Tuwasapoti bongo movie katika hili

Jun 8, 2013
42
35
Wanajamvi katika siku za hivi karibuni kumekuwa na maandamano na matamko mengi kuhusu kazi za bongo movie na movie za nje (kikorea) lakini watu hawa wanaoandamana walikosa uwakilishwaji mzuri wa hoja zao mpaka kufika mahali watu kutowaelewa.
UKWELI ni kwamba ni kwel kazi za movie za nje zinaua soko la movie za ndani.
Tunafahamu hitaji(demand) la bidhaa katika soko inategemea sana na vitu vifuatavyo'
Bei ya bidhaa yenyewe(price of commodity). Hapa tuwe wawazi kama bidhaa itauzwa kwa bei kubwa sokoni basi hitaji lake litashuka sana (elastic demand). Hii haiwadhuru bongo movie.
Bei ya bidhaa ya mfanano sokoni(price of related goods). Hii ndio inayowaumiza bongo movie.
Bei ya bidhaa ya mfanano sokoni (movie za nje)ikiwa ndogo kuliko bidhaa yako(bongo movie) basi wanunuzi watapendelea sana kununua ile bidhaa nyingine(movie za nje)kuliko bidhaa yako (filamu za bongo)sokoni. Hata bongo muvi wakitengeneza filamu bora za aina gani haziwezi kulifikia soko la muvi za nje.
Tuungane tuiambie serikali kitu kimoja ifanye filamu za nje nazo zilipe kodi kwa serikali na kupitia hatua zote kama wanazopitia bongo muvi (hapa itafanya bei kupanda na kufanana na bei ya filamu ya bongo) au serikali iwaondolee kodi kabisa bongo movie ili bei za filamu sokoni zifanane ili kuwe na ushindani. Baada ya apo tuwaachie bongo movie waboreshe ubora wa kazi zao.

Maoni yako mdau.
 
Bongo muvi:
  1. Title English, ndani Kiswahili. Sijui kwa nini huwa wanafanya hivi?
  2. Mwanzo wa muvi unatabiri mwisho wake. Sijui kwa nini hawapendi kuishughulisha akili ya hadhira?
  3. Unaweza kuangalia mwanzo mwisho usijue kisa kikuu cha vituko na matukio ya muvi nzima.
  4. Baadhi ya matukio na uhusika wa wahusika hukosa uhalisia.Mfano, Wahusika wengine wanaonekana kabisa wanaigiza badala ya kuonekana wanayaishi hayo maisha ndani ya muvi
Tukiboresha maeneo hayo, tutawapata wateja hata kwa bei kubwa
 
Muv zao ni zipi kwani????manaje ninachokua unapokua na product nzur sokon huna haja ya kuandamana barabaran na kutoa matamko kua bidha inayifanana na yako kutoka nje isiingie ili wewe0 upate soko.Hapo patakuabhakuna ushindan na hutatumia brain kuifanya bidha yakobiwe bora kwakua utabweteka,na kwakua walijiingiza kwenye siasa kwa ahadi hewa kua serekali utawasaidia sasa naona wanakaribia kuomba nguvu ya jeshi maybe ili tynunue kazi zao.Achen ujinga ingien kazin mfanye jitu kizuri muondoe zile watch out part 5,muwe wabunifu enzi za marehem Kanumba mlikua na soko kubwa sanaa kwakua hamkua wanasiasa uchwara mlikua wachapa kazi.Et lile libaba likubwa limekaa mbele linalilia muv za nje zipigwe marufuku dah aibu hii.Angalau mngeomba hzo muv za nje zipigwe kodi kubwa ningewaelewa
 
Yaani CD ya Iris iuzwe 5000 na CD ya bongo movie iuzwe 5000 yaani niache Iris nichukue bongo movie ni kama vile dagaa wa kigoma wauzwe bei sawa na wa mwanza nani atawanunua wa mwanza?

Mfano season mpya ya prison break iliyotoka leo hii iwekwe sokoni na picha zenu za bongo movie tuone kama haitouzika

Mbona diamond kwenye industry ya muziki na kampuni yake ya wcb anafanya vizuri na mashabiki wake wananunua kazi zake

Diamond anatumia kiasi kikubwa cha pesa kutengeneza quality music hawa bongo vilaza wana act kijinga yaani Ray ni director,editor,author,main character yeye yaani kila kitu yeye khaaa

Wakati movie za nje zikiisha mwishoni utakuta list ndefu ya ya presenters ,waigizaji ,waliohusika nk lakini bongolala utakuta list fupi


Movie za nje huchukua muda mpaka inakuwa inaisha lakini huku kwetu miezi 4 movie imeisha

Mwishoni hata wafanyaje bongo movie itabaki vile vile

Waombe tu housegals waongezeke na wanunue kazi zao kwa wingi wawashawishi

Hebu tizama tamthilia za wafilipino,Venezuela na mexico utafananisha na upuuzi wa bongo movie

Movie za nje ni kama dagaa wa kigoma wawekee price tag ya 5000 na bongo movie dagaa wa mwanza 5000 aah kila mtu atakimbilia dagaa wa kigoma
 
Wanajamvi katika siku za hivi karibuni kumekuwa na maandamano na matamko mengi kuhusu kazi za bongo movie na movie za nje (kikorea) lakini watu hawa wanaoandamana walikosa uwakilishwaji mzuri wa hoja zao mpaka kufika mahali watu kutowaelewa.
UKWELI ni kwamba ni kwel kazi za movie za nje zinaua soko la movie za ndani.
Tunafahamu hitaji(demand) la bidhaa katika soko inategemea sana na vitu vifuatavyo'
Bei ya bidhaa yenyewe(price of commodity). Hapa tuwe wawazi kama bidhaa itauzwa kwa bei kubwa sokoni basi hitaji lake litashuka sana (elastic demand). Hii haiwadhuru bongo movie.
Bei ya bidhaa ya mfanano sokoni(price of related goods). Hii ndio inayowaumiza bongo movie.
Bei ya bidhaa ya mfanano sokoni (movie za nje)ikiwa ndogo kuliko bidhaa yako(bongo movie) basi wanunuzi watapendelea sana kununua ile bidhaa nyingine(movie za nje)kuliko bidhaa yako (filamu za bongo)sokoni. Hata bongo muvi wakitengeneza filamu bora za aina gani haziwezi kulifikia soko la muvi za nje.
Tuungane tuiambie serikali kitu kimoja ifanye filamu za nje nazo zilipe kodi kwa serikali na kupitia hatua zote kama wanazopitia bongo muvi (hapa itafanya bei kupanda na kufanana na bei ya filamu ya bongo) au serikali iwaondolee kodi kabisa bongo movie ili bei za filamu sokoni zifanane ili kuwe na ushindani. Baada ya apo tuwaachie bongo movie waboreshe ubora wa kazi zao.

Maoni yako mdau.
Bongo movie ni mbaya kupindukia na mimi unipe bure halafu uniambie utanilipa nikiangalia basi hiyo offer nitaikataa..kwani bongo movie industry inaendeshwa na watu wenye IQ ndogo na wengi wao ni failure kwani hamna creativity na hao actors na ma actress hata kua act ngonjera shuleni hawafai wenzetu hivi vitu wanasomea lakini kwetu hata mimi nikitaka kuwa director wa movie au script writer naweza kuwa..
Kwa hivyo siyo kama wanashindwa kwa sababu ya kodi hata kama bongo movie zisitozwe kodi na ovie za nje kodi iwe maximum basi bado watakuja kulalamika kwa kukosa market.
kwa hivyo njia pekee ya kufanya wawaachie kazi wenye uwezo na akili ya kuzifanya wazifanye, waende shule na au waachane kabisa na kufanya movie na tujue moja na siyo kuendelea kututengenezea movie unaacha kuangalia baada ya dakika 10 na kujilaumu umepoteza pesa zako bure
 
Washirikiane watoe muvi bora sio kila mmoja anataka kuwa steringi na director.
Halafu waachane na siasa wasigawe wateja kwa vyama binafsi nitanunua za wema tu za kibashite sitotaka kuzijua.
 
Hata bei ikipanda kwenye movie za nje....tutanunua za nje

Bongo movie wakae watulize vichwa waje na movie nzuei zenye viwango acting ya maana zitajiuza... la sivyo kwa takataka wanazozitoa hizi watabaki kulalamika tu
 
Tatizo lenu mnatumia sana reference za hollywood ili kupata sababu ya kuwa mko nyuma ya technology. Wakati wa filipino na wakorea wanatumia mazingira ya kawaida kutengeneza filamu ambazo mnaandamana kuzifungia, binafsi yangu filamu za bongo za sasa hazina hata thamani ya kununua kwa tsh 500 ya vocha.
 
Bongo movie waende shule kwanza ili kupata uelewa wa kile wanachofanya sio eti mtu kashindwa shule anaona pa kutokea ni huko. Wanashindwa kuishi kile wanachokiigiza, ukiangalia mpaka kichefuchefu. Kwangu mimi sijawahi hata kufikiria kutoa pesa yangu kununua bongo movie huwa naona kwenye mabasi na wawashukuru hawa wenye mabasi.
 
Shida kwenye bangi movie, mtu akishirikiswa kwenye filam moja na yeye kesho anakuwa director, mtuzi kisha anafungua ka kampuni kake. Van dame na sinema zake zote na umashuhuri wake wote hajawa movie director au kuwa na kampuni ya filamu.

Kama wanataka buashara nzuri.
1. Vikampuni vyote vya binafsi vifungwe. Pawe na kampuni zenye weledi na kazi.
2. Kazi za utunzi na kudirect ziwe kazi za weledi, zifanywe na watu walio somea, tena vyuo vinavyo eleweka sio vya uchochoroni.
3. Pawe na kampuni chache zenye vifaa vya kurekodi vyenye sifa na ubora na wapiga picha walio somea kazi hiyo kwa kiwango cha juu. Kazi ya editing ifanywe na watu mahiri walio somea kwa hali ya juu.

4. Waigizaji wawe na kozi fupi fupi za kiuweledi. Sio mtu umekutwa sokoni kwamaana unatako kubwa unapewa script baada ya dakika mbili unaingia location, nawewe unajiita super star.


Nina mwaka wa kumi sasa sijaangalia bongo movie, nikukuta kwenye basi navaa headphone namsikiliza fally kisha natoa kitabu nakula ufahamu.
 
Back
Top Bottom