Uchambuzi wangu kuhusu vituo vya redio vya Mwanza

Uchambuzi wangu kuhusu vituo vya redio vya Mwanza

mayowela

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2014
Posts
2,125
Reaction score
1,757
Jiji la Mwanza kuna vituo vingi vya redio nikimaanisha Local/regional radios, kama
Jembe fm, Lake fm, Metro fm, Afya radio, Dira fm, Passion fm, Sauti fm, Iqrafm, Kwa Neema fm naomba nisiziweke RFA na KISS FM

Redio hizi zilianza kwa kasi sana lakini kwa sasa zinaonekana kama kushuka kwa kasi nakupoteza umaarufu
sijajua tatizo ni kuzoeleka masikioni, watangazaji wanaopendwa kuondoka, menejimenti kubadilishwa, mishahara midogo au kukosa matangazo

Naomba nizungumzie redio kadhaa ambazo nilizishuhudia kuanzishwa kwake kipindi nipo huko na kwa sasa nilivosikia na nimezifatilia hata nikiwa mbali through online (TuneIn)

JEMBE FM
Moja kati ya redio iliyoanza kwa kasi miaka ya 2015 na niseme ilileta ushindani mkubwa na timu yake ya watangazaji ilikuwa nzuri na ni redio maarufu yenye usikivu safi, ila kwa sasa naona kama imepunguza kasi kidogo tofauti na hapo awali sijajua shida ni nini

METRO FM
Naweza kusema hii ni moja kati ya redio za mwanza ambayo inajitahidi kumantain huwa haishuki wala haipandi sana na inasikilizwa sana sana nikili hilo nadhani nikutokana na customer base iliyojiwekea, ni redio ambayo mtangazi aondoke au menejimenti ibadilike huwezi ona kama imeyumba

PASSION FM
Ni redio ya muda mrefu sana ila huwa nashindwa kuielewa mpaka kesho, hpo zamani ilikuwa Dar kuna studio na Mwanza sijafahamu kwa sasa, ni redio ambayo haibadiliki iko vilevile miaka nenda rudi

LAKE FM
Ni redio ambayo pindi inaanzishwa mwaka 2016 tulijua italeta mapinduzi makubwa, ila naweza sema ni redio ambayo inapitia wakati mgumu na ni redio ambayo imepitia changamoto nyingi, kukatishwa tamaa naweza sema na vihujuma vya hapa na pale, kwa asilimia kubwa redio hii imeshuka sana sana, timu ya kwanza kuanzisha reio hii ilikuwa timu baab kubwa na ingeifikisha redio hii mbali, ila ile timu naona sahizi kila mtu anafanya issue zake na fursa zingine, pia kubadilika kwa watangazaji mara kwa mara yaani inakata sana, menejimenti pia naona inabadilika sana. Kama redio hii ikipata menejimenti nzuri na watangazaji wazuri watakaokaa muda mrefu itatisha siku zijazo.. Hii redio huw inaniuma sana

DIRA FM
Redio hii tangu nimeanza kuisikiliza naona iko tofauti kidogo na naweza sema kwa sasa Mwanza ndio redio pendwa sijajua ni kwa sababu ya miziki inayochezwa na madj kila kipindi bila sauti ya mtangazaji au ni nini, ila nimepita sehemu nyingi sana naona inasikilizwa, Bg up kwao wamefanya mapinduzi. Kuna mdau alionesha moja ya picha ya studio mara ya kwanza kabisa inaanza kurusha matangazo nilicheka sana ila nikaona picha zingine ni bonge moja la transformation

AFYA RADIO ni redio pia yenye base yake na ni redio niseme inayotoa watangazaji wakali sana ambao hunyakuliwa na media zingine za mwanza, hii redio huwa haipandi wala kushuka iko pale pale ni redio kongwe pia kwa mwanza, SAUT FM Redio ya chuo ambayo ni community based hii pia ina base yake na haiwezi kuchuja kwa wasikilizaji wake kwa sababu imeishajiwekea msingi flani,

Naomba niishie hapo nisizungumzie KWA NEEMA FM na IQRA FM, Hizi ndio media zetu na sisi tunazojivunia zinazoleta maana ya Jiji

I love rock city
 
mwanza kuna vituo vingi vya redio nikimaanisha Local/regional radios, kama
Jembe fm, Lake fm, Metro fm, Afya radio, Dira fm, Passion fm, Sauti fm, Iqrafm, Kwa Neema fm naomba nisiziweke RFA na KISS FM

Redio hizi zilianza kwa kasi sana lakini kwa sasa zinaonekana kama kushuka kwa kasi nakupoteza umaarufu
sijajua tatizo ni kuzoeleka masikioni, watangazaji wanaopendwa kuondoka, menejimenti kubadilishwa, mishahara midogo au kukosa matangazo

Naomba nizungumzie redio kadhaa ambazo nilizishuhudia kuanzishwa kwake kipindi nipo huko na kwa sasa nilivosikia na nimezifatilia hata nikiwa mbali through online (TuneIn)

JEMBE FM
Moja kati ya redio iliyoanza kwa kasi miaka ya 2015 na niseme ilileta ushindani mkubwa na timu yake ya watangazaji ilikuwa nzuri na ni redio maarufu yenye usikivu safi, ila kwa sasa naona kama imepunguza kasi kidogo tofauti na hapo awali sijajua shida ni nini

METRO FM

Naweza kusema hii ni moja kati ya redio za mwanza ambayo inajitahidi kumantain huwa haishuki wala haipandi sana na inasikilizwa sana sana nikili hilo nadhani nikutokana na customer base iliyojiwekea, ni redio ambayo mtangazi aondoke au menejimenti ibadilike huwezi ona kama imeyumba

PASSION FM
Ni redio ya muda mrefu sana ila huwa nashindwa kuielewa mpaka kesho, hpo zamani ilikuwa Dar kuna studio na Mwanza sijafahamu kwa sasa, ni redio ambayo haibadiliki iko vilevile miaka nenda rudi

LAKE FM
Ni redio ambayo pindi inaanzishwa mwaka 2016 tulijua italeta mapinduzi makubwa, ila naweza sema ni redio ambayo inapitia wakati mgumu na ni redio ambayo imepitia changamoto nyingi, kukatishwa tamaa naweza sema na vihujuma vya hapa na pale, kwa asilimia kubwa redio hii imeshuka sana sana, timu ya kwanza kuanzisha reio hii ilikuwa timu baab kubwa na ingeifikisha redio hii mbali, ila ile timu naona sahizi kila mtu anafanya issue zake na fursa zingine, pia kubadilika kwa watangazaji mara kwa mara yaani inakata sana, menejimenti pia naona inabadilika sana. Kama redio hii ikipata menejimenti nzuri na watangazaji wazuri watakaokaa muda mrefu itatisha siku zijazo.. Hii redio huw inaniuma sana

DIRA FM
Redio hii tangu nimeanza kuisikiliza naona iko tofauti kidogo na naweza sema kwa sasa Mwanza ndio redio pendwa sijajua ni kwa sababu ya miziki inayochezwa na madj kila kipindi bila sauti ya mtangazaji au ni nini, ila nimepita sehemu nyingi sana naona inasikilizwa, Bg up kwao wamefanya mapinduzi. Kuna mdau alionesha moja ya picha ya studio mara ya kwanza kabisa inaanza kurusha matangazo nilicheka sana ila nikaona picha zingine ni bonge moja la transformation

AFYA RADIO ni redio pia yenye base yake na ni redio niseme inayotoa watangazaji wakali sana ambao hunyakuliwa na media zingine za mwanza, hii redio huwa haipandi wala kushuka iko pale pale ni redio kongwe pia kwa mwanza, SAUT FM Redio ya chuo ambayo ni community based hii pia ina base yake na haiwezi kuchuja kwa wasikilizaji wake kwa sababu imeishajiwekea msingi flani,

Naomba niishie hapo nisizungumzie KWA NEEMA FM na IQRA FM, Hizi ndio media zetu na sisi tunazojivunia zinazoleta maana ya Jiji

I love rock city
Ungetoa na megahaZ ungewasaidia watu wa huko
 
Katika Radio ninayoumia "kufwafwanzika" kwake hapa Tanzania ni Kiss FM hii radio ilikuwa kweli inafaa kusikilizwa na Wanaume lakini toka ilivyoanza kutumia na Lugha ya Kiswahili ndio ikafa kibudu hadi Leo sijui kama ipo maana Iringa huu mwaka wa 3 haipatikani.
Sinaga radio ya kisikiliza zaid ya kiss FM naikubal sana
 
Tatizo za radio za mwanza hazifik mbali radio gan zinashika wilaya moja au mbili kwa mfano jembe FM radio inashika wilaya ya nyamagana peke Yake, kuna radio nyingine inaitwa radio Sengelema nayo inashika sengelema pekee
 
Mara ya mwisho mimi kusikia redio nakumbuka bado nasoma shule ya msingi miaka ya 90
 
Hizi radio hata hazivuki maji. Mwisho wake Igoma, usagara, airport, buswelu , mi huwa sizitofautishi na takataka
 
Tatizo la redio za mikoani watangazaji wake wanaiga maudhui ya vipindi mpaka sauti na namna ya kutangaza kwa redio kama Clouds! Ubunifu ni sifuri
kweli kabisa
 
kiss FM ilijiua baada ya kuanza kutangaza kwa kiswahili
walihisi Kingereza hakina wasikilizaji kumbe ndio walikuwa wanajipoteza kabisa, sawa na Choice walivoanza kutangaza kiswahili yaani ndio wamekuwa tia maji tia maji
 
Tangu anguko la RFA kutokea kutokana na kutosikika kwa watangazaji mahiri niliokua na wakubali...hata sina muda tena hizi zilizo ibuka jana,maisha yanaenda kasi sana
 
Hata RFA haina uhakika wa kusikika mda wote. Ni redio unayoweza kusikia sasa hivi halafu ikakatika zaidi ya siku mbili kabla haijarudi hewani!
 
Mi hapa nasikiliza Dira Efm, nikivuta muda uende nisogee MJ kona ya Bwiru kuchek Epl, Nasikiliza sana Dira Efm sababu hawana matangazo mengi,ni mziki wa kutosha.
 
Back
Top Bottom