Ubora wa maji ya Kilimanjaro unatia shaka!

ilogelo

JF-Expert Member
Jul 30, 2015
726
710
Kwa kipindi cha takribani miezi miwili, kumekuwa na maji ya kilimanjaro yenye chumvi tofauti na kilimanjaro iliyozoeleka.

Najua watumiaji wa maji haya tu wengi, ikiwa ni watu binafsi na taasisi binafsi na za umma. Vikao, mikutano na hafla zote muhimu huwezi kukuta maji tofauti na kilimanjaro.

Na ukweli usiopingika kwamba, hali hii inatokana na ubora wa maji haya pendwa ya kilimanjaro. Lakini ninachelea kusema kwamba kumbe ni kweli mgema akisifiwa tembo hulitia maji. Kama haya maji yanazalishwa na Bonite bottlers, basi kampuni inatakiwa itoe maelezo kwa wateja wake kuhusu chanzo halisi cha maji haya badala ya kutuandikia Shirimatunda ilhali yanonyesha ni ya kisima.

Na kama kuna uchakachuaji pahala basi kampuni itoe tamko ili kuwalinda watumiaji wa maji haya.

Ninajua humu jukwaani hawawezi kukosekana watu wa kampuni. Na nimeliweka hapa baada ya kutopata namna ya kuwasilisha malalamiko kwa kampuni kwani, kwenye chupa kuna sanduku la posta tu. Hakuna email wala namba ya simu.

Kazi njema.
 
Ahsante mkuu kwa kuliona hilo maana na mimi nilidhani hii kero naihisi peke yangu.
Kiukweli tangu kero hiyo ilipojitokeza nimeamua kuwa mdau wa maji ya AFYA ni mazuri sana,Maji ya KILIMANJARO ilikuwa zamani na ilikuwa siyo mtu wa kawaida utaona anakunywa hovyo hovyo,na ukikuta mtu nakunywa maji ya KILIMANJARO lazima utakuta kapaki ndinga pembeni,doooo kiukweli yalikuwa na heshima na hadhi fulani hivi ya kustaajabisha!

#AFYA
 
Sasa hv kampuni ya kilimanjaro haiuzi yenyewe direct kwa wateja inachofanya imeruhusu au imewapa mawakala kuuza so mawakala wanaenda kuchukua kiwandani then wanasupply madukani na hapo ndo uchakachuaji unapofanyika hii kitu nahisi imeanza miezi miwili hv ni kosa kubwa sn wamefanya kuwatumia mawakala imesababisha ongezeko la maji feki mtaan
 
Nikishaacha kuyanywa hayo maji miaka 2 iliyopita nadhani ni baada ya kukutana aina hiyo ya test ya kachumvi kwambaaali yaan sio yale maji ya awali kabisa ukiyanywa kiu inakatika poa...... Mi nadhan hiyo brand ishahuka thamani uenda wakawa wanatufungia maji ya bahari hao si bure..... Anashindwa hata na maji ya bhakhresa
 
Sio miez ina miaka 2 tayari mkuu mie nishayakataaga kitambo kwel
Sasa hv kampuni ya kilimanjaro haiuzi yenyewe direct kwa wateja inachofanya imeruhusu au imewapa mawakala kuuza so mawakala wanaenda kuchukua kiwandani then wanasupply madukani na hapo ndo uchakachuaji unapofanyika hii kitu nahisi imeanza miezi miwili hv ni kosa kubwa sn wamefanya kuwatumia mawakala imesababisha ongezeko la maji feki mtaan
 
Kwa kipindi cha takribani miezi miwili, kumekuwa na maji ya kilimanjaro yenye chumvi tofauti na kilimanjaro iliyozoeleka.

Najua watumiaji wa maji haya tu wengi, ikiwa ni watu binafsi na taasisi binafsi na za umma. Vikao, mikutano na hafla zote muhimu huwezi kukuta maji tofauti na kilimanjaro.

Na ukweli usiopingika kwamba, hali hii inatokana na ubora wa maji haya pendwa ya kilimanjaro. Lakini ninachelea kusema kwamba kumbe ni kweli mgema akisifiwa tembo hulitia maji. Kama haya maji yanazalishwa na Bonite bottlers, basi kampuni inatakiwa itoe maelezo kwa wateja wake kuhusu chanzo halisi cha maji haya badala ya kutuandikia Shirimatunda ilhali yanonyesha ni ya kisima.

Na kama kuna uchakachuaji pahala basi kampuni itoe tamko ili kuwalinda watumiaji wa maji haya.

Ninajua humu jukwaani hawawezi kukosekana watu wa kampuni. Na nimeliweka hapa baada ya kutopata namna ya kuwasilisha malalamiko kwa kampuni kwani, kwenye chupa kuna sanduku la posta tu. Hakuna email wala namba ya simu.

Kazi njema.
Maji ni uduzungwa
 
Sasa hv kampuni ya kilimanjaro haiuzi yenyewe direct kwa wateja inachofanya imeruhusu au imewapa mawakala kuuza so mawakala wanaenda kuchukua kiwandani then wanasupply madukani na hapo ndo uchakachuaji unapofanyika hii kitu nahisi imeanza miezi miwili hv ni kosa kubwa sn wamefanya kuwatumia mawakala imesababisha ongezeko la maji feki mtaan
Kama hii ndo sababu, basi mwisho wa siku atakayeumia ni kampuni mama. Hakuna kitu kinaudhi kama kununua kitu halafu ukaishia kile ambacho hujakitarajia.

Ukweli katika biashara ni tunu adimu ambayo sisi Watanzania baadhi yetu hatuna hivyo kuishia kujiharibia sifa tuliyoijenga kwa gharama na muda wetu.
 
Back
Top Bottom