Ubora na mapungufu ya "First eleven" ya SIMBA Mnyama

The hammer

JF-Expert Member
May 17, 2011
2,381
1,760
1:Vicent Angban

Anaweza kupanga safu yake ya ulinzi vizuri.Ni goalkeeper ambaye hajawahi kupata kashi kashi yoyote ambayo inaweza kumpima uwezo wake.Ingekuwa si uimara wa safu ya ulinzi wa Simba,basi huyu goalkeeper angekuwa ndo kipa mbovu kuliko wote katika msimu wa ligi kuu Tz bara.Kimo chake kinamfanya mipira inayotambaa chini kuwa tabu kwake na upana wa goli haukadirii ipasavyo.

2:Bokungu.
Ni mchezaji imara na anajua kukaba vyema na kulinda upande wake usiwe chanzo cha matatizo langoni mwake.Tatizo lake hana mbio sana na hivyo hawezi kupandisha mashambuli ipasavyo.Tatizo hilo limetatuliwa kwa kuwepo kichuya ambaye ana mbio na anauwezo wa kumiliki mpira katika winga ambayo alitakiwa Bokungu kusaidia team inaposhambulia.

3:Mohamed Hussein.
Ni mlinzi anayejituma sana,ana control nzuri ya mpira na ana mbio kiasi.Tatizo lake anapopiga mpira iwe cross,kona au foul hanyanyui mpira juu kiasi kwa kama ni kona,foul au cross basi mipira mingi inaishia kwa mlinzi wa kwanza tu.Pia ana tabia akipata mpira ana nyanyua kichwa juu akiwa anaangalia mahali pa kupeleka mpira,yes ni sahihi lakini inakuwa sahihi sana iwapo upo nyuma sehemu kama mita 18 na hakuna adui ila si katikati ya uwanja na mara kwa mara ananyang'anywa mpira kwa style hii.

4:Mwanjali
Anaweza na ni mlizi mzuri(Kasoro zake sijazitambua bado)

5:Murshid
Ni mlinzi mzuri na wa kutumainiwa sana,anajua kukaba na anashambulia pia pale team inapopoteza matumaini ya kurudisha goli.Tatizo lake anacheza madhambi sana kiasi kwamba mnaweza kufanya sub isiyopangwa kwa kuogopa red card.

6:Mkude
Amekuwa nguzo muhimu pale katikati ana control na anajuwa kugawa mipira.

7:Kichuya.
Ana kasi na ana uwezo mkubwa wa kumiliki mpira,ana kasi na anajua kupiga mipira ikalenga goal.Sijaona tatizo lake sana.

8: Mzamiru Yassin
Ana uwezo wa kuchezesha team na kugawa mipra ipasavyo.Tatizo lake pasi zake wakati mwingine ni za hovyo na zisizo na macho.

9:Mavugo
Huyu sasa amekuwa kama wale nyoka wasio na madhara.Mashabiki walikuwa na matumaini makubwa sana kuliko Okwi ila sasa imekuwa tofauti.Anajua kuuchezea mpira na kuumiliki ila inapofikia hatua ya yeye kugawa mpira kwa mtu aliyeko katika nafasi ya kufunga ndipo utakapoona vioja..ni mchoyo sana na anajali matokeo yake yeye kuliko ya team,na hii ni kutokana na alichofikiria ni tofauti na anayoyakuta field ni kama vile student anasoma UDSM then anawaza akihitimu tu atapata ajira na mwaka mmoja kazini atakuwa na nyumba,gari na mtoto mkali ndani but akiwa fueld sasa miaka 4 no ajira no money unafikiri nini kinatokea.

10:Ajib

Ni mshambuliaji mzuri,anajua kuuchezea mpira na kuhadaa walinzi na kutoa pasi.

11: Kazimoto
Anajitahidi sana na anajua kuchezesha team na kugawa mipira.Tatizo anachoka hasa kipindi cha pili na anahitaji awe na msaidizi sio wa kumaliza dk 90 hii ni kutokana umri unakaribia kufikia tamati katika mchezo wa mpira wa miguu.

Sub

1:Manyika
Ni mzuri kuliko Angban ila hajapewa nafasi labda kuna sababu kadhaa za kinidhamu.

2:Lufunga
Ni mzuri ila timing ya kukaba inamsumbua hivyo Murushid atabaki kuwa bora zaidi kuliko Lufunga.

3:Blagnon
Ana uwezo mzuri hata kuliko Mavugo ila bado hajajiamini tu katika ligi ya Tz.
 
Mwaka huu tutashuhudia kila aina ya majisifu...utafikir Simba itachukua kombe la dunia
Sio majisifu mkuu,mbona nimetoa kasoro za wachezaji kibao wa Simba kama M.Hussein mimi kiwango chake hasa anavyopiga kona,foul au cross zake sizipendi na si muamini saaana hasa akikitana na mchakamchaka wa Waarabu huyo M.Hussein si chochote
 
Ivi Vicent Angban, hakuanza msimu huu kuchezea Simba, iweje usimjuwe uzuri wake au ubaya wake, ama mwaka jana ulikua nje ya nchi?
 
Ivi Vicent Angban, hakuanza msimu huu kuchezea Simba, iweje usimjuwe uzuri wake au ubaya wake, ama mwaka jana ulikua nje ya nchi?
Toka Angban asajiliwe na kipindi chote alichokuwa langoni hajawahi kupata misukosuko aliyopata kama Dida,AishiManula n.k. Yeye likipigwa ni goli au shuti hafifu amedaka.Umeshamuona Angban amegalagala chini kwa maumivu ya ku-save mpira au kugongana na mcgezaji katika harakati za kuokoa mpira usiingie langoni.Nikuambie,anaingia akiwa msafi na anatoka hivyo hivyo na jezi zake nyeupe.
 
Toka Angban asajiliwe na kipindi chote alichokuwa langoni hajawahi kupata misukosuko aliyopata kama Dida,AishiManula n.k. Yeye likipigwa ni goli au shuti hafifu amedaka.Umeshamuona Angban amegalagala chini kwa maumivu ya ku-save mpira au kugongana na mcgezaji katika harakati za kuokoa mpira usiingie langoni.Nikuambie,anaingia akiwa msafi na anatoka hivyo hivyo na jezi zake nyeupe.
Simba, simba ya mwaka jana ilikua simba ya kawaida sana, ilikua inapata misukosuko sana, unakumbuka timu ilikua inacheza vizuri kipindi kimoja tu, kuumia kwa kipa au kugalagala hakuamanishi kuwa kipa mzuri, kwa sababu hizi unatudanganya ndugu. Haiwezekani Timu bingwa kipa wake apate misukosuko kuliko timu iliyoshika nafasi ya tatu. Hivi umeshawa kumsikia mchezaji alikua anaitwa Samli Ayubu wa majimaji, alikua anaitwa beki mstarabu kwa sababu zipi unazijua, unazani alikua mchezaji m- bovu hebu uliza watu wa zamani wakwambie.
 
Hii Simba ya mwaka huu bora ya mwaka jana,kinachowasaidia kwa sasa ni kushuka kwa viwango vya wapinzani wao hasa Yanga na Azam.
 
Ubora au Mapungufu upo machoni kwa kwa mtazamaji.. Kama hayo unayoyaita mapungufu yangekuwepo.. Simba S.C isingekua inagawa dozi nzito nzito.. Na isingekua inaongoza ligi mpaka sasa.
Kwangu mimi na wapenzi lukuki wa soka.. Tunaamini
Simba S.C hii ni miongoni Mwa timu bora kabisa katika ukanda huu wa CECAFA.
 
Ubora au Mapungufu upo machoni kwa kwa mtazamaji.. Kama hayo unayoyaita mapungufu yangekuwepo.. Simba S.C isingekua inagawa dozi nzito nzito.. Na isingekua inaongoza ligi mpaka sasa.
Kwangu mimi na wapenzi lukuki wa soka.. Tunaamini
Simba S.C hii ni miongoni Mwa timu bora kabisa katika ukanda huu wa CECAFA.
Hakuna mchezaji asiye na mapungufu yake na kugawa dozi si kwamba wachezaji wa Simba hawana mapungufu.Jaribu kuona kona za M.Hussein kwamba huwa zinaishia wapi.
Mtazame Bokungu hasa speed,nenda kwa Angban,yaani mpira hadi unamgonga bahati mbaya bila kujua ulishamfikia.Mbona sijasema kwaMwanjali au Mkude.Mapungufu yapo na wengine mapungufu yao ni makubwa sana.

Ubora wa Simbasi sawa na ule wa Yanga msimu uliopita.Mimi ni mpenzi wa Simba ila ukweli lazima usemwe.

Kwa msimu huu,pale katikati angekuwepo angalau Kiiza,Simba ingepata ushindi wa kutosha sana.
 
Ni dhahiri kabisa Angban sio mlinda mlango mzuri,ni kama pazia tu pale na sijui kocha anampendea nini yule mlinda mlango.

Leo Simba wamecheza kwa dharau kipindi cha kwanza wakiwa na uhakika wa kushinda.Hili ndo tatizo la Simba siku zote.
 
Ubora au Mapungufu upo machoni kwa kwa mtazamaji.. Kama hayo unayoyaita mapungufu yangekuwepo.. Simba S.C isingekua inagawa dozi nzito nzito.. Na isingekua inaongoza ligi mpaka sasa.
Kwangu mimi na wapenzi lukuki wa soka.. Tunaamini
Simba S.C hii ni miongoni Mwa timu bora kabisa katika ukanda huu wa CECAFA.
Kama ilivyogawa dozi leo kwa African Lyon mkuu!
 
Back
Top Bottom