Uchaguzi wa mitaa ni utapeli mtupu

Uchaguzi wa mitaa ni utapeli mtupu

Nilitaman kama kijana mwenye kujielewa utasema nan anafaa kusimamia badala hao unaowakataa
Kinyume na hapo keleleeeeeee zenu zinaishia ulipo
 
Yaani Waziri wa Tamisemi ndio mkuu wa uchaguzi? Nashauri wanaharakati wapenda haki twendeni Mahakamani tukazuie uchaguzi huu unaokwenda kumwaga damu za watu,kwakuwa tume huru iko Mahakamani sasa ni muda uchaguzi huu wa Serikali mitaa ukazuiwe Mahakaman hadi pale utakapokuwa huru.

Plz wasomi tuokoenI kwa hili msiwe vichwa mizigo.Uchaguzi huu kama utafanyika chini ya Mbunge wa CCM yaani Waziri wa Tamisemi tusitegemee haki kutendeka sana sana itakuwa ni kuwachosha tu wapiga kura.

Tume sio huru na huu wa mitaa sio huru.

Naomba kutoa hoja
Badala ya kwenda mahakamani kurudisha kiwanja ulichotapeliwa we unaenda kuwapigania wanasiasa? Lowassa uliyempigia kura na kuzungusha mikono yupo wapi?? Jiongeze wewe bavicha
 
Nyie toeni stress zenu mitandaoni sie tunachaguana tu
Mnawafanya watu wajinga,mlipokua na ukawa mlizoa mitaa mingi kwa sheria hizi hizi za Tamisemi,leo hamna ukawa hamna cha kuwaambia wananchi,mnakimbilia kubeza uchaguzi mitandaoni,sie tunafyeka tu

Toka jiwe kaingia madarakani, jeshi la polisi ndio linaratibu mabox ya kura yakajazwe kura za ccm. Mwanaume/mwanamke kabisa unayejitambua utaweza kusimama kwenye mstari wa kura kushiriki huo utoto? Mkuu kusanyeni mpaka na mifugo yenu mkapige kura ili mshinde kwa kishindo. Hamna mtu ana muda wa kupata kilema kwa kushiriki uchaguzi ambao vyombo vya dola ndio vinaratibu ukatili dhidi ya wapinzani, eti kisa ccm haina uwezo wa kushindana lakini inataka kushinda. Halafu kichekesho mahakama hazina uwezo wa kuamua kwa haki, kisa zitaleta mgogoro na mihimili mingine.
 
Nilitaman kama kijana mwenye kujielewa utasema nan anafaa kusimamia badala hao unaowakataa
Kinyume na hapo keleleeeeeee zenu zinaishia ulipo

Mkuu nyie msiopiga kelele tangulieni vituoni hata kesho, lakini hakuna mtu anayejitambua ana muda wa kushiriki huo ushenzi wa mtu mweusi.
 
Badala ya kwenda mahakamani kurudisha kiwanja ulichotapeliwa we unaenda kuwapigania wanasiasa? Lowassa uliyempigia kura na kuzungusha mikono yupo wapi?? Jiongeze wewe bavicha

Hao unaowatetea ww waendelee kukaa madarakani bila ridhaa ya umma sio wanasiasa bali ni mashahidi wa Yehova?
 
Kumbe hii sheria inayompatia mamlaka Waziri wa Tamisemi kusimamia uchaguzi siyo mpya? Nilidhani ni sheria mpya kumbe akina Waitara walishinda uenyekiti wa serikali ya mtaa kwa sheria hii hii wakati wakiwa CHADEMA!!

Wakati hao akina Waitara wakishinda ilikuwa ni wakati wa JK, sio kwamba wakati huo demokrasia ilikuwa nzuri bali ilikuwa ina afadhali ukilinganisha na sasa, wangalau wizi ulikuwepo japo kulikuwa na soni kwa mbali. Sasa hivi sio wizi bali ni ubabe wa kishamba, polisi wanashiriki kiwaziwazi kwenye uratibu wa wizi wa kura. Ili mjue watanzania sio wajinga na hawana muda wa kushiriki upuuzi, subiri uone jinsi idadi ya wapiga kura itakavyokuwa ndogo.

Upuuzi unaofanyika kila mwenye akili timamu anaufahamu. Karne huu unashinda kwa kukubalika, ukilazimisha kushinda ili ujifanye unakubalika watu wanakuachia ushinde vizuri. Uzuri sasa hivi hata kiongozi akiitisha wananchi hawatokei kwa wingi, maana ni viongozi wasio na uhalali wa umma bali mabavu ya dola.
 
Jambo hili lingekuwa ndio kipimo halisi cha mahakama zetu. Lissu aliambiwa angekuwa sawa kama angepinga uchaguzi na sio kuapishwa.

Waziri hawezi kuwa na mamlaka yoyote na uteuzi wa wasimamizi wa uchaguzi. Tunasema tuna tume huru - uhuru wake uko wapi kama anayechagua na kutangaza wasimamizi ni waziri??
 
Yaani Waziri wa Tamisemi ndio mkuu wa uchaguzi? Nashauri wanaharakati wapenda haki twendeni Mahakamani tukazuie uchaguzi huu unaokwenda kumwaga damu za watu,kwakuwa tume huru iko Mahakamani sasa ni muda uchaguzi huu wa Serikali mitaa ukazuiwe Mahakaman hadi pale utakapokuwa huru.

Plz wasomi tuokoenI kwa hili msiwe vichwa mizigo.Uchaguzi huu kama utafanyika chini ya Mbunge wa CCM yaani Waziri wa Tamisemi tusitegemee haki kutendeka sana sana itakuwa ni kuwachosha tu wapiga kura.

Tume sio huru na huu wa mitaa sio huru.

Naomba kutoa hoja
Na hiyo Mahakama iko huru?
 
Back
Top Bottom