UDA Scandal Files: Part I (Revealing)

Hata hivyo tumechoshwa na habari za skendo za rushwa. Hakuna muda wa kutosha wa kujadili watu wamepanga nini, wameiba sh ngapi n.k. Huu ni muda wa kujenga taifa letu changa lililokwama kwenye wimbi la umasikini.

Taifa haliwezi kujengwa kwa ufisadi ndo maana kila wakati ni lazima tufichue maovu! we unataka kuacha watu wale nchi alaf unataka utegemee kumaliza umaskini
 
Sasa hapa Simon Group wanahudhuria kama nani wakati hawajakabidhiwa rasmi na inakuwaje wakati bado kuna utata kuhusu malipo maana hata baadhi ya doccument alizotumia Simon Group ni forged?
wanamiliki hisa 52%
 
Hata hivyo tumechoshwa na habari za skendo za rushwa. Hakuna muda wa kutosha wa kujadili watu wamepanga nini, wameiba sh ngapi n.k. Huu ni muda wa kujenga taifa letu changa lililokwama kwenye wimbi la umasikini.
Mi bado sijachoshwa na habari hizo, tena nazihitaji kwa wingi ili niujue uoza na watu wanaohusika ili nipange jinsi ya kuwashughulikia
 
Tukifanikiwa kuwanyang'anya makuwadi hawa hili Shirika, tutakuwa tunaandika historia kwa nchi yetu.

Kwamba mtu hajalipia hisa zake apewe lakini bado apewe Shirika?.....hapana
Kwamba hata vijisenti alivyotoa vikaenda kwa akaunti ya mtu binafsi lakini apewe Shirika?....wazalendo tuseme hapana
Kwamba waendeshe kikao haramu ili kupeana Shirika?....wana wa nchi tuseme hapana

Nyerere alikufa kwa huzuni, akiwa OT International - Jo'burg alijawa bashasha kuona kidege cha ATC kimepark kati ya madege makuuubwa lakini ghafla huzuni ikamkumba alipokumbuka wakubwa (Mkapa) nyumbani wanataka kuipiga bei. Akafa kwa huzuni....

Wale tulibahatika kusoma bure kwa hisani ya Nyerere, tulosoma skuli ambapo kalamu/daftari ikiiisha wenda chukua ofisi ya mwl mkuu, skuli mwapata kifungua kinywa/uji, treni twapanda kwa warrant, n.k TUSIMAME KWA PAMOJA NA KUIFANYA TANZANIA ISIWE MAHALA SALAMA (HAVEN) KWA MABAKA UCHUMI.
 
Kuna taarifa za uhakika kwamba Robert Kisena alikwenda kwenye ofisi za UD na askari wa Ultimate Security na kuvunja milango kuchukua ofisi baada ya kukataliwa na bodi kukabidhiwa shirika hadi atakapokamilisha malipo. Polisi waliarifiwa na kukamata waliokutwa wakivunja milango wakiwamo askari wa Ultimate. Baadae Robert akaenda polisi kuwawekea dhamana ndipo na yeye akakamatwa. Alipokamatwa mchezo ndio ukaanza maana alitolewa na yeye kuwadhamini wenzake na kutoka polisi moja kwa moja wakaenda tena UDA kuchukua ofisi.

Consolidating Holding Corporation CHC ambao walikuwa wakisimamia uuzwaji wa UDA wakabaini kuwapo jinai katka tukio hilo ikiwamo kuvunja milango na pia kuona kuna forgery katika barua aliyodai Robert imetoka UDA ikimuelekeza kupeleka fedha kwenye akaunti ya Mwenyekiti. Cha kushangaza hakuna hatua zilizochukuliwa kuhusiana na jinai hizo hadi sasa.

Jambo lingine ni kwamba CHC hadi sasa wanashangaa kuona kwamba waliingia mkataba na Simon Group February 2011 na kutoa ratiba ya malipo kwa ununuzi wa hisa na malipo ya awali yalikuwa hizo milioni 280 ambazo zililipwa vyema. Simon walitakiwa kulipa malipo ya pili kabla ya kukabidhiwa shirika na baadaye malipo ya tatu yangelipwa kwa awamu lakini ndani ya kipindi cha miaka miwili.

Kwa maelezo hayo CHC na menejimenti ya UDA ikashangaa imekuaje Simon wadai kwamba walilipa fedha za mkupuo wa pili mwaka 2009 kwenye akaunti ya Mwenyekiti wakati mkataba ni wa mwaka 2011 na malipo ya awali yalilipwa mwaka 2011 inakuaje ya pili yalipwe kabla ya hata mkataba haujasainiwa? Hiyo jeuri ya kusema hayo maneno Simon wameipata wapi? Unless tunapata maelezo mengine mapya na yenye maelezo ya kina, tunashawishika kuona kwamba hapa hata wabunge wetu akiwamo Makamu Mwenyekiti wa POAC, Deo Haule Filikunjombe, walikurupuka na walipaswa kuchunguza kwanza kabla ya kutoa tamko linalotuhumu watu na linaloonyesha kumtetea Simon kana kwamba alionewa.

Kwa kweli ni vyema Bunge likachyukua hatua za makusudi kujisafisha ili tusiendelee kuona yaliyotokea kwenye Kamati ya Mrema kule Tanga baada ya Kafulila kuibua kashfa ya rushwa na ya Jairo pamoja na mengine ambayo kwa kweli si vyema chombo nyeti kama Bunge kikapoteza uaminifu wake kwa jamii. TUNALIAMINI BUNGE NA WABUNGE WENGI na ni vyema wale wachache wakadhibitiwa.
 

jumatano, 13 julai 2011



Ufisadi wa kutisha UDA

• Yauzwa kwa mil. 288/- badala ya bil. 1.4/-

na Mwandishi wetu


SHIRIKA la Usafiri Jijini Dar es Salaam (UDA), limebinafsishwa kwa Kampuni ya Simon Group Limited kwa bei ya kutupwa ya sh milioni 285 badala ya sh bilioni 1.4.
Kibaya zaidi, shirika hilo limebinafsishwa kwa kampuni hiyo bila kuwashirikisha wanahisa kwa sababu zisizojulikana.
Wanahisa wa shirika hilo linalokadiriwa kuwa na mtaji wa sh bilioni 12 ni Jiji la Dar es Salaam (24.5), Serikali (23) na asilimia 52.5, zimechukuliwa na mwekezaji mpya ambaye ni Simon Group Limited.
Uchunguzi uliofanywa na gazeti hili, umebaini kuwa Simon Group Ltd, yenye makao yake jijini Mwanza, imeuziwa hisa 52.5 za UDA ambazo zilikuwa chini ya Msajili wa Hazina.
Katika moja ya barua ya Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Februari 28 mwaka huu, iliyotiwa saini na ofisa aliyejitambulisha kwa jina moja la Mgendera, kwenda kwa Meneja Mkuu wa UDA, ilimuagiza asitishe uuzaji wa hisa hizo kwa madai kuwa shirika hilo la umma lipo chini ya Consolidated Holding Corporation (CHC) wanaosimamia ubinafsishaji wa mashirika ya umma.
Aidha, uchunguzi umebaini kuwa mnunuzi huyo amepewa baraka za ununuzi na bodi ya wakurugenzi ya UDA, inayoongozwa na Mwenyekiti wake, Iddi Simba.
Simon Group Ltd imelipa shilingi milioni 285.6 ambazo ni asilimia 12 ya hisa za UDA zipatazo 15,000,000.
Kwa mujibu wa nyaraka za mauzo ya shirika hilo ambazo nakala zake tunazo, zinabainisha kuwa Machi 4, mwaka huu, kampuni hiyo iliilipa UDA sh milioni 200 kwa stakabadhi namba 16628, na stakabadhi namba 16629 ya sh milioni 85 ikiwa ni sehemu ya malipo ya hisa 7,880,303, sawa na sh 145 kwa kila hisa.
Malipo hayo yalifanyika kwa ahadi kuwa hisa zilizosalia zingelipwa ndani ya siku 120, jambo ambalo halikufanyika hadi Juni 10, mwaka huu.
Badala yake inadaiwa kuwa mwekezaji huyo, alifika katika ofisi za UDA na kujitangaza kuwa ndiye mwekezaji mpya aliyenunua hisa za UDA kwa asilimia 52.5.
Hata hivyo Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Simon Group Ltd, Robert Kisena, anadaiwa kuvunja ofisi ya Meneja Mkuu wa shirika hilo, Victor Milanzi na kuchukua nyaraka muhimu zikiwamo hati za umiliki wa ardhi na kutuma ujumbe wa maandishi kwa njia ya simu ya mkononi, akitishia maisha ya Milanzi.
Kwa mujibu wa habari hizo, Meya wa Jiji, Didas Masaburi, alishuhudia siku mwekezaji huyo alipofika ofisi za UDA na kumuondoa meneja wake, Milanzi.
Milanzi alichukua tahadhari ya vitisho hivyo kwa kutoa taarifa kwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Temeke, David Misime na kufungua RB namba 4610/2011, lakini hakuna hatua zilizochukuliwa hadi sasa.
Alipohojiwa na gazeti hili juu ya kuwapo kwa taarifa hizo, Kamanda Misime alikiri kuwapo kwa tukio hilo, lakini alisema wametumia busara kurudisha suala hilo mikononi mwa wahusika.
“Ni kweli tumefikishiwa tuhuma hizo nasi tukawashauri wakayazungumze kwa kuwa tumebaini mkataba wa UDA na mwekezezaji una hitilafu zinazosababisha misuguano hiyo,” alisema Kamanda Misime.
Naye Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa UDA, Iddi Simba, alipohojiwa ushiriki wa bodi yake katika sakata la mwekezaji huyo, alisema suala hilo amelipeleka kwa wahusika ambao ni Consolidated Holding Corporation (CHC), hivyo hawezi kulitolea maelezo yoyote kwa kuwa wao ndio wenye mamlaka.
Mkurugenzi wa Simon Group Ltd, Robert Kisena, alipoulizwa juu ya sakata hili, hakuwa tayari kutoa ushirikiano na badala yake alisema CHC wanatarajia kutolea ufafanuzi suala hilo.
Kwa upande wa CHC, msemaji wake, Joseph Mapunda, jana aliitisha mkutano na waandishi wa habari na kukiri kuwapo kwa mvutano kati ya UDA na mwekezaji huyo.
“Ni kweli kuna mvutano na mwekezaji, hivi sasa hatuna cha kuzungunza kwa vile ametufungulia kesi Mahakama Kuu ya biashara inayohusu madai. Mshitakiwa namba moja UDA na sisi washitakiwa namba mbili. Kesi hiyo ilifunguliwa Desemba 22, mwaka jana na kupewa namba 100/2010,” alisema Mapunda.
Meya wa jiji alipohojiwa juu ya ushiriki wake kumng’oa Milanzi, alisema alihusika kwa kuwawakilisha wana hisa upande wa jiji, baada ya kupata malalamiko kutoka kwa mwekezaji huyo kuwa fedha alizonunulia hisa zimetumika vibaya.
“Ni kweli nilihusika kumsimamisha meneja wa UDA kwa kuwa mwekezaji alilalamika namna fedha alizotoa zilivyotumika vibaya, nikachukua hatua za awali ili kunusuru hali hiyo, ikiwamo kufunga akaunti zote,” alisema Masaburi.
Akizungumzia mkataba uliotumika kuruhusu mwekezaji huyo kumiliki shirika hilo la umma, alisema mkataba huo aliukuta umeshasainiwa na Bodi ya Wakurugenzi wa UDA, hivyo asingeweza kuingilia kati kwa kuwa mahakama ndiyo inaweza kuutengua.
“Unajua mwandishi, ule mkataba nimeusoma, kuna vitu vingine kama vile hisa alizouziwa Simon Group ni zile ambazo hazijagawiwa ambazo ni asilimia 52.5, jiji linamiliki asilimia 24.5 na serikali inamiliki asilimia 23, ukiangalia mwekezaji anaunda timu ya utawala,” alisema.
Aidha, alisema hivi karibuni madiwani watafanya kikao ambapo pamoja na mambo mengine watachambua kuona kama mkataba huo una maslahi kwa taifa au la
Kwa upande wake, Milanzi alisema hakutendewa haki kwani bodi iliyomwajiri, ndiyo yenye mamlaka ya kumwachisha kazi.
“Mimi niliajiriwa na bodi ya wakurugenzi wa UDA na ndio wanaopaswa kunipa barua ya kuniondoa kazini, haiwezekani dhamana niliyopewa ya kuongoza na kusimamia shirika la umma nikabidhi bila maandishi,” alisema Milanzi.
UDA ina mtaji unaofikia sh bilioni 11.7, yakiwemo mabasi 20, wafanyakazi 120 samani za ofisi, maghala na maeneo ya wazi.






 

Mkuu, huu ni mtego wa panya aliyekuwemo na asiyekuwemo................!!! Yaleyaleeeeee ya Adadi Rajabu vs Mahita a.k.a zombe!!!!!!!
WOOOTE MANZI GA NYANZA!!!!!!!!!!!!

 
Tunakwenda wapi jamani!!!!Mbona kila kukicha ni kama shetani yuko kazini!!!! CCM wakati mwingine muwe mnafikiria utu jamani, hizi mali tutaziacha!!!!!!!!!!!!!! ohooooooooooo!
 
Mkuu Invsible asante, ngoja niikalie halafu tuone.
a ya magamba!!
Aluta continua... Nawashauri muache kupoteza nguvu zenu kubishana na Mwita25; huyu ni kijana aliyelewa favour-ism; ser
 
Thanks for sharing with us, we will keep our eye watching this stupid game. We are still waiting onather stuped game/ scandle concerning 3 Trilion Tshs.
 
Tanzania shamba la bibi,chukua chako mapema jamani,watu wanakana wakati kila kitu kinajulikana.shame on then ngoja tuone mdaharo wao wa kesho wa kubebana.
 

Siku zote penye harakati na pilikapilika kwenye UFISADI, "shareholders" ambao ni "minority" wanakuwa kwenye mabano yaliyo wazi ili kufanikisha lengo zima la dhuluma.

Mimi nafikiri, shirika la UDA kisheria bado linahesabika lipo ila kinamna watu wanafanya mambo yao kuhalalisha njama za kugawana mali hio, maaana mali ni pamoja na assets kama majumba na vifaa vingine na pia kama kulikuwa na salio kwenye akaunti benki.
 
Hata hivyo tumechoshwa na habari za skendo za rushwa. Hakuna muda wa kutosha wa kujadili watu wamepanga nini, wameiba sh ngapi n.k. Huu ni muda wa kujenga taifa letu changa lililokwama kwenye wimbi la umasikini.

Hakuna kichwa kinachoweza kuzaa wala kusimamia jambo lolote la maendeleo ya taifa hili kama
kinashiriki kwenye wizi,kwa namna yoyote ile, hata kwa kuuangalia unafanyika mbele yake. hakipo.

Haya yanayofanyika ni somo tosha kwa yeyote anayefikiria kukwiba rasilimali za taifa hili,
kwamba chances za kujulikana ni 100%.Then, we shall all be able to seat down and make
this country better for every one.

Aluta continua
 
Dr. Masaburi na kelele zote kuhusu UDA kumbe yeye naye ni mmoja wa wasuka deal. Sijui ni sheria ipi ambayo inampa mamlaka ya mnunuzi kuwa Katibu wa mkutano wa wanahisa wakati hata ununuzi halisi haujakamilika. Pamoja na kupokea ushauri toka kwa lawyers bado hawa jamaa wakaamua kupindisha sheria, taratibu na kanuni, na Masaburi akaangua signecha.

Baada ya Masaburi kuumbuliwa sasa anakuja na vitimbi vyake kwamba yeye ndiye kagundua ufisadi ule. Umeugundua vipi na wakati wewe mwenyewe umeingia choo cha kike kwa kuidhinisha Shareholder Extra-ordinary Meeting ambao kwa mujibu wa sheria na ushauri wa mwanasheria, haukuwa halali. Huyo ndiye Meya wa Jiji - Kada wa CCM (Magamba).
 

Hiyo picha ya Kisena mbona inafanana na ya DCI Manumba? Au lenzi yangu inahitaji macho...teh..teh.
Kuna uhusiano wowote na Manumba?
 
Magonjwa ya kuambukiza nayo yana mashaka sana katika kupambana nayo..kipindupindu wanakufa nacho waliowazima kusogelea mwili ni mwiko.na mengine pia.Sasa hapa kuna Gonjwa limegonga watu na walio na akili wanaona kwa macho kabisa..Sasa kutokomeza ni gharama ya Moyoni hapa..Duuu..Nchi ina wezi sijaona ...Mungu Wangu...Njoo tusaidie kung'oa hivi vimelea maana watu wako Tunaangamia.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…