Tuwalinde watoto wetu jamani hata baina yao

Tuwalinde watoto wetu jamani hata baina yao

elmagnifico

JF-Expert Member
Joined
Jul 7, 2011
Posts
8,260
Reaction score
9,743
Jana mida ya jioni nilikuwa nimetulia mara nikasikia mama flani jirani na nilipo anamshushia kipigo mtoto wake wa kike mwenye umri wa miaka kama mitano au sita. Alimpiga sana ikabidi niingilie nikamwambia atamuumiza anampiga mtoto vibaya, hakunijibu aliendelea kumshushia kipigo.

Mara akaanza sema hii ni mara ya tatu anamkamata wakiwa na wenzake wanafanya michezo ya kikubwa. Mwenzake akawa anasema tena unakuta vitoto vya kiume zaidi ya viwili, akawa anauliza vitoto alivyokuwa navyo vimeenda wapi.

Nilistaajabu sana maana watoto wote hao hakuna mwenye umri unaozidi miaka saba.

Kuna kitoto kimoja kina miaka kama saba kinasifika kuwalala wenzake, yaani kinaogopwa na watu wakikiona kipo karibu na mtoto wa kike wanakifukuza. Nikawa ninajiuliza hawa watoto wadogo hivi wanajua haya mambo, itakuwaje wakiwa na miaka 16 huko?

Tuwalinde watoto maana kwa sasa naona hata wao kwa wao wanaharibiana.
 
Jamani mbna kawaida sana?
Kwani umri sahihi wa kuanza kulalana ni upi? Maana sisi wengine toka tukiwa na miaka 5 tulianza kupiga mashine japo hatukujua kuwa tunatafuta nini huko ila ilikuwa nibufahari tu kusimulia kwa wenzangu kuwa nimewapiga miti fulani na fulani.
Alafu sio hivyo tu hawa watoto wadogo wa kiume huwa wanafundishwa sana haya mambo na mabinti wakubwa waliobalehe hivyo kudeal na haya mambo ni kuwafunga gps labda.
 
Ila watoto wa siku hizi wamepinda sana,nilimsikia mtoto wa kiume wa miaka 10 au 11 hivi anamwambia mwenzake nitakut**** kama msichana
 
Huyo mtoto anayewala wenzie hana wazazi?

Mtaa mzima mnashindwa ku-deal na wAzaI wake ili wajifunze ku discipline mtoto wao??
Nakumbuka nilipokuwa mdogo
Nikiwa darasa la 1 nilikua navuta karatasi kama sigara,

kuna siku niko chimbo na wana tunavuta,mzee mmoja akatukamata,alituchapa sana akatupeleka home tunalia mno,niliacha hiyo tabia
 
Ila watoto wa siku hizi wamepinda sana,nilimsikia mtoto wa kiume wa miaka 10 au 11 hivi anamwambia mwenzake nitakut**** kama msichana
Afrika inabidi tubadili utamaduni wetu wa malezi. Kuiga mambo mazuri siyo vibaya. Hya mambo ya kuwaachia watoto wacheze na wenzao mtaa mzima bila uangalizi umepitwa na wakati. Mtoto anatakiwa kila anapocheza aiswe mbali na watu wazima na aiswe mabli na nyumbani labda tu kama yuko sehemu yenye watu wanaoaminika na familia ya mtoto. Ukienda Ulaya huu upuuzi wa watoto wadogo kutoka mtaa mmoja kwenda kucheza mtaa mwingine bila uangalizi hakuna.
 
Afrika inabidi tubadili utamaduni wetu wa malezi. Kuiga mambo mazuri siyo vibaya. Hya mambo ya kuwaachia watoto wacheze na wenzao mtaa mzima bila uangalizi umepitwa na wakati. Mtoto anatakiwa kila anapocheza aiswe mbali na watu wazima na aiswe mabli na nyumbani labda tu kama yuko sehemu yenye watu wanaoaminika na familia ya mtoto. Ukienda Ulaya huu upuuzi wa watoto wadogo kutoka mtaa mmoja kwenda kucheza mtaa mwingine bila uangalizi hakuna.
Mkuu vipi kuhusu huko shuleni,umezungumzia mtaani
 
Mkuu vipi kuhusu huko shuleni,umezungumzia mtaani
Shuleni anakuwa kwenye uangalizi wa waalimu. Ila kuna shule na shule. Ukiweza kumpeleka shule nzuri na uangalizi nao ni mzuri. Na mtu kama una nafasi siyo vibaya ukamsindikiza na kumchukuwa kila siku.
 
Chanzo hapo ni wazazi kufanya tendo la faragha mbele ya watoto wakiamini bado ni wadogo, hawaelewi kitu.
Familia za chumba la moja.
 
Aisee, hi hatari sana
Jana mida ya jioni nilikuwa nimetulia mara nikasikia mama flani jirani na nilipo anamshushia kipigo mtoto wake wa kike mwenye umri wa miaka kama mitano au sita. Alimpiga sana ikabidi niingilie nikamwambia atamuumiza anampiga mtoto vibaya, hakunijibu aliendelea kumshushia kipigo.

Mara akaanza sema hii ni mara ya tatu anamkamata wakiwa na wenzake wanafanya michezo ya kikubwa. Mwenzake akawa anasema tena unakuta vitoto vya kiume zaidi ya viwili, akawa anauliza vitoto alivyokuwa navyo vimeenda wapi.

Nilistaajabu sana maana watoto wote hao hakuna mwenye umri unaozidi miaka saba.

Kuna kitoto kimoja kina miaka kama saba kinasifika kuwalala wenzake, yaani kinaogopwa na watu wakikiona kipo karibu na mtoto wa kike wanakifukuza. Nikawa ninajiuliza hawa watoto wadogo hivi wanajua haya mambo, itakuwaje wakiwa na miaka 16 huko?

Tuwalinde watoto maana kwa sasa naona hata wao kwa wao wanaharibiana.
 
Afrika inabidi tubadili utamaduni wetu wa malezi. Kuiga mambo mazuri siyo vibaya. Hya mambo ya kuwaachia watoto wacheze na wenzao mtaa mzima bila uangalizi umepitwa na wakati. Mtoto anatakiwa kila anapocheza aiswe mbali na watu wazima na aiswe mabli na nyumbani labda tu kama yuko sehemu yenye watu wanaoaminika na familia ya mtoto. Ukienda Ulaya huu upuuzi wa watoto wadogo kutoka mtaa mmoja kwenda kucheza mtaa mwingine bila uangalizi hakuna.
Umezungumza vema sana mkuu, swala la malezi kwenye jamii zetu bado sana. Ni jambo la kawaida kuona mtoto wa miaka 7-10 anatoka asubuhi kuzurula akirudi jioni giza lishaingia kama kuku wa kienyeji na mzazi wala haoji mtoto alikuwa wapi, amekula nini, kikubwa uzima tu. Kiufupi bongo watoto huwa wanajilea wenyewe.
 
Back
Top Bottom