VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,140
- 18,004
Kati ya waliokuwa makada waandamizi wa CCM waliokataa waziwazi,kwa maneno,ujio wa katiba mpya alikuwa ni Edward Ngoyai Lowassa. Alipofuatwa na waliokuwa Wajumbe wa Tume ya Jaji Warioba,Lowassa alitaka katiba mpya isubiri uchaguzi wa 2015.
Hoja na kivutio cha Lowassa kwenye katiba ya sasa ni Urais wenye nguvu. Aliiona katiba mpya kama chombo cha kuminya madaraka na mamlaka ya Rais. Alitamani kuwa Rais mwenye nguvu kubwa kikatiba. Kwa katiba ya sasa. Hakuitaka katiba mpya. Katiba mpya ikakwama kweli.
Lowassa akaukosa Urais wenye nguvu. Akaupata Mhe. Dr. J. P. Magufuli. Leo hii,Lowassa ni kati ya wanaoupinga Urais wenye nguvu. Wanauita udikteta. Ni mambo ya sizitaki mbichi hizi!
Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam
Hoja na kivutio cha Lowassa kwenye katiba ya sasa ni Urais wenye nguvu. Aliiona katiba mpya kama chombo cha kuminya madaraka na mamlaka ya Rais. Alitamani kuwa Rais mwenye nguvu kubwa kikatiba. Kwa katiba ya sasa. Hakuitaka katiba mpya. Katiba mpya ikakwama kweli.
Lowassa akaukosa Urais wenye nguvu. Akaupata Mhe. Dr. J. P. Magufuli. Leo hii,Lowassa ni kati ya wanaoupinga Urais wenye nguvu. Wanauita udikteta. Ni mambo ya sizitaki mbichi hizi!
Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam