Tutaendelea kulia

Peterking1

New Member
Jul 27, 2022
3
1
KIZUNGUMKUTI: Waweza ita hivyo ama vinginevyo, lakini katika hili linanipa shida kwa ninavyoendelea kukua, kuishi na kuyaona mambo yanayofanyika katika nchi hii. Najaribu kujiuliza ni lini basi mambo haya yatafika ukomo? Kila tunapoamka yapo na yanaendelea. Najiuliza ni nani basi ataweza kuwa suluhisho la mambo haya? Ama ni lini tutafika tamati katika kuchezea pesa za walipa kodi?

Ni siku ya jana tu, pale nilipopitia kwenye vyombo vya habari vya luninga, redio na mitandao ya kijamii. Ikawa na taarifa endelevu ya matendo ya ubadhirifu wa fedha katika miradi ya serikali. Siku ya jana Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania alipoamuru milango iliyowekwa kwenye moja ya jengo la hospitali ya Wilaya ya Namtumbo iweze kuondolewa na kuwekwa milango yenye hadhi ya kuendana na kodi za wananchi.

Si jambo jipya sana kusikia WM akitoa amri ya namna hiyo pindi anapotembelea miradi ya serikali. Hapa ndipo penye shida ya moyo wangu, hapa ndipo ninapokosa majibu. Kwa nini mpaka WM aje ndio mambo haya yaonekane yana shida?

Hivi hii miradi haina msimamizi kuanzia ngazi ya kata mpk taifa? Hivi hakuna mtendaji? hakuna diwani? hakuna mbunge? hakuna katibu tarafa wa wilaya/mkoa? Hakuna mkurugenzi? Hakuna mkuu wa wilaya? Hakuna mkuu wa mkoa? Vipi kuhusu kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya na mkoa iliyojaa wataalamu, wachunguzi, wapelelezi, waendesha mashataka, wanasheria, polisi, magereza, jeshi n.k.

Hivi hawa wote haoni pindi haya mambo yanapotokea? Au ndio hayawahusu? Au wanakula pamoja? Kama hali ndio hii basi tutaendelea kuumia katika hali hiyo. Kwa kifupi inaonekana ni kama hakuna suluhisho la kutufikisha kwenye ukomo kwenye jambo hili.

Kwa leo tuishie hapa, tunapoendelea kujiuliza, huenda siku moja tutapata jibu la kututoa katika hali hii inayoumiza na kukatisha tamaa.

NI MIMI MTOTO WA MOROGORO
+255 682 527 228
PMO_9685-1024x727.jpg
 
Kassim Majaliwa ni rais ajaye
HAPO si mlango tu hata flemu yenyewe ni poor quality halafu watu wanatetea ati daktari hajui ubora wa hiyo milango?ajabu sana hata mtoto wa chekechea atasema mbona baba umeweka mlango mbaya una matobo.
 
Ukijua kwamba corruption ni ideology inayoambukiza kutoka juu kushuka chini ndani ya mifumo utakuwa umeelewa kiini cha tatizo.
 
HAPO si mlango tu hata flemu yenyewe ni poor quality halafu watu wanatetea ati daktari hajui ubora wa hiyo milango?ajabu sana hata mtoto wa chekechea atasema mbona baba umeweka mlango mbaya una matobo.
Hiyo lawam ya kumpa daktari ipo sawa kbs ila tunawez kujiuliz nchi hii ina wakandaras wangap wa ujenzi ilikuwaj kuwaje mukaenda kumpa kazi ya usimamizi wa ujenz daktari 🤔🤔🤔
 
HAPO si mlango tu hata flemu yenyewe ni poor quality halafu watu wanatetea ati daktari hajui ubora wa hiyo milango?ajabu sana hata mtoto wa chekechea atasema mbona baba umeweka mlango mbaya una matobo.
Nafikiri hapo walilenga kutengeneza mlango unaojifunga wenyewe, kwa nini wasitumie ya aluminium.......angalau serikali ianze kuwa conscious kutumia products za mbao kwa ajili ya kuhifadhi mazingira, tutaishia kuteketeza miti yote kwa utaratibu huu wa hadi milango ya hospitali kutumia mbao.​
 
Nafikiri hapo walilenga kutengeneza mlango unaojifunga wenyewe, kwa nini wasitumie ya aluminium.......angalau serikali ianze kuwa conscious kutumia products za mbao kwa ajili ya kuhifadhi mazingira, tutaishia kuteketeza miti yote kwa utaratibu huu wa hadi milango ya hospitali kutumia mbao.​
hata finishing ya huo mlango ni poor na hauna mvuto kabisa.
 
Ndu
Ni siku ya jana tu, pale nilipopitia kwenye vyombo vya habari vya luninga, redio na mitandao ya kijamii. Ikawa na taarifa endelevu ya matendo ya ubadhirifu wa fedha katika miradi ya serikali. Siku ya jana Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania alipoamuru milango iliyowekwa kwenye moja ya jengo la hospitali ya Wilaya ya Namtumbo iweze kuondolewa na kuwekwa milango yenye hadhi ya kuendana na kodi za wananchi.
Ndugu utakufa kwa presha na hawa wazugaji. Wanaacha kupamba na ufisadi huko wizarani na BOT wanaenda kujionesha kwa wanyonge kwa visa vya milango?😅😅
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom