TV aina ya ZUNE

TV aina ya ZUNE

Hamna kitu hapo ni Chinese brand mbaya sana kuna zile sabufa zao ndo kabisa takataka...
Mnapondaga sn vitu vya kichina hasa vyenye majina yasiyo brand kubwa kisa mna ma Samsung na LG za kichina kiuhalisia hapa bongo maelectronics mengi ni ya kichina tu ma HISENSE yanakufa kila sku yakiwa hata hayana mwaka wkati watu wanatumia zunne au star x wanadunda miaka na miaka
 
Mnapondaga sn vitu vya kichina hasa vyenye majina yasiyo brand kubwa kisa mna ma Samsung na LG za kichina kiuhalisia hapa bongo maelectronics mengi ni ya kichina tu ma HISENSE yanakufa kila sku yakiwa hata hayana mwaka wkati watu wanatumia zunne au star x wanadunda miaka na miaka
Kuna mchina wa low budget ambae life span (durability) yake ni ndogo na ikifa inakufa kweli ukianza kutengenezesha ndo kama unafuga ugonjwa kila siku itakua kwa fundi tu...Na kuna mchina gadgets za ubora wa kati na pia kuna mchina gadgets quality nzuri kabisa standards za kimataifa hizi mara nyingi huwa sio rahisi kuzipata huku dunia yetu ya 3 soko lao kubwa ni ulaya na marekani sana ndo hizo huwa zinapelekwa huko..

So overall mchina sio mbaya ila anauza kitu chake accordingly na hali ya maisha ya watu alio walenga ilimradi tu kila mtu awe satisfied kua na alichokua anakitaka kumiliki...

Sasa turudi kwa Zunne hao hao ni mchina wa low quality and durability kuna dogo binamu yangu alikua na Subwoofer lao jipya alinunua halikumaliza hata miezi 6 likafa IC baadae twita zake zikaanza kufa moja baada ya nyingne, kapeleka kwa fundi sana lakini wapi hivi navyokwambia aligawa kwa fundi kama spares tu.

Si Hisense pekee tu zinakufa hata hizo brands kubwa zinakufa, lakini kuharibika kwa electronics devices nyingi kunachangiwa na factors nyingi, umeme wetu pia hauko stable karibu nchi nzima una changamoto sana so kuunguza vifaa vya umeme tunavyomiliki ni kugusa tu na mbaya zaidi majority ya watanzania hawatumii vifaa vya ku regulate kiwango cha voltage though voltage regulators nyingi kubwa na imara ni gharama sana ila hata hizi TV & FRIDGE GUARDS hawanunui unategemea nini? Haya kingine unakuta mtu ana extension cable moja hiyo hiyo anaweka TV, Subwoofer, Fridge, Heater, Pasi, Rice Cooker utegemee kifaa kimojawapo hapo kisipige shoti kweli? Kwanza Extension Cables maximum load ni Amperes 13 na Maximum Watt ni 3000 tu ila unakuta mtu kaiwekea vifaa kibao yanatumia umeme mwingi...

Kifaa chochote cha electronics kinahitaji matunzo na kufata principles za matumizi yake, watu hawasomi hata manual guide akinunua anatupa makaratasi huko hajali mradi anajua akinunua TV basi inatumiaga umeme wowote yaani mradi ikiwaka tu basi kila kitu anahisi kamaliza, vifaa vya umeme vinahitaji uangalizi mzuri ili vidumu..
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom