UDA waandika historia Dar

UDA waandika historia Dar

Wamiliki wa daladala wanauzana wao kwa wao.
Wameingia choo cha kike.We basi gani za Uda hazina Ruti maalum.
Hata Ulaya gari zote zina Ruti maalum na haibadiliki.
Ila Uda wao wanafanya wanavyotaka kwa amri ya dereva na utingo tu.Halafu eti wanasema wanafuata mifumo ya wenzetu.
UDA + DECI = Familia moja


Yote uliyosema ni mazuri, ila naomba sana msipende kulinganisha na Ulaya. Hapa sio Ulaya na wala hakuna sababu ya kufuata ya Ulaya tunapofanya ya kikwetu. Taja adhari za mfumo ili tuchangie kurekebisha kama zipo. Natumai ni vema kuangalia mazingira na mazingara ya mambo yenyewe ndipo tuone ni yapi yanalinganishwa na Ulaya na yapi ni ya kikwetu kwetu. Ulaya nao kabla ya kufikia hapa walikuwa na taabu taabu zao. Walivyozitatua ni kuangalia hali zao wakafikiria suluhisho, hawakujiuliza kwa mbona Afrika au Asia au marekani wanafanyaga hivi?
 
MAMLAKA ya Usafirishaji Majini na Nchi Kavu (Sumatra), imesema Shirika la Usafiri Dar es Salaam (UDA), kipindi hiki linawapa wakati mgumu kutokana na kushindwa kutii taratibu zilizowekwa barabarani.

Akizungumza na Tanzania Daima jijini Dar es Salaam jana, Ofisa Mfawidhi Sumatra Kanda ya Mashariki, Conrad Shio, alisema hadi sasa kuna mabasi ya UDA 150 ambayo yanafanya safari bila kusajiliwa na mengine ambayo yamesajiliwa, bado hayajapakwa rangi na kuwekwa vibao vinavyoonyesha yanakotoka na yanakokwenda.

Alisema mwitikio wa UDA kuweka rangi na vibao hivyo haupo huku makondakta nao wakikaidi kuvaa sare, sambamba na kukatisha njia.

"Bado tunasisitiza UDA zipakwe rangi na pia ziwekwe vibao ambavyo vinaonyesha sehemu zinakotoka na zinakokwenda, tunaomba UDA kufanya utaratibu unaofanywa na daladala ili kuweza kwenda sawa," alisisitiza Shio.

Aliongeza kuwa kwa sasa wana vikao vya mara kwa mara na UDA na siku za usoni muafaka utapatikana.

Alibainisha kuwa kwa wastani wamekuwa wakizikamata UDA tatu kwa siku na huzipiga faini kati ya sh. 150,000 na 250,000 kulingana na makosa husika.

Shio, alitoa wito kwa abiria kuendelea kutoa taarifa pale magari hayo yanapokatisha njia ama kupandisha nauli.

Alipotafutwa Msemaji wa UDA, George Maziku, alisema kwamba si kweli kuwa kuna mabasi yao 150 hayajasajiliwa na akahoji kama yapo kwanini washindwe kuyakamata.

Kuhusu sare, alisema madereva na makondakta wao wote wamepewa, ila kama ni suala la kutozivaa ni ukaidi wao wenyewe.

Kumekuwa na malalamiko kutoka kwa wananchi kutokana na jinsi UDA inavyofanya kazi zake, ikiwamo njia zake kutoeleweka, kukatisha njia na kutoza nauli kubwa.

Alimradi tu UDA wasikute wana ka-thread kwenye sheria kanakowalinda halafu Serikali/SUMATRA ikajikuta inakaanga mbuyu. UDA wamewahi kusema wana leseni ya Dar nzima na route yoyote. Hivyo ikifika maji shingoni wasije wakakatumia hako
 
Kumbe mabasi yaendayo kasi yatakua ndio haya haya ya UDA yalioko mitaani Tanzania bwana duh.!!!

Hilo sasa neno, maana wengine tulidhani yanaletwa aina fulani tofauti yenye muudo unaopatana na miundombinu uliyogharimu muda sana na feza nyingi. Alamsiki
 
Na mkuu wa mkoa na Waziri wanahusika nini na UDA kusaini mkataba huo na daladala? Au ni ujumbe wanataka kutupa
 
Unajua wakuu kuna issue hapa inatakl upigizwa ila Umoja wa Daladala hawajui.
Wameingia kichwa kichwa kuuza gari kwa Uda kwa mfumo wa wao kununua hisa bila kujua mpango wa UDA ilionao wa muda mrefu.
UDA ina Order na Tender ya Gari nyingi sana ambazo hazijaletwa nchini,na zimebaniwa huko kwa makusudi maalum.
Na ni gari kweli za Mwendo Kasi zile ndefu za kisasa kabisa.
Sasa target yao ya kuwahadaa wamiliki wa daladala ni kwamba wao watafanya kama walivyokubaliana ila ju kwamba itafika muda watawabana kwamba wanataka gari za mfumo mmooja,ambapo itawalazim gari hizo zitokea njiani zote zitafute chochoro kama ilivyo hizi Dungu.Watafakuwa nao kwa muda kama wa Miaka miwili tu lakini wajue kwamba watu wa daladala wamekwisha.Yaani no bora wangejiunga wao kwa wao wakawa washindani wa UDA.UDA kama haina mshindani ni kero ile ile tu.

Nyie subiri miaka kama miwili muone,UDA itakuwa chini ya wao 98% kwa kuleta Gari za kisasa baada ya kuikamata Biashara na watu kusahau.Inaitwa uwa kimya kimya
 
Mimi napenda wazawa wawezeshwe ila hii naipinga; kwanza tutafute wenye uwezo na ujuzi wa usafirishaji sio hawa wababaishaji full ajali
 
kumbe zabuni ya waendesha mradi wa dart wameshapewa uda ?!. kazi ipo.
 
Back
Top Bottom