leipzig
JF-Expert Member
- Jan 9, 2013
- 2,766
- 1,714
Katika utafiti nilioufanya yapata miaka miwili ilyopita niligundua kazi za udereva hasa mabasi na malori ya mizigo pamoja na upolisi zinamilikiwa na watu waliofeli darasa la saba,ukikuta ana elimu ya ziada basi atakuwa amejiendeleza akiwa kazini.
Kilichonisukuma kufanya utafiti huu ni pale nilipojiuliza ni kwa nini ajali zimekuwa nyingi hivi!nikagundua kuwa udereva ni taaluma mahsusi inayohitaji mtu mwenye elimu nzuri ya jiografia,fizikia na mahesabu.
Dereva anatakiwa alijue gari lake,uzito,mapungufu ya gari analoendesha,nguvu ya uvutano inayosababishwa na mwendo ktk kona,mabonde na milima nk, sasa kwa bahati mbaya watu waliopewa dhamana ya kuongoza nchi wanachukulia kazi hii ya udereva kama kazi ya daraja la chini afadhali ya housegirl.
Sasa unakuta dereva hajui mahesabu hayo na ndio maana tumeshuhudia ajali nyingi za kizembezembe na huku tunamuomba Mungu atuepushe pasipo sisi kuchukua hatua madhubuti.
Vile vile kazi ya upolisi,nakumbuka jamaa zangu wengi ambao hawakuwa wazuri darasana leo hii wengi wao ni mapolisi, sasa huwa najiuliza hivi hawajui kuwa mhalifu ni mtu mwenye maarifa ya ziada na hivyo polisi anatakiwa awe na maarifa kumzidi mhalifu? Leo hii tunashudia polisi anatumia nguvu zaidi kuliko maarifa katika kumhoji mtuhumiwa kiasi cha kumsababishia majeraha na ulemavu.
Kwa bahati nzuri nimetembelea nchi mbalimbali duniani hali ni tofauti sana,polisi anapokuwa anakuhoji hakugusi mwilini hata siku moja.
Naziasa mamlaka husika zijaribu kuangalia masuala haya kwa jicho pevu ili tuondokane na majanga haya ya ajali na uhalifu katika nchi yetu. NAWASILISHA
Kilichonisukuma kufanya utafiti huu ni pale nilipojiuliza ni kwa nini ajali zimekuwa nyingi hivi!nikagundua kuwa udereva ni taaluma mahsusi inayohitaji mtu mwenye elimu nzuri ya jiografia,fizikia na mahesabu.
Dereva anatakiwa alijue gari lake,uzito,mapungufu ya gari analoendesha,nguvu ya uvutano inayosababishwa na mwendo ktk kona,mabonde na milima nk, sasa kwa bahati mbaya watu waliopewa dhamana ya kuongoza nchi wanachukulia kazi hii ya udereva kama kazi ya daraja la chini afadhali ya housegirl.
Sasa unakuta dereva hajui mahesabu hayo na ndio maana tumeshuhudia ajali nyingi za kizembezembe na huku tunamuomba Mungu atuepushe pasipo sisi kuchukua hatua madhubuti.
Vile vile kazi ya upolisi,nakumbuka jamaa zangu wengi ambao hawakuwa wazuri darasana leo hii wengi wao ni mapolisi, sasa huwa najiuliza hivi hawajui kuwa mhalifu ni mtu mwenye maarifa ya ziada na hivyo polisi anatakiwa awe na maarifa kumzidi mhalifu? Leo hii tunashudia polisi anatumia nguvu zaidi kuliko maarifa katika kumhoji mtuhumiwa kiasi cha kumsababishia majeraha na ulemavu.
Kwa bahati nzuri nimetembelea nchi mbalimbali duniani hali ni tofauti sana,polisi anapokuwa anakuhoji hakugusi mwilini hata siku moja.
Naziasa mamlaka husika zijaribu kuangalia masuala haya kwa jicho pevu ili tuondokane na majanga haya ya ajali na uhalifu katika nchi yetu. NAWASILISHA