tatum
JF-Expert Member
- Jan 16, 2018
- 5,786
- 4,490
Kufuatia majimbo kutangazwa na Tume ya Uchaguzi kufanyika uchaguzi wa marudio kufuatia majimbo hayo kuwa wazi kutokana na wabunge waliochaguliwa mwaka 2015 kuhamia CCM na Mbunge mmoja kufariki baada ya kuugua ghafla Hospitali ya Taifa ya Muhimbili akiwa anaendelea na vikao vya Bunge kuna uwezekano mkubwa sana kwa majimbo hayo ambayo yalikuwa chini ya chama cha Chadema kuchukuliwa na chama cha CCM kutokana na kila kinachaminika kuwa vyama vya upinzania kutokuwa na sera na imani wanayoisimamia kwa sasa baada ya wabunge wengi na madiwani kuhama vyama vya upinzania na kuhamia CCM kwa hiari yao wenyewe.
Kesho kuna maadhi ya majimbo yanafanya uchaguzi na mengine ni September mwaka huu uwezekano ni mkubwa sana wa majimbo hayo kwenda CCM kutokana na CCM walivyojipanga kuhakikisha wanachama wao wanapiga kura za kutosha ili kuibuka kidedea kwenye hizo chaguzi ndogo.
Mara nyingi kwenye uchaguzi huwa kila mmoja anatafuata mbinu za kuhakikisha anapata wafuasi wengi wa kuwapigia kura kwa kufanya kampeni ktk mikutano ya hadhara kutanga sera zao,kampeni ya makundi kwa makundi na kampeni hata ya nyumba kwa nyumba kama tulivyomuona Mhe Zitto Kabwe kwa baadhi ya maeneo.
Na tukumbuke sana maeneo mengi ya vijijini CCM inakubalika sana na ndiko waliko wapiga kura wengi ambao bado wana imani kubwa na chao chao cha CCM katika kuwahakikishia wanaendelea kuwa na amani,umoja na maendeleo kwa ujumla.
Vyama vya upinzani wanatakiwa kujipanga kisawasawa kupambana na chama hiki dume ambacho kina mizizini toka taifani mpaka mashinani.
Kesho kuna maadhi ya majimbo yanafanya uchaguzi na mengine ni September mwaka huu uwezekano ni mkubwa sana wa majimbo hayo kwenda CCM kutokana na CCM walivyojipanga kuhakikisha wanachama wao wanapiga kura za kutosha ili kuibuka kidedea kwenye hizo chaguzi ndogo.
Mara nyingi kwenye uchaguzi huwa kila mmoja anatafuata mbinu za kuhakikisha anapata wafuasi wengi wa kuwapigia kura kwa kufanya kampeni ktk mikutano ya hadhara kutanga sera zao,kampeni ya makundi kwa makundi na kampeni hata ya nyumba kwa nyumba kama tulivyomuona Mhe Zitto Kabwe kwa baadhi ya maeneo.
Na tukumbuke sana maeneo mengi ya vijijini CCM inakubalika sana na ndiko waliko wapiga kura wengi ambao bado wana imani kubwa na chao chao cha CCM katika kuwahakikishia wanaendelea kuwa na amani,umoja na maendeleo kwa ujumla.
Vyama vya upinzani wanatakiwa kujipanga kisawasawa kupambana na chama hiki dume ambacho kina mizizini toka taifani mpaka mashinani.