Twashindwa kulima ndio twaweza kiwanda cha dawa?

Twashindwa kulima ndio twaweza kiwanda cha dawa?

MPadmire

JF-Expert Member
Joined
Mar 7, 2006
Posts
3,956
Reaction score
3,245
Sukari tumeshindwa , Je tutaweza viwanda vya dawa?

Ni akili mbovu tu.....Sukari kutoka Brazil or Pakistan iwe cheap kutoka Tanzania?

Sukari ya Brazil na Pakistan iwe bei rahisi kuliko kilombero au Kagera?

Mafuta ya Alizeti ya Sunbelt Lita 3 ni 19,000 na Fresh ya Kenya ni 13000?

Kilimo tumeshindwa..Je tutaweza Viwanda?

Wake up Watanzania...Huu ni usaniii Tanzania ya Viwanda

Hata blender ni kiwanda cha vinywaji...Ooh My God...!
 
Nadhani hoja ya mtoa hoja ni tujikite kwanza kwenye mambo madogo yanayowezekana huku tukijipanga kwa makubwa.
Nimemuelewa na uhenda kuliko ulivyomuelewa. Yeye katoa kejeli eti serikali inafanya usanii! Hajaona juhudi na nia njema.

Kitu kikubwa ni ujasiri wa kuamua makubwa baada ya kujipanga. Yanayofanywa na serikali ya sasa ni Kama maajabu ukizingatia Tanzania ilivyokuwa. Anasema sukari tumeshindwa, sawa anashindwa ku recognise juhudi za kuanzisha viwanda vya sukari. Aulize maendeleo ya Mkulazi kwa muda mfupi namna hii.

Anasema viwanda tumeshindwa, hivi hajui juhudi za kuendeleza viwanda zitachangia kuendeleza kilimo?

Lkn kibaya zaidi anakaa pembeni na kukosoa, haonyeshi kufanya juhudi ya kushiriki sera ya viwanda. Kuna watu wameharibiwa akili kiasi kwamba wanafikiri serikali ni lidude linalojitegemea na wao wanafaa pembeni wanaliangalia na kisha litaonyesha maajabu ndiyo wao wajiunge! Foolish
 
Serikali ya salad inataka kukimbia kabla ya kutembea , JK kilimo kwanza iliishia kwenye makaratasi,JPM viwanda vitaishia kwenye midomo
Ona unavyotumika bila kujitambua!
JPM katoa focus ya uongozi, na ana haki sababu kachaguliwa baada ya kuahidi Hilo kwenye kampeni. Na sisi tukamchagua tukikubaliana na Hilo. Ni jukumu la wewe na mimi kushiriki. Vinginevyo siyo kosa lake
 
Kuna watu walishaambiwa na kiingozi wao ata brenda za kusaga juice nyumbani ni kiwanda. Sasa kwa hili...

Hukawii kusikia ☆wakisha kusanyika Wamasai watano na dawa zao ni kiwanda cha Dawa☆
 
Mafuta ya Korie kutoka Thailand na Malaysia bei ya reja reja Lita ni Tshs 3,600 wakati mafuta ya Alizeti bei ya reja reja kwa Lita ni Tshs 4,600 mpaka Tshs 5,000
Unatamani kuwa Mzalendo, lakini katika pesa, hakuna uzalendo
 
Ndo nimeamini msukuma hata asome vipi,hawanaga akili hata punje wale watu,mfano mtu unaPhD lakn vitu vidogo vimemshinda anadandia vitu ambavyo hata wamarekani vinawatoa kijasho
 
Nadhani hoja ya mtoa hoja ni tujikite kwanza kwenye mambo madogo yanayowezekana huku tukijipanga kwa makubwa.
Yaaani badala ya kupambana kuwaondolea wananchi magonjwa lenyewe linawatia magonjwa watu kwa pressure ya kutolipwa mafao yao
 
Ona unavyotumika bila kujitambua!
JPM katoa focus ya uongozi, na ana haki sababu kachaguliwa baada ya kuahidi Hilo kwenye kampeni. Na sisi tukamchagua tukikubaliana na Hilo. Ni jukumu la wewe na mimi kushiriki. Vinginevyo siyo kosa lake
Mbumbumbu wa karne
 
Mafuta ya Korie kutoka Thailand na Malaysia bei ya reja reja Lita ni Tshs 3,600 wakati mafuta ya Alizeti bei ya reja reja kwa Lita ni Tshs 4,600 mpaka Tshs 5,000
Unatamani kuwa Mzalendo, lakini katika pesa, hakuna uzalendo
Wazalendo watabaki wawili tu jiwe na mkewe makondakta
 
Mfumo wa kodi nyingi usio na tija kwa mzalishaji wa bidhaa na mnunuzi wa bidhaa.

Hivi kweli inakuwaje pamoja na kodi kuwa juu kupindukia lakini pesa inayokusanywa haionekani inaenda wapi.

Maendeleo hakuna na kila mradi ili ufanyike tunakopa fedha, hivi makusanyo yetu yanaenda wapi?

Nchi za wenzetu kodi ni ndogo mno that's why bidhaa inazalishwa huko na gharama ya usafirishaji pamoja na kodi itakayotozwa bado bei zinakuwa chini.
 
Back
Top Bottom