Hakika kama Taifa kuna magonjwa makuu matatu ya msingi nayo Uchama, Rushwa na Ufisadi-aka umimi.Hili lako ulilolisemea ni baya sana.Ubaya wa hili la Uchama,ni kuwa chama kama kikundi cha watu wenye malengo Fulani, unaweza yumbisha malengo ya Msingi ya Taifa endapo chama husika akiendi kwenye mstari kulingana na mkataba wake na Umma [Yani Taifa].
Uchama umefanya Taifa lisimame na mambo mengi kwenye Taifa yaende ndivyo sivyo na kwa kuwa wasimamizi wa kuu kwenye Taifa kofia iliyowaweka wakae kwenye dhamana ya Uongozi wa Taifa ni kofia ya chama, basi mambo mengi yanayotendwa na yeyote aliye ndani ya chama yakiwa na sura ya kubomoa Utaifa hayana mdhibiti na hivyo kupewa fursa ya kumea kwa tiketi ya Mwenzetu huyu , au ndugu yetu huyu.Ufisadi umetamalaki kwa sababu ya uchama, rushwa imejijenga kwa sababu ya uchama.
Walinzi wa Utaifa baadhi wamegeuka kuwa walinzi wa Uchama.Upofu umekwenda hata kwa wenye weredi wa usomi wa dalasani [Academicians] nao akisha simama kwenye chama HAONI tena Ukweli [REALITY] na kushauri mabaya kwa faida ya kulinda Uchama [Kikundi] na kukwepa dhamana ya kuona mambo kwa jicho la UTAIFA.Keki ya Taifa imegawanywa kwa kuangalia nani anastahiki kupewa keki fulani kwa kuwa ni wa chama fulani-neno upinzani [Kwa lugha ya wenzetu Opposition maana ya opposite yani kinyume] limebeba tafsiri HASI kwenye jamii.Viongozi wa vyama wamepandikiza tafsiri hasi vichwani mwa Wananchi wenye uanachama wa vyama vya kisiasa,uchama umevaa kofia ya Utaifa kwenye maamuzi magumu ya Taifa,wakati Utaifa ulipaswa kumeza Uchama.
Leo walinzi wa Taifa wanaumiza vichwa hatima ya Taifa, wakati kama kweli Mlinzi wa Taifa angekuwa havai Kofia ya Chama hakika vuguvugu ili ambalo liko mikononi mwa Wananchi kuhusu ukuu wa chama kutamalaki ukuu wa Taifa basi wananchi wasingekuwa na jaka moyo la Rushwa wala Ufisadi...iwe vipi hata kama walinzi wa Nchi wanasema hayo yanayopita kwenye Rushwa ni michezo ya kutungwa..basi ndio kusema mtungaji awajengi Wananchi kuichukia rushwa bali anajenga wanachi kuipenda rushwa kwa kuwa wale wanao kuwa wanahusishwa kwenye michezo hiyo hupata kukimbia mkono wa sheria kwa kofia ya uchama.Na matokeo ya viongozi hao kupata huruma ya uchama kwenye vyombo vya sheria Wananchi uanza pole pole kuona kuwa ukiiba kingi cha umma, ufungwi na ukiiba jenga ukaribu na uchama utoshughulikiwa na yeyote yule.
Uchama umeondoa uzalendo kwa Umma,leo hii kila raia yuko tayari kusifia uovu, wizi, uongo, rushwa, uzandiki, uchonganishi na mengineyo mengi kwa kuwa mtendaji wa tendo husika ni mwenzake kwenye chama chake.Yani liliotendwa na mhusika binafsi ugeuzwa kuwa mtendaji kasingiziwa na wabaya wa chama chake.Kwa kuwa Chama kimevaa kofia ya Utaifa basi wenye dhama ya kidola uwashambulia waliosimama kusema au kekemea mtendaji mwenye haiba ya uchama.Ila natumaini bado Taifa lina watu makini makosa yaliyofanywa siku za nyuma HAKIKA wamejifunza kuwa waliona HAYAWAHUSU wakae mbali, laini wamefika sehemu wameona mambo hayo yanawahusu kama ya KIDOLE na jicho.
Ni muda mwafaka kutenganisha chama na siasa na pia kuwatoa nje wote wenye tabia za kimakundi katika mfumo wa uongozi wa KITAIFA.Taifa linapokuwa na watu wenye tabia ya mfumo wa kimakundi, iwe rafiki, kichama, uswahiba au undugu kwa hulka ya kibinadamu kama mtu amajijenga kupitia kutegemea watu, ndio kusema siku wakitofautiana na wenzie hao basi malengo yaliyotafutwa kwa mfumo wa kijikundi na si kuzingatia maono [Vision] za wahusika mmoja mmoja ila kwa dhamana ya chama umoja kuunda ujumla wao na kutoa vision moja na sio vision ya kikundi cha watu, YANAPOTEA na kukosa DIRA ya kuyafikisha walikotarajia.Ni wakati murua sasa Wanautaifa kutoa maono ya ujenzi wa Taifa kwa kofia ya TAIFA sio Uchama...na kofia ya Kiongozi mkuu wa Taifa imkae mtu ambae watu wote wenye vyama CCM, CDM,CUF NCCR na wasio vyama wakimuona kakaa kwenye KITI CHA URAIS wanajiona wote wanamkubali kweli huyu ni kiongozi wa TAIFAna si kiongozi wa genge.
Na ndio maana kwa nchi za wenzetu yule ambae uteuliwa na chama huwa sio ndio yule kiongozi mkuu wa chama, bali mteuliwa uwa ni yule ambae uwa pia MTAIFA na WANAUTAIFA bila kujali ITIKADI zao za kivyama UAMINI PIA mteuliwa huyo kwenye chama husika INAPOFIKA KWENYE MASWALA YANAYO HUSU UTAIFA CHAMA CHAKE HAKINA NAFASI.Leo hii kuna Wananchama wanadiliki kushangilia kwa kusema akiingia kiongozi fulani chama FULANI kitakufa au mtu fulani atatafuta pa kwenda ...binafsi uwa najiskia vibaya sana na tena sana.Yana nafasi kuu ya Utakatifu [URAIS] apewe mtu mwenye dhamira ya kwenda kulipa visasi kwa kuwa tu alipingwa na fulani au alikataliwa na fulani kisa si Mwenzao bais hiyo ni laana kubwa tena mno.
UTAIFA KWANZA