Mkuu
qnizxy
Nimepita hapo muda hivyo naamini mambo mengi yanaweza kuwa sivyo yalivyo leo, kwa uchache strength ya Udom wakati uko chuoni ni malazi, nadhani ndio chuo pekee bongo ambacho mwanafunzi anaweza kuwa na uhakika na malazi kwa miaka yake yote atayokuwa chuoni. Pili mazingira mazuri ya kusoma, chuo kimejitenga na kina majengo ya kutosha kwa ajili ya madarasa kwa kujisomea au kufanya chochote bila kuhangaika na venue.
Kitaaluma, wakati nipo kuna baadhi ya college kweli zilikuwa shida kwa njia moja au nyingine(Kila college ina kautawala kake) lakini watu wa Informatics na walimu walikuwa makini sana na wanachofanya na hata baada ya kutoka chuo sifa zao zinasikika sijui sasa labda na wengine wameunga. Pia kuna baadhi zilikuwa matatizo kama watu wa biashara.
Udhaifu wa Udom ilikuwa maji aisee, ni shida, kuanzia ya kunywa mpaka ya matumizi mengine. Maji yalikuwa na ladha ambayo wengi hawakuipenda hivyo kuna bajeti ya kununua maji maisha yako yote chuoni labda uridhike nayo, pili maji kwa ujumla ni tatizo hasa chuo cha walimu, social sciences na humanities angalau(Nimeishi hivyo viwili).
Udom kuitwa chuo cha kata nadhani ni just a myth, labda mwanzo watu wenye vigezo hafifu waliweza kudahiliwa hasa walikuwa wanalinganisha na UD au kuchukua wanafunzi wengi etc lakini all in all Udom ni chuo bora kuliko vyuo vingi sana nchini.
Mwisho kwa mawazo yangu, chuoni is about mhusika hasa chuo ambacho kimejumuisha kada nyingi tofauti na watu wengi wenye utaalamu tofauti. Ni sehemu pekee ambao unaweza kujifunza vitu unavyopenda/unavyohitaji kwa gharama nafuu au bure na kuwa mhitimu bora baadae ukizingatia muda loose chuoni ni mkubwa sana, mimi nafanya kitu tofauti na nilichosomea kitaaluma na nilijifunzia chuoni kwani wakati naanza chuo nilikuwa mweupe sana kwenye upande huo, kupitia marafiki na kupenda kujua nimekuwa bora sana bila kutoa hata senti tano na naamini nafanya vizuri kuliko hata baadhi ya waliosomea.
NB: Miaka mingi imepita na nimetaja vitu angalau nilikuwa na ufahamu navyo au vilinihusu, unaweza kutafiti upya.