Uchumba wangu umevunjwa

 
Habari wadau. Heshima kwenu.
Asanteni kwa kuchangia uzi wangu na kunishauri.
Naomba kutoa mrejesho.
Ukweli ni kwamba huyo niliyekuwa namchukulia kama mchumba wangu kipindi tunaanza mahusiano aliniambia yeye ni single, tena single wa muda mrefu. Kumbe alikuwa na mtu wake ambae wapo nae kwa muda wa kama miaka miwili na walishafanya mengi ya pamoja. Shida ni kwamba walikuwa na migogoro ya hapa na pale na huyo mtu wake....kibaya zaidi huyo jamaa yake alikuwa ni mtu wa kusafiri anaweza asiwe karibu na mwanamke wake huyo karibu hata kwa miezi mitatu. Kipindi anaanza na mimi hakuwa karibu na huyo mtu wake. Kiukweli tulipoingia kwenye mahusiano alinionesha mapenzi ya hali ya juu zilikuwa hazipiti dakika tano bila kunambia nakupenda tukiwa wote....na nikijibu nampenda pia, anasema ndo unioe jamani....tulikuwa tunakuwa nae karibu mara nyingi ananipikia na kufurahi.....sikuwahi kuhisi kama kuna tatizo mpaka ilipotokea issue ya ile conversation....... Ilipotokea ile issue tulielewana na tukaendelea. Kumbe jamaa yake alirudi na hivyo akawa anatafuta mbinu ya kuniacha. Hata hivyo alishindwa namna ya kuniacha mpaka pale jamaa yake alipogundua. Ndo akamua kukata mahusiano na mimi akabaki na huyo jamaaa.

Asanteni kwa maoni yenu,maana yali-base kwenye ukweli.
#longLiveJamiiforums

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Asante kwa kuchangia. Inawezekana, lakini huyo mwanamke ananipenda sana...na ananihitaji sana katika maisha yake,ila kibinadamu ameshindwa kuhimili.

Sent using Jamii Forums mobile app
Usijiaminishe hvo mkuu kwa mwanamke.
Mwanamke akiamua kukugeuka ni sekunde tu unabaki unalia. Kikubwa we fanya uchunguzi kwa kina huo n mchezo tu umesukwa ili akuache vizuri.
Kama anakupenda tatzo dogo tu hilo why alikukimbia na kukuacha pekeako, why msingeshilikiana kumtafta huyo alietuma sms?
Mfano, ungeziweka hzo no kwenye simu ya mpenzi wako ili akampigia yeye huenda angepokea no ngeni!!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huyo ndo mwanamke so ogopa kuanzia leo kiumbe anaeitwa mwanamke.
Usimwamini 100% mwanamke na ukiwa nae gegeda kabisa as if kesho hutamwona tena! Yan piga, komoa akiondoka hata usiwe na habari nae. Hapo hata akizingua huwezi kuumia

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…