Uandishi Maandazi ndani ya Clouds FM

Uandishi Maandazi ndani ya Clouds FM

Damaso

JF-Expert Member
Joined
Jul 18, 2018
Posts
6,132
Reaction score
10,514
Leo ni siku ya mchezo wa mwisho wa kundi la AFCON, mjadala mkubwa haupo tena uwanjani bali pia kwenye vyombo vya habari. Leo asubuhi baadhi ya waandishi wa Clouds FM wamejikuta wakilaumiwa kwa kile kinachoonekana kama kulazimisha matumaini yasiyo na msingi kwa Watanzania.
images (3).png
Asubuhi ya leo kwenye kipindi cha Power Breakfast nikasikia mahojiano baina ya mwandishi mmoja wa kituo cha Clouds FM akiwahoji wananchi kuhusu game ya leo. Aisee huyo Dickson Masanja sio mwandishi kabsa.
images - 2025-12-30T102128.173.jpeg
Clouds FM mmefeli sana kwa Dickson Masanja, we bwana mkubwa badala ya kuwasilisha uhalisia wa kiwango cha timu ya taifa ya Tanzania, umechagua kusukuma simulizi linaloilinganisha Tanzania na mataifa yenye nguvu na uzoefu mkubwa barani Afrika kama Tunisia? Serious!?
tunisia.webp
Wananchi si wajinga kama waandishi wengi wanavyodhania. Wanaona uchezaji, wanafahamu mapungufu, na wanatambua tofauti ya viwango. Tatizo linapokuja pale ambapo waandishi wanapofanya mahojiano kwa mtindo wa kushinikiza—wakihitaji kusikia jibu moja tu: kwamba Taifa Stars itafuzu ama Taifa Stars ndio Bingwa wa AFCON mwaka huu. Huu si uandishi wa habari huru; ni propaganda isiyo na msingi wowote.
taifa-pict.jpg
Uandishi wa habari wa michezo unapaswa kujengwa juu ya ukweli, takwimu, na uchambuzi wa kitaalamu futailieni waandishi wengine wanaozungumza ukweli. Kukataa kukiri udhaifu wa timu ni kuwakosea heshima mashabiki na wachezaji wenyewe, we dogo unadai kuwa kwenye game ya Nigeria tulicheza vizuri na tukicheza vile leo tutafuzu.
images - 2025-12-30T102128.173.jpeg
Kama taifa, tuna wajibu wa kuikubali hali halisi ya soka letu: bado tuko safarini, bado tunajifunza, na bado hatujafikia kiwango cha vigogo wa Afrika. Waandishi wanapaswa kuwa sauti ya uhalisia, si walazimishaji wa ndoto za Mchana. Dickson Masanja wewe sio mwandishi wa habari kabsa, yaani badala ya kuuliza watu msimamo wao we jamaa unalazimisha watu waitazame Taifa Stars ikiwa na kiwango cha juu kuzidi timu ya taifa ya Tunisia.
 
Tanzania ikitaka kufanikiwa iwekwe sheria wachezaji wa taifa star wasizidi umri wa 23,
Kuna vijana wengi wapo vizuri sana ila siasa zinatumika na kuweka wachezaji wazee eti kwa kisingizio cha uzoefu na ndipo tunafeli pakubwa

Hao wazoefu wangekuwa benchi la ufundi tu ila majukumu ya kucheza wapewe vijana under 23 basi na world cup tutacheza

Huwezi kutenganisha mpira na siasa lakini unaweza kujali taifa lako, ni aibu kuona hata comoro wanacheza vizuri ila sie sasa hata pasi tatu hatuwezi,

Nashauri sasa waziri wa michezo awe samata na naibu msuva hata kwa mpito tu
 
Leo ni siku ya mchezo wa mwisho wa kundi la AFCON, mjadala mkubwa haupo tena uwanjani bali pia kwenye vyombo vya habari. Leo asubuhi baadhi ya waandishi wa Clouds FM wamejikuta wakilaumiwa kwa kile kinachoonekana kama kulazimisha matumaini yasiyo na msingi kwa Watanzania.
Asubuhi ya leo kwenye kipindi cha Power Breakfast nikasikia mahojiano baina ya mwandishi mmoja wa kituo cha Clouds FM akiwahoji wananchi kuhusu game ya leo. Aisee huyo Dickson Masanja sio mwandishi kabsa.
Clouds FM mmefeli sana kwa Dickson Masanja, we bwana mkubwa badala ya kuwasilisha uhalisia wa kiwango cha timu ya taifa ya Tanzania, umechagua kusukuma simulizi linaloilinganisha Tanzania na mataifa yenye nguvu na uzoefu mkubwa barani Afrika kama Tunisia? Serious!?
Wananchi si wajinga kama waandishi wengi wanavyodhania. Wanaona uchezaji, wanafahamu mapungufu, na wanatambua tofauti ya viwango. Tatizo linapokuja pale ambapo waandishi wanapofanya mahojiano kwa mtindo wa kushinikiza—wakihitaji kusikia jibu moja tu: kwamba Taifa Stars itafuzu ama Taifa Stars ndio Bingwa wa AFCON mwaka huu. Huu si uandishi wa habari huru; ni propaganda isiyo na msingi wowote.
Uandishi wa habari wa michezo unapaswa kujengwa juu ya ukweli, takwimu, na uchambuzi wa kitaalamu futailieni waandishi wengine wanaozungumza ukweli. Kukataa kukiri udhaifu wa timu ni kuwakosea heshima mashabiki na wachezaji wenyewe, we dogo unadai kuwa kwenye game ya Nigeria tulicheza vizuri na tukicheza vile leo tutafuzu.
Kama taifa, tuna wajibu wa kuikubali hali halisi ya soka letu: bado tuko safarini, bado tunajifunza, na bado hatujafikia kiwango cha vigogo wa Afrika. Waandishi wanapaswa kuwa sauti ya uhalisia, si walazimishaji wa ndoto za Mchana. Dickson Masanja wewe sio mwandishi wa habari kabsa, yaani badala ya kuuliza watu msimamo wao we jamaa unalazimisha watu waitazame Taifa Stars ikiwa na kiwango cha juu kuzidi timu ya taifa ya Tunisia.
Mpuuzi mwingine hapo clouds ni somebody luambano,ni mtangazaji asiye na maadili kabisa,akipewa tu pesa basi anachukua upande na kuupigia debe hadharani
 
Si afadhal hao mawingu fm ukisikiliza TIMES FM unaweza zimia mkuu hasa kipindi cha saa kumi jion kinaitwa vuvuzela kuna binti huko anaongea kama kameza flash
Namfahamu yule dada 😔 ovyo sana
 
Tanzania ikitaka kufanikiwa iwekwe sheria wachezaji wa taifa star wasizidi umri wa 23,
Kuna vijana wengi wapo vizuri sana ila siasa zinatumika na kuweka wachezaji wazee eti kwa kisingizio cha uzoefu na ndipo tunafeli pakubwa

Hao wazoefu wangekuwa benchi la ufundi tu ila majukumu ya kucheza wapewe vijana under 23 basi na world cup tutacheza

Huwezi kutenganisha mpira na siasa lakini unaweza kujali taifa lako, ni aibu kuona hata comoro wanacheza vizuri ila sie sasa hata pasi tatu hatuwezi,

Nashauri sasa waziri wa michezo awe samata na naibu msuva hata kwa mpito tu
Huyu Dickson anawauliza watu, "Tanzania tunakwenda kushinda magoli mangapi?" wanaojua soka wanakwambia tunakwenda kutolewa, jamaa analazimisha kuwa "kwann hatuipendi timu yetu?" nimecheka kama fala acha tu
 
Mpuuzi mwingine hapo clouds ni somebody luambano,ni mtangazaji asiye na maadili kabisa,akipewa tu pesa basi anachukua upande na kuupigia debe hadharani
Luambano alikuwa zamani! Kuna kipindi alikuwa vizuri sana ila kwa sasa bahasha ndio zimemvuruga kichwa
 
Tatizo ni uchawa ndio mzizi wa mambo yote hayo.

Mtu anaogopa kusema ukweli kwa sababu ya kuogopa mamlaka
 
Tatizo ni uchawa ndio mzizi wa mambo yote hayo.

Mtu anaogopa kusema ukweli kwa sababu ya kuogopa mamlaka
Dogo mpaka akakatisha mahojiano maana ni kama watu walitaka kumtukana! 😃 Power Breakfast ya leo imekuwa ya kipuuzi sijapata kuona
 
Tumefuzu, ndio maajabu ya mpira, ila ukweli utabaki pale pale hatujui mpira ila tunaupenda

So tubadilike sasa tufanye mabo serious
 
Back
Top Bottom