiweza kuushirikisha uongozi namna ya kupata fedha zaidi naamini utabarikiwa kwa sababu hiyo ndo changamoto kubwa. Kuwa na mainjinia na wataalamu wengi si kigezo pekee. Utaalamu unahitaji mipango na fedha ili utoke kwenye karatasi uhamie kwenye uhalisia. Halafu jengo la utawala na Nkrumah si chakavu hata kidogo. Ule muonekano wa zege ndo ulikuwa hivyo toka mwanzo na utaendelea kuwa hivyo hivyo. Rangi zinapigwa kwenye hayo majengo mengine mapya.
 
Na hizo Hall 2 & 5 bado zinatumika tu? Tuombe Mungu aepushe makuu
 
kuna jamaa yangu aliwahi kwenda uholanzi baada ya kumaliza degree ya banking& finance pale IFM.Alipofika kule akaomba kazi na alipoenda kwenye interview akaonyesha cheti chake cha Ifm.Jamaa wakamjibu palepale kwamba hawakitambui hicho chuo wao kwa East Africa wanavitambua vyuo vitatu tu University of Makerere,UDSM na University of Nairobi kwahiyo jamaa akakosa kazi.

Tuache ushabiki wala nini UDSM kitaendelea kuwa amongst the best universities in Africa and international wise. Angalia kilivyokua na hazina kubwa ya wataalamu maprofesa,wahadhiri.

Kupata udahili UDSM inabidi uwe na first au second division.Licha ya TCU kuanzisha mfumo wa udahili wa pamoja kwa vyuo vyote yaani CAS Central Admission System bado vigezo vya kuchaguliwa kusoma UDSM ndio vigumu na vitaendelea kuwa hivyo kuliko vyuo vyote Tanzania kwa sababu hicho ndio chuo bora na kikongwe kuliko vyote.

Proudly to be UDSM alumni
 
Serikali lazima ichukue hatua ili kukifanya Chuo hiki kibebe heshima ya kuitwa chuo cha taifa.

Naipongeze serikali kwa kuanza kujenga maktaba kubwa ya kisasa Afrika ya mashariki na Kati.
 
Na swala la usalama ni Tatizo, hawa auxiliary police kazi yao ni kupambana na wrong packing, na kula rushwa pindi wakikamata watu wakivunja sheria, hawa auxiliary police wa UDSM ni uozo hawajui sheria, mwenendo wao ni wa jazba jazba tu, ikifika saa sita usiku tu unakuta wameshakimbia vituo vya kazi, maskini wanafunzi wa pale wanajilinda wenyewe, poor them!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…