Tuwa thamin wazazi wetu

Tuwa thamin wazazi wetu

Ambiele Kiviele

JF-Expert Member
Joined
Dec 29, 2014
Posts
15,271
Reaction score
29,934
Wandugu hebu sikia hii, inaweza kutupa fundisho fulani.

Imetokea jana kwa familia ninayoifahamu vizuri huko Bukoba.
Wamezaliwa watoto 10, angalau 6 miongoni mwao wana kipato kizuri,

wanakaa ktk mikoa ya Dar, Mwanza na Mara.
Wazazi wao wanaishi ktk nyumba ya udongo kwa miaka mingi, jirani zao wote wana nyumba za kisasa na zina umeme.

Baba yao amekuwa akisononeshwa na hiyo hali, hasa kwa kuzingatia kuwa watoto wake wana uwezo kwa muda mrefu.

Mwanzoni mwa mwaka huu watoto wakaungana wakaazimia wawajengee wazazi wao nyumba nzuri, wakamtuma fundi kutoka Mwanza.

Nyumba ilikamilika Oktoba mwaka huu.
Wakakubaliana waifungue rasmi Xmas hii(jana).

Juzi wote waliwasili na familia zao, wakaanza maandalizi ya tafrija ya kuwaingiza wazazi wao kwenye nyumba ya kisasa siku inayofuata.

Ilipofika jana asubuhi mzee akawaita watoto wote kwa mazungumzo, akawaambia, "Watoto wangu nawashukuru sana kwa uamuzi mzuri wa kutujengea nyumba ya kisasa wazazi wenu.

Tunashukuru kwa kuwa mmetambua ktk eneo hili, ni sisi wazazi wenu tu tuliokuwa tumebaki kwenye nyumba ya udongo.Hata hivyo mlichokifanya kinawafurahisha nyie wenyewe, lakini siyo mimi, mama yenu wala wana kijiji wenzetu.

Baadhi yenu hapa mmekuwa na maisha mazuri kwa zaidi ya miaka kumi na tano, wakati mwingine mmekuwa mkitupeleka kwenye nyumba zenu nzuri kwa ndege, huko Dar na Mwanza.

Lakini mkasahau kuwa hata sisi huku tulihitaji kuishi kwenye makazi bora.
Angalieni umri wangu, sina mwaka mmoja zaidi wa kuishi, mwangalie mama yenu, hawezi tena kutembea.

Mimi najua, mmeona tunakaribia kufa, mkatambua kuwa rafiki zenu watakaowasindikiza kuja kutuzika watawashangaa kwa kuona sisi tunaishi kwenye nyumba duni,

Ndio maana mmejenga nyumba hii, wala sio kwamba mnatupenda bali mnakwepa aibu.
Kwa hiyo sisi hatuingii kwenye hiyo nyumba, tutabaki kwenye hii nyumba yetu ya udongo, mliyozaliwa na kukulia hadi mkapata maisha mazuri."

Baada ya maneno hayo, mzee aliwataka wabomoe hiyo nyumba mpya kwakuwa wameijenga kwenye shamba lake bila idhini yake.

Jamaa wamechanganyikiwa. Juhudi za wazee na uongozi wa kijiji kumshawishi mzee abadili msimamo wake zimegonga mwamba.

Wengine wamerudi Bukoba mjini kutafuta guest house za kulala, na wengine wameanza safari ya kurudi Dar na Mwanza, hasa waliokuja na magari yao.

Je ndo wewe sasa ungefanyaje jitambue.

Nyumba imebomolewa.
 
wadhee wengine bana iko wakoloni thana!bora mie nishawajengea wadadhi wng kagholofa kamoja,nimewanunulia kahelcopiter kama ka wale jamaa chaga dev manif...kakutembelea,kila mwedhi nawaagidhia kamilion kakula,wakiugua ata mafua nawapeleka india for tretment,niigen mie
 
wadhee wengine bana iko wakoloni thana!bora mie nishawajengea wadadhi wng kagholofa kamoja,nimewanunulia kahelcopiter kama ka wale jamaa chaga dev manif...kakutembelea,kila mwedhi nawaagidhia kamilion kakula,wakiugua ata mafua nawapeleka india for tretment,niigen mie

Unavojisifia utakuta hata mlo mmoja wazazi wako ni taabu huku wewe uko mjini maboyz wakipasiana kama mpira wa kikapu
 
Ila jamani wahaya wanawasahau sana wazazi wao/vijijini kwao,ingawa sio wote!Wengi wao hurudishwa wakiwa maiti kwenda kuzikwa tu!!Vijiji vyao ukienda utanambia kama nasema uongo!!Makazi duni,miundo mbinu mibovu,uchafu na giza bado!!Ndio maana wachaga wapewe sifa yao...no offence!
 
Sipingani na wale wote wanaodai kuwa watoto wanatakiwa kuwasaidia wazazi wao,, but ninachotaka kushaur n kwamba wazaz waliochinivya miaka 65 wajitegemee tu ili wawape fursa watoto wao kuandaa maisha yao ya badae na watoto wao. Nadhan hii itawaepusha hta watoto wao kuja kuwa ombaomba kwa wajukuu.
 
mi nngenunua hilo shamba! na kukaa wangekaa!!! afu kumbe si bukoba eeh? wee ingekua kule mweeh! wangekwambia ujenge ya ghorofa kabisa..... hahahhaha
 
Safi.. Nimemkubali Mzee, unakuta mtu anaweka heshima bar wakati wazazi wake hawana hata kiatu! Na hiyo ishakuwa laana, itawaandama mpaka vizazi na vizazi!
 
Mzee yupo sawa wamejenga kuogopa aibu siku watakapokuja na rafiki zao kwenye msiba

Ni vizur kuthamini wazazi wetu hata kwa kidogo tukipatacho
 
katika mipango ya awali kujenga mpaka nyumba inaisha hawakumshirikisha mzee wao??aliafiki au hakuafiki??hao wanne wasio na kipato kizuri hawawezi kuishi mzee atakapofariki??....tukisema tatizo ni asili yao...mbona majirani zake wamejenga vizuri?..ama ni wa makabila mengine..tukisema tatizo ni watoto...kama mmoja au wawili sio mbaya sana..lakini wote sita!!!..huoni pengine na malezi yao(ubinafsi) yamechangia(msingi wa wazazi..)??....too tough to judge this... naona kuna tatizo pande zote if this is the real case...
 
baba kama huyu nitamuuliza mbona yeye hakujenga nyumba ya babu??
 
Back
Top Bottom