Tuyaite magari ya taka au magari aina ya taka

Mhache

JF-Expert Member
Jun 20, 2008
345
24
Ni jambo la kawaida kuona magari ya taka yakiwa yameharibika katika maeneo mbalimbali ya jiji la Dar es Salaam, Moshi na hata Arusha. Magari hayo yanapoharibika hukaa kwenye eneo yalipoharibikia kwa siku kadhaa kabla hajatolewa. Cha kushangaza zaidi ni kwamba yanakuwa yana uchafu/taka ambazo wakati likiwa hapo lilipoharibikia uchafu huo huendelea kuoza na kutoa harufu mbaya.

Kwanza hali ya magari hayo ni mbaya kiasi yanakatisha tamaa. Mimi binafsi huwa nashindwa niyaite magari ya taka au yenyewe ni aina ya taka au uchafu. Na baada ya kufanya uchunguzi na kusikiliza kipindi za Mazingira kinachorushwa na Radio One nimegundua kwamba wakati wa kuomba tenda watafuta tenda hupeleka magari mazuri na hata mapya. Baada ya kupata tenda magari yalioonyeshwa wakati wa tenda hayaonekani na hayajulikani yanapopelekwa.

Kuna haja ya serikali kuu, serikali za mitaa kuwa na utaratibu wa kufuatilia magari ya kubebe taka na kuhakikisha checkup zinafanyika kila baada ya muda fulani. Ila mtoa huduma ya taka akilegalega achakuliwe sheria kulingana na taratibu za tenda.
 
Mhache,
Hoja ya msingi sana hii. Ni kwenye mambo madogo madogo kama haya ndipo kero za wananchi zilizonyingi huonekana. Wakurugenzi wa serikali za mitaa na viongozi wahusika wote katika swala zima wanapaswa kutenda kazi zao. Hapa ni mfano dhahiri kuwa kuna watu hawafanyikazi zao za kukagua hayo magari. Swali ni: je watawajibishwa au kuwajibika?

SteveD.
 
Ni jambo la kawaida kuona magari ya taka yakiwa yameharibika katika maeneo mbalimbali ya jiji la Dar es Salaam, Moshi na hata Arusha. Magari hayo yanapoharibika hukaa kwenye eneo yalipoharibikia kwa siku kadhaa kabla hajatolewa...... .

Huku Mwanza mambo ni mazuri kabisa hakuna tatizo kama katika majiji hayo. Ni bora mkaja kujifunza mbinu za ukusanyaji na utupaji taka hapa.pamoja na utunzaji wa Vitendea kazi
chee%20085.jpg

 
Hii ya leo kali sasa inaoneka tanzania imepiga hatuwa kubwa hata kufikia kuwa na magari ya taka au ni mimi nimelewa vibaya ?au mtowa maoni alikuwa na niya kuandika magari ya kubebeya taka?
 
Nashukuri kwa ushauri wako wa kuja kujifunza hapo Mwanza. Nipatapo nafasi nitatembelea Jiji hilo la Mwanza ili kujionea usafi ulivyo. Usiwe mchoyo unaweza ukatueleza jitihada mlizofanya na kuliweka Jiji la Mwanza katika hali ya usafi kwani si wote wataweza kuja Mwanza kujionea hali ya usafi hapo.
 
Kutokuelewa sio tatizo, tatizo ni kutokuelewa ukajifanya umeelewa na kuacha kuuliza. Nilimaanisha magari ya kubebea taka. Ni mabovu kiasi kwamba mtu unashindwa kuyatofautisha na kazi yanayofanya. yenyewe yanaonekana kama takataka.
 
Back
Top Bottom