Uchaguzi mkuu wa mwaka 2030, ndio mwanzo wa mwisho wa CCM! Wajinga karibu wote watakuwa wamemalizika!

Uchaguzi mkuu wa mwaka 2030, ndio mwanzo wa mwisho wa CCM! Wajinga karibu wote watakuwa wamemalizika!

Pascal Mayalla

Platinum Member
Joined
Sep 22, 2008
Posts
57,103
Reaction score
128,718
Wanabodi,
Nimenote baada ya matokeo ya Kinondoni na Siha, kuna watu wanajifanya na kujidai wamekasirika sana!, na wako tayari kwa lolote na kufanya lolote kuiondoa CCM madarakani!. Ushauri wangu kwa watu wa type hii, ni kuwaasa kwa sasa wasijisumbue bure!, CCM is there to stay for a long long time!, kwasababu mpala sasa Tanzania hapa tulipo, bado hatuna any serious opposition, ya kuiondoa CCM madarakani, labda mpaka 2030, ndipo CCM itaanza tena kutikiswa tikiswa na opposition ili kufungashwa virago, viginevyo CCM itaendelea kutawala na probably, itatawala milele nchini Tanzania if nothing changes!.

Siasa ni sayansi, kuna sayansi ya siasa. Kinachoifanya CCM iendelee kushinda chaguzi mbalimbali na kuendelea kutawala ni matumizi sahihi ya mtaji mkuu wa CCM ilionao, ambao ni watu, na haswa wa vijijini, ambako CCM ime invest a lot on ignorance na lindi la umasikini wa kutupa uliotopea, hivyo as long as mtaji huu upo, na unaendelea kuwepo, CCM itaendelea kutawala daima dumu!.

Kufuatia idadi kubwa ya Watanzania walio wengi, wanaishi vijijini kwenye lindi la umasikini uliotopea na ambao wengi wao ni watu goi goi wajinga wa kutupa, walioishia darasa la saba, hivyo hawajui huwa wanachagua nini!, hawa wataendelea kuichagua CCM mwaka hadi mwaka na kila uchao!.

Idadi ya goi goi na wajinga hawa ni kubwa kuliko idadi ya Watanzania werevu, wanaojitambua na kuwa na uwezo wa kufanya kitu kinachoitwa "informed decisions", hivyo watu wanaichagua CCM kwa mazoea tuu, na kuna maeneo CCM hata ikisimamisha jiwe, jiwe litapita.

Kufuatia rais Dr. John Pombe, Joseph Magufuli kutoa elimu ya bure kwa Watanzania wote, batch ya kwanza ya wanafunzi walioanza darasa la kwanza la bure, watapiga kura kwa mara ya kwanza uchaguzi wa mwaka 2030, hivyo hawa hawatakuwa wajinga wajinga tena!
, wa kupelekwa pelekwa kama mazuzu!, na Tanzania ya viwanda, mapinduzi ya kilimo na uchumi wa gesi, utaigeuza Tanzania kuwa nchi ya uchumi wa kati, hivyo kupunguza ule umasikini uliotopea, sasa huu ndio utakuwa mwanzo wa mwisho wa CCM!.

Angalizo: Nimesema ni mwanzo wa mwisho wa CCM, sijasema ni mwisho wa CCM!. Hivyo kipindi chote hiki kutoka sasa hadi hiyo 2030, CCM haitajikalia tuu hivi hivi tuu kusubiria kufa kibudu, CCM wakati wote itakuwa busy kutekeleza ilani yake ili muda wa uchaguzi ulifika, CCM iibuke na kusema tuliahidi, tumetekeleza, hivyo kuzidi kujiimarisha ili kuendelea kutawala milele!.

Wengi wa wajinga wajinga waliokuwa wanaichagua CCM kwa mazoea tuu, most of them will have been long gone! na masikini wa kutupwa wenye kuweza kuuza kura yao kwa T-shirt na kofia, na shibe ya siku moja, watakuwa wamepungua!, mimi mwenyewe will be at 60s!.

Hata hivyo sio wote wanaiochagua CCM ni wajinga wajinga, kuna wengine wenye akili zao timamu, wanaichagua CCM kwa sababu hakuna alternative, hatuna any serious, credible opposition to choose from, upinzani uliopo ni upinzani uchwala. Wapinzani hawana hoja, wanatumia hoja za nguvu, badala ya nguvu za hoja, wamekalia siasa za matukio!.

Wapinzani mtanisamehe kuwaita Upinzani Uchwala, kwa sababu huu ndio ukweli wenyewe!. CCM ilikwisha chokwa siku nyingi ila kukosekana kwa upinzani imara kumewakatisha tamaa waliowengi na kuamua kutokupiga kura, badala ya kupoteza muda!, kwa sababu haoni cha kuchagua!.

Upinzani uliopo ni upinzani wa kupinga kila kitu, kupayuka, kutukana na kuhamasisha chuki, na uvunjifu wa amani kwa kutumia hoja za nguvu, badala ya kutumia nguvu za hoja, Upinzani wa kweli ni upinzani wenye hoja mbadala. Upinzani huu tulionao, bado haujaonyesha ukomavu wa kutosha kuaminiwa na kukabidhiwa ikulu yetu, hivyo japo CCM ni Li Zimwi, hili ndilo zimwi Watanzania walijualo!.

Hivyo wale wote wenye hasira na CCM, nawashauri washushe pressure zao, kwa sasa kwa siasa za Tanzania, mpango mzima ni CCM, uchaguzi wa 2020, karibu majimbo yote yaliyokuwa yanashikiliwa na upinzani, yatarejeshwa CCM, na Tanzania kuwa nchi ya chama kimoja, kwa miaka 10, kuanzia 2020 hadi 2030.

Hiki ni kipindi cha upinzani kujijenga upya, kwa kuhakikisha, tunabadili sheria ya uchaguzi, kuutoa ujinga wa kudhaminiwa na vyama na kuruhusu wagombea binafsi, tunasawazisha uwanja wa mchezo wa siasa kwa kutengeneza a level playing field, ili kufanya uchaguzi katika ushindani sawia, na kuifanyia maboresho Tume ya Taifa ya Uchaguzi ambayo japo ni Tume Huru ila sio Inclusive, hivyo Tume itafanywa more inclusve ili kuwapata viongozi wasio na vyama, na makamishna, wajumuishe wawakilishi wa vyama vikubwa angalau toka vyama vitatu vikuu. Na hapa sasa ndio tutaona kuibuka kwa upinzani wa kweli ambao utaanza tena 2030!.

I pray to God, to grant me the privilege to witness this day.

Paskali
 
Wanabodi,
Nimenote baada ya matokeo ya Kinondoni na Siha, kuna watu wanajidai wamekasirika sana na wako tayari kufanya lolote kuiondoa CCM madarakani!. Ushauri wangu kwa watu hawa ni kwa sasa wasijisumbue, CCM is there to stay mpaka 2030, ndipo itaanza kufungashwa virago.

Siasa ni sayansi, kuna sayansi ya siasa. Kinachoifanya CCM iendelee kushinda chaguzi mbalimbali na kuendelea kutawala ni kwa sababu idadi ya Watanzania ambao ni wajinga na hawajui wanachagua nini ni kubwa kuliko idadi ya Watanzania waliojitambua na kuwa na uwezo wa kufanya informed decisions.

Kufuatia rais Dr. John Pombe, Joseph Magufuli kutoa elimu ya bure kwa Watanzania wote, batch ya kwanza ya wanafunzi walioanza darasa la kwanza la bure, watapiga kura kwa mara ya kwanza uchaguzi wa mwaka 2030, hivyo hawa hawatakuwa wajinga wajinga tena, kupelekwa pelekwa kama mazuzu!, hivyo sasa huu ndio utakuwa mwanzo wa mwisho wa CCM!.

Wengi wa wajinga wajinga waliokuwa wanaichagua CCM kwa mazoea tuu, most of them will be long gone, mimi mwenyewe will be at 60s!.

Hivyo wale wote wenye hasira na CCM, nawashauri washushe pressure zao, kwa sasa kwa siasa za Tanzania, mpango mzima ni CCM, uchaguzi wa 2020, majimbo yote yaliyokuwa yanashikiliwa na upinzani, yanarejeshwa CCM, na Tanzania kuwa nchi ya chama kimoja, kwa miaka 10, kuanzia 2020 hadi 2030.

Hiki ni kipindi cha upinzani kujijenga upya, na upinzani utaanza tena 2030.

I pray to God, to grant me the privilege to witness this day.

Paskali
Nakubaliana nawe
 
Pascal Mayalla unaongea kitu gani ndugu yangu, afadhali ya ujinga wa kutokwenda darasani kabisa kuliko huu ujinga uliopo sasa hivi, angalia maelezo ya viongozi wa usalama na jeshi letu kuhusu kifo cha mwanafunzi wa tukio la Kinondoni ndio utajua kansa ya ujinga unaotutafuna, huo hautoki kwa kwenda shule.

PhD holders, Maprofesa, achilia mbali tuliokua tunawahesabu wasomi wanavyofanya mambo ya hovyohovyo, huo ujinga wa aina hii usipofikia tamati CCM itatawala milele.
 
Kwa mtindo wa uchaguzi wa juzi 2020 hamna mpinzani atakayerudi bungeni.

Hii ni kama imeshaamriwa kama sio kupitishwa kwamba, kuanzia sasa na kuendelea, uchaguzi wowote kuanzia wa mjumbe wa nyumba kumi kumi hadi kile cheo cha juu kabisa, lazima chama kuu liibuke kidedea, iwe kwa GHARAMA yeyote ile.

Bora wananchi tuachane kabisa na haya mambo ya kupiga kura tufanye mambo ya muhimu...
 
Huko 2030 kama ndio mwanzo wa mwisho wa sisiemu, poa tu! Huko sidhani kama hawa upinzani uchwara watakuwa na pumzi, mbowe na genge lake watakuwa hoi bin taaban wameshastaafu, hapo kweli upinzani mpya utaanza kuzaliwa.

Ila kinachosikitisha zaidi ni kina Yericko Nyerere ndio watakuwq figure head wa upinzani. Bado kazi ni pevu.
 
Hii ni kama imeshaamriwa kama sio kupitishwa kwamba, kuanzia sasa na kuendelea, uchaguzi wowote kuanzia wa mjumbe wa nyumba kumi kumi hadi kile cheo cha juu kabisa, lazima chama kuu liibuke kidedea, iwe kwa GHARAMA yeyote ile.

Bora wananchi tuachane kabisa na haya mambo ya kupiga kura tufanye mambo ya muhimu...
Haswa, sipotezii tena muda wangu kupiga kura nchi hii
 
Kufuatia rais Dr. John Pombe, Joseph Magufuli kutoa elimu ya bure kwa Watanzania wote, batch ya kwanza ya wanafunzi walioanza darasa la kwanza la bure, watapiga kura kwa mara ya kwanza uchaguzi wa mwaka 2030, hivyo hawa hawatakuwa wajinga wajinga tena, kupelekwa pelekwa kama mazuzu!, hivyo sasa huu ndio utakuwa mwanzo wa mwisho wa CCM!.

Batch yenu mliosomeshwa bure na nyerere mlianza lini kupiga kura?,je mliiondoa ccm au ni miongoni mwa wajinga watakaoisha 2030.

Chama kinaondoka madarakani kikishindwa kutekeleza ilani walau chini ya 50% na si kwa kuangalia nchi ina watu wangapi wamesoma

Kingine ni aina ya viongozi wa upinzani,hata nchi nzima tuwe maprofessor,usitegemee upinzani kwenda ikulu kama kuna watu aina ya mbowe na genge lake
 
To be true hii nchi ina wafu wengi wanaotembea!! Mleta mada ana hoja ya msingi sana!! Pamoja na kelele nyingi za walioshindwa but hoja ya upumbavu na ujinga uliokithiri kwa wapiga kura ina mashiko!!

Ktk hali ya kawaida ni wazi watu wetu wengi hasa CCM ni marehemu wasiojua wanataka na kuchagua nini!!

KINYAA!!
 
2030 ni ngumu sana, ukumbuke kuwa rais atakae chaguliwa mwaka 2025 atakuwa madarakani kwahiyo hatakubali kuondoka kizembe
 
Back
Top Bottom