Wewe wasema,
Hayajawahi kukukuta au hujala chumvi bado ndio maana mawazo yako yamekutuma hivyo, au labda unaishi mbinguni na si dunia hii...
Mtu asiyeamini kwamba ushirikina/nguvu za giza zipo bila shaka ahamini uwepo wa Mungu pia, na hapo ndipo tunasema asiyeamini ana akili ndogo saaana
Naanza kuamini u mtoto kiumri hujakutana na shuruba au ni mtoto wa mama sana hujui mtaa upojeImani za kidini na imani za kishirikina ni pande mbili za sarafu ile ile.
Ni nadra kuwa na akili kubwa halafu ukaamini upuuzi wa habari za kishirikina.
Hakuna kitu kabisa.
Naanza kuamini u mtoto kiumri hujakutana na shuruba au ni mtoto wa mama sana hujui mtaa upoje
Hujui unaloliandika wewe, pangusa miguu ushushe neti ulale.Hakuna uchawi wewe.
Kama upo na kama unamjua mchawi yeyote yule, mwambie aniroge.
Mwenzio gfsonwin alijaribu akachemsha akaishia kula kona.
Na hii ofa ni kwa wachawi wote walio JF.
Nirogeni mnithibitishie kuwa kweli uchawi upo na si longolongo tu.
Hujui unaloliandika wewe, pangusa miguu ushushe neti ulale.
Hujakua bado na kukutana na shuruba utakapokutana nazo hutahitaji kuwa Tomaso tena, uchawi haupo kipumbavu na kizembe kama unavyosema eti waambie wachawi wakuroge...
Amina
Baki na imani yako hiyo...
Siwezi endelea kubiashana na wewe, yaelekea hapo bado umejifunika shuka uliyonunuliwa na wazazi ndio maana una jeuri ya kuongea. Waliopitia shuruba na wenye akili timamu hili si suala la kubiashanaNinachokwambia siyo imani. Ni ukweli.
Wewe ndo baki na imani yako na wenzio wenye akili ndogo.
Siwezi endelea kubiashana na wewe, yaelekea hapo bado umejifunika shuka uliyonunuliwa na wazazi ndio maana una jeuri ya kuongea. Waliopitia shuruba na wenye akili timamu hili si suala la kubiashana
Naamini wewe u mtoto sababu kama unasema hakuna uchawi basi hakuna shetani na kama hakuna shetani basi hakuna Mungu..kua uyaone wewe bado mtoto wa Mama
Mkuu,Bila Shaka umewahi kusikia kuhusu wachawi kula nyama za watu waliokufa, awali sikuwa nikiamini mambo haya lakini nilipoanza kupata akili za utambuzi ndipo nilianza kushuhudia mauza uza.
Nilikuwa kabla sijalala lazima nioge na kuwa safi kabisa lakini cha ajabu kila nikiamka asubuhi miguu ilijaa vumbi na udongo na kuchoka sana. Hali hiyo ilinitokea mara kadhaa kisha ikapotea, nikaanza kujiona kila nikilala usiku nilikuwa nanyanyuka na Nilikuwa nikitazama kitandani najiona nimelala. Kisha nikawa napaa kama ndege naelea angani na nikawa naenda popote ila sikujua kwanini hali ile ilikuwa inanitokea pasipo ridhaa yangu. Ikafika mahali nikawa kila nikipaa natokea mahali nyumba ya mtu hata simjui, nakuta watu wengi kisha nakaribishwa sinia la nyama. Hakika zilikuwa ni nyama za ng'ombe aliyechomwa vizuri nikawa nakula mpaka nashiba ndiii. Ilikuwa kila nikiamka asubuhi nimeshiba na hamu ya kula ikawa inaniondoka. Haikuishia hapo ikawa nakutana na mwanamke mmoja amenona sana ila sura siikumbuki nikawa nabanjuka naye ipasavyo nikiamka nimechafuka ile ile. Hali ile ikaendelea kwa muda nikawa sasa usiku nikilala naona wachawi wanaoingia chumbani kwangu yaani nawaona kama mchana kabisa ila cha ajabu nipo usingizini. Nilipokutana na mtaalamu mmoja ndipo akanieleza nilishalimishwa sana kichawi kisha baadae nikawa naweza kutoka na kupaa nilishalishwa sana nyama za watu pasipo kujua na nikawa na uwezo wa kuona watu pia nimeshazini na majini pasipo kujijua. Ila nilipoanza kukemea hali ile ikapotea kabisa nikawa nalala kwa amani mpaka leo miaka kadhaa hali hiyo haipo tena katika maisha yangu.