Uchaguzi wa Serikali za Mitaa Afrika ya Kusini

Uchaguzi wa Serikali za Mitaa Afrika ya Kusini

Sele Mkonje

JF-Expert Member
Joined
Oct 2, 2011
Posts
643
Reaction score
846
Kampeni za Uchaguzi wa Mitaa nchini Afrika ya Kusini zimekamilika rasmi siku ya Jana ambapo tumeshuhudia Vyama vyote vya siasa vikifanya kampeni zake za mwisho katika miji mikubwa tofauti hapa nchini. Uchaguzi wa mwaka huu unatarajiwa kuwa na mvutano mkubwa hasa baada ya ANC kutangaza nia yake kubwa katika uchaguzi huu ni kulichukua tena Jimbo La Western Cape hasa jiji la Cape town ambalo lipo chini ya serikali ya DA. Tofauti na miaka iliyopita mwaka huu chama kipya chenye umribwa miaka 3 EFF kimekuja juu kwa kuweka wagombea wake katika kila mtaa nchi nzima kitendo ambacho hakikuwahi kufanywa na chama pinzani cha DA ambacho kina zaidi ya miaka 20 na Hakikuwah kusimamisha wagombea nchi nzima.
Mimi kama mtanzania ninaeishi hapa Afrika ya kusini ninajifunza mengi sana kupitia uchaguzi huu,nahisi Afrika ya kusini Ndio nchi pekee afrika yenye demokrasia ya kweli. Tumeshuhudia Mwaka huu kuwepo na ongezeko la vyama vingi vya siasa vikiwemo pia vya kidini kama vile vya kikristo na kiislam kitu ambacho kwa nchi yangu Tz hakipo. Uchaguzi Umeanza leo ambapo watu 800000 wenye mahitaji maalum watapiga kura na Siku ya Jumatano Utafanyika Rasmi uchaguzi huo wa serikali za mitaa ambapo zaidi ya Raia Milion 26 wanatarajiwa kupiga kura.
 
UPDATES

Jeshi la Afrika ya kusini limesema litasaidiana na polisi kuhakikisha Amani inatawala katika uchaguz huu kwa kutoa Wanajeshi wake pamoja na helikopta kwajili ya kuwapeleka polisi katika vituo mbali mbali vya kupigia kura. Pia tume ya uchaguzi imewakataza watu kupiga picha wakati wa kupiga kura
2016-08-02_19.26.07.jpg

Picha ni Jeshi la Polisi limemaliza kufanya mkutano wake muda mfupi uliopita
 
Hii ndo nchi pekee afrika ambapo Raisi anafikishwa mahakamani na kuhukumiwa.
Ongezea kwamba Raisi alihukumiwa na kushindwa kesi. EFF katika uchaguzi huu watafanya vizuri kuliko DA
 
Ongezea kwamba Raisi alihukumiwa na kushindwa kesi. EFF katika uchaguzi huu watafanya vizuri kuliko DA
kwa Hapa cape town DA watachukua. Ni vigumu sana kuing'oa DA Western Cape
 
kwa Hapa cape town DA watachukua. Ni vigumu sana kuing'oa DA Western Cape
Usisite kuendelea kutupa kinadlcho endele hapo downtown kwa madiba mkuu. Atleast wao wameshawekaga miguu kuelekea kwenye siasa za ustarabu sisi bado tunapiga maktaima hapa.
 
kwa Hapa cape town DA watachukua. Ni vigumu sana kuing'oa DA Western Cape
Western Cape ndio ngome ya DA Kuwang'oa ni kama haiwezekani. Mungu awasaidie EFF wazidi kuimarika napenda sana wanavyojiamini pamoja na uchache wao.
 
Western Cape ndio ngome ya DA Kuwang'oa ni kama haiwezekani. Mungu awasaidie EFF wazidi kuimarika napenda sana wanavyojiamini pamoja na uchache wao.
EFF ni chama kichanga sana na kimefanya mambo makubwa sana tangu kianzishwe. mwaka huu kitachukua viti vingi sana na miaka ijayo kinaweza kuchukua nchi. DA kimejaa Uzungu mwingi na ndo maana sasahivi tunashuhudia wazungu wakimiminika kuhamia Cape town kutoka miji mingine na hata wengine wanatoka Ulaya na kuhamia Hapa.
 
EFF ni chama kichanga sana na kimefanya mambo makubwa sana tangu kianzishwe. mwaka huu kitachukua viti vingi sana na miaka ijayo kinaweza kuchukua nchi. DA kimejaa Uzungu mwingi na ndo maana sasahivi tunashuhudia wazungu wakimiminika kuhamia Cape town kutoka miji mingine na hata wengine wanatoka Ulaya na kuhamia Hapa.
Kweli kabisa EFF wamefanya mambo makubwa ndani ya muda mfupi. Wabunge wao wanaitetemesha vilivyo serikali ya Zuma
 
UPDATES

Jeshi la Afrika ya kusini limesema litasaidiana na polisi kuhakikisha Amani inatawala katika uchaguz huu kwa kutoa Wanajeshi wake pamoja na helikopta kwajili ya kuwapeleka polisi katika vituo mbali mbali vya kupigia kura. Pia tume ya uchaguzi imewakataza watu kupiga picha wakati wa kupiga kuraView attachment 375047
Picha ni Jeshi la Polisi limemaliza kufanya mkutano wake muda mfupi uliopita
Polisi wote wanamimba
 
Back
Top Bottom