Uchepukaji salama

Uchepukaji salama

Baba C

Senior Member
Joined
Mar 15, 2012
Posts
125
Reaction score
55
Suala la uchepukaji limekuwa haliepukiki na limekuwa changamoto kwa watu wengi. Sishauri sana ila kama imekulazimu kuchepuka chukua tahadhari zifuatazo uwe salama;

1.Uwazi: Uwe wazi kwa huyo unaemchepukia kwamba una njia kuu(mke)na anapaswa kumuheshimu
2.Muda wa mawasiliano: Kamwe asikupigie simu usiku kuanzia saa kumi na mbili kuendelea na ikibidi wewe ndo unapaswa kuchokoza mawasiliano na si yeye
3.Frequency ya mawasiliano: Msipende kuwasiliano hovyo hovyo kwani risk yake ni kubwa
4. Message: Msipende kutumiana sms za mapenzi na kama italazimu futa the moment unamaliza kusoma
5.Usipende kumwambia mchepuko madhaifu ya mkeo kwani ni hatari sana na hujui atayatumiaje?
6.Wivu: Ule ni mchepuko na huna mpango wa kumuoa sasa akitoka na mtu mwingine wivu wa nini?Hiyo haijatulia


Uchepukaji si vizuri ila ikilazimu...karibuni wengine kwa michango zaidi
 
siku hizi kuna ukuni au kupishana na upara kwa kisu
mchepuko chunga
 
Utajisahau tu ukikolea,wanaoshikwa huwa hawapendi....
 
Suala la uchepukaji limekuwa haliepukiki na limekuwa changamoto kwa watu wengi. Sishauri sana ila kama imekulazimu kuchepuka chukua tahadhari zifuatazo uwe salama;

1.Uwazi: Uwe wazi kwa huyo unaemchepukia kwamba una njia kuu(mke)na anapaswa kumuheshimu
2.Muda wa mawasiliano: Kamwe asikupigie simu usiku kuanzia saa kumi na mbili kuendelea na ikibidi wewe ndo unapaswa kuchokoza mawasiliano na si yeye
3.Frequency ya mawasiliano: Msipende kuwasiliano hovyo hovyo kwani risk yake ni kubwa
4. Message: Msipende kutumiana sms za mapenzi na kama italazimu futa the moment unamaliza kusoma
5.Usipende kumwambia mchepuko madhaifu ya mkeo kwani ni hatari sana na hujui atayatumiaje?
6.Wivu: Ule ni mchepuko na huna mpango wa kumuoa sasa akitoka na mtu mwingine wivu wa nini?Hiyo haijatulia


Uchepukaji si vizuri ila ikilazimu...karibuni wengine kwa michango zaidi

Nimeipenda hii. wanaume bwana. Eli79, umemsikia mwenzenu yaani anawapa mbinu za kuchepuka, Mimi nikikukamata na mchepuko wako. Napita tu wala sikuulizi kitu. Utajicheki ni kiasi gani utakavyoumia wewe mwanaume.
 
Hapo ndo umefikiria hadi mwisho wako wa kifikiri, na kuja kutupa experiance yako ya uzinzi. Watanzania bwana!
 
Unapotoa njia za kuchepuka maana yake unahalalisha jambo hili,kwanini tusiwekeze kwa wake zetu vitu ambavyo tunaona havipo kwao na tunavipata kwenye hiyomichepuko?Kama naona mke wangu hana kitu fulani na ninakipenda namwambia kuwa nataka hiki na hivi kuliko nianze kuangalia upande mwingine kitu ambacho baadae kinaleta matatizo katika familia na jamii kwa ujumla.
Cha msingi wakuu yafaa tubaki njia kuu itatusaidia zaidi kuweka familia zetu katika maisha yaliyo bora.
 
Unapotoa njia za kuchepuka maana yake unahalalisha jambo hili,kwanini tusiwekeze kwa wake zetu vitu ambavyo tunaona havipo kwao na tunavipata kwenye hiyomichepuko?Kama naona mke wangu hana kitu fulani na ninakipenda namwambia kuwa nataka hiki na hivi kuliko nianze kuangalia upande mwingine kitu ambacho baadae kinaleta matatizo katika familia na jamii kwa ujumla.
Cha msingi wakuu yafaa tubaki njia kuu itatusaidia zaidi kuweka familia zetu katika maisha yaliyo bora.

U r the only 1 remained in 100 millions
 
Wazo la kuwekeza kwa wake zetu ni zuri ila chukulia mkewe kakeketwa na u lipoonja ambaye hajakeketwa ukachanganyikiwa!Hapo utafanyaje mkewe aweze kuziba hilo pengo?
 
Unapotoa njia za kuchepuka maana yake unahalalisha jambo hili,kwanini tusiwekeze kwa wake zetu vitu ambavyo tunaona havipo kwao na tunavipata kwenye hiyomichepuko?Kama naona mke wangu hana kitu fulani na ninakipenda namwambia kuwa nataka hiki na hivi kuliko nianze kuangalia upande mwingine kitu ambacho baadae kinaleta matatizo katika familia na jamii kwa ujumla.
Cha msingi wakuu yafaa tubaki njia kuu itatusaidia zaidi kuweka familia zetu katika maisha yaliyo bora.

hili nalo neno
maana ukifuatilia vizuri kila MTU anakuwa mchepuko wa mwingine
 
Back
Top Bottom