Uchaguzi wa CHADEMA mkoa wa Singida, ukabila watawala

Uchaguzi wa CHADEMA mkoa wa Singida, ukabila watawala

Yusuph Jr

JF-Expert Member
Joined
Jan 10, 2014
Posts
217
Reaction score
49
Wadau jana CHADEMA mkoa wa singida walifanya uchaguzi wa kuwapata viongozi wao,watakaodumu hadi 2019.

Kwa sehemu kubwa uchaguzi huo uliendeshwa kwa utulivu na umakini mkubwa chini ya msimamizi David Jumbe,ambaye wajumbe wengi wamempongeza kwa kuzingatia kanuni,miongozo na katiba ya CHADEMA.

Jumbe amejitofautisha kabisa na Shaban Limu aliesimamia chaguzi za majimbo na wilaya kwa kukiuka kanuni za uchaguzi kwa makusudi ili awapitishe wale ambao wangemuunga mkono.

Licha ya uchaguzi wa jana kwenda vizuri tatizo lililojitokeza ni ukabila wa wazi kabisa uliofanywa na baadhi ya wagombea,uliopelekea viongozi wote waliochaguliwa kuwa ni wanyaturu pekee.

Walijinadi kwa wapiga kura kwa lugha yao ya kinyaturu kana kwamba huo ulikuwa mkutano wa wanyaturu.

Tabia hii ya ukabila hasa kwa wanyaturu isipokemewa itazaa makundi yenye mirengo ya kikabila,jambo ambalo ni hatari kwa ustawi wa demokrasia.


Ndugu wana jamvi, naomba kufafanua kidogo kuhusu ukabila uliotajwa na mtoa maada, kwanza nakushukuru kwa kukiri mwanzoni wa post yako kwamba nilisimamia uchaguzi vizuri kwa kufuata katiba ya Chadema, katiba ndio msingi wa uchaguzi huo, na katiba hiyohiyo haina hata kipengele kimoja kinachosema watu wachaguliwe kwa uwiano wa makabila.... ni vyema kwanza ukajua kwamba kulikuwa na wagombea wangapi wa kinyiramba kwenye kinyang'anyiro hicho na baadae utuambie kwanini walikuwa wachache ukilinganisha na wanyaturu,, halafu sio kweli kwamba walioshinda ni wanyaturu peke yao... yupo mnyiramba Katibu bawacha, yupo mnyamwezi Mwenyekiti Bavicha ambaye alichuana na wanyiramba wawili, yupo mpare Mwenyekiti bawacha aliyewashinda wanyaturu wawili....nawashauri ndugu zangu wanajamvi, tuache kufukua ardhi kwa lengo la kutafuta sumu badala yake tusema ukweli kuhusu mambo halisi yalivyofanyika ili tusiipotoshe jamii.
 
singida karibu wote ni wanyaturu na wanyiramba ambao lugha zao zinaingiliana.
kwahiyo uwenda wameamua kutumia lugha ili kujaribu kuwashawishi wapiga kura kuwachagua.
Ila wakazi wa singida waepuke kutumia lugha yao kila sehemu yenye mkusanyiko wa watu tofati
 
Niwapongeze wapiga kura kwa kutambua kuwa wanyiramba wangewaangusha kwani hawakawii kununuliwa na mwigulu nchemba, mambo iko kwa LISSU.

Isichukuliwe kama ni ubaguzi, bali mtambue kuwa ni utani wa jadi, wanyiramba wamepumbazwa na rushwa za kina madelu, jairo, kiula n.k
 
acha kudanganya watu mbona mie mnyiramba cjalalamika na nilikuwepo kwenye uchaguzi, ina maana watu kutumia lugha zao ni kubaguana? kwanza sisi wanyiramba na wanyaturu tunafahamiana maana ni watani na hata tukiongea lugha zinaingiliana, ndo maana lugha zote pale pale zilitumika labda kama mnyaturu au mnyiramba angeongea akiwa Tabora Au Morogoro ndo ingekuwa hoja!
 
acha kudanganya watu mbona mie mnyiramba cjalalamika na nilikuwepo kwenye uchaguzi, ina maana watu kutumia lugha zao ni kubaguana? kwanza sisi wanyiramba na wanyaturu tunafahamiana maana ni watani na hata tukiongea lugha zinaingiliana, ndo maana lugha zote pale pale zilitumika labda kama mnyaturu au mnyiramba angeongea akiwa Tabora Au Morogoro ndo ingekuwa hoja!

Achana naye mkuu! hata siasa hazijui.
 
Mkoani singida kabila ni wanyaturu ndo mengine yakafata kama wanyiramba, wagogo,wasukuma,wachaga n.k. Wanyaturu kutumia lugha yao ni sababu ya wingi wao. Hoja yako mufilisi sana kawadanganye wanaokuzwa kwa kuku wa kukuzwa na ARVS.
 
Ndugu wana jamvi, naomba kufafanua kidogo kuhusu ukabila uliotajwa na mtoa maada, kwanza nakushukuru kwa kukiri mwanzoni wa post yako kwamba nilisimamia uchaguzi vizuri kwa kufuata katiba ya Chadema, katiba ndio msingi wa uchaguzi huo, na katiba hiyohiyo haina hata kipengele kimoja kinachosema watu wachaguliwe kwa uwiano wa makabila.... ni vyema kwanza ukajua kwamba kulikuwa na wagombea wangapi wa kinyiramba kwenye kinyang'anyiro hicho na baadae utuambie kwanini walikuwa wachache ukilinganisha na wanyaturu,, halafu sio kweli kwamba walioshinda ni wanyaturu peke yao... yupo mnyiramba Katibu bawacha, yupo mnyamwezi Mwenyekiti Bavicha ambaye alichuana na wanyiramba wawili, yupo mpare Mwenyekiti bawacha aliyewashinda wanyaturu wawili....nawashauri ndugu zangu wanajamvi, tuache kufukua ardhi kwa lengo la kutafuta sumu badala yake tusema ukweli kuhusu mambo halisi yalivyofanyika ili tusiiposhe jamii.
 
Back
Top Bottom