Tusishangilie Magufuli kuruhusu Wimbo wa Ney wa Mitego, ni chambo

Stabilaiza

JF-Expert Member
Jul 11, 2012
1,843
1,143
Wale wavuvi wa samaki wanafahamu chambo kinavyotumika kumnasa samaki. Si kitu cha kushangilia hata kidogo kwa rais Magufuli kuruhusu wimbo wa Ney wa Mitego ambao BASATA ilikuwa imeufungia.

Naiona ruhusa ya Magufuli kama chambo cha kunasia wananchi. Kuruhusu kwa namna alivyofanya Magufuli kunamjenga na kumwonyesha kama mtu mweye funguo za kufunga na kufungua chochote hapa Tanzania, kitu ambacho si kizuri hata kidogo.

Kwa rais kuwa na funguo ya kufunga na kufungua maana yake ni kwamba taasisi zote za umma na zingine zinakosa maana na wala hazitafanya kazi kwa kujiamini. Matokeo yake ni kwamba taasisi na wananchi wanajengwa na kuzoeshwa kisaikolojia kuwa maamuzi katika nchi hii yanafanywa na mtu mmoja, ambaye ni Magufuli. Tafsiri ya hali hii ni kukosekena kwa demokrasia na utawala wa sheria. Na inafahamika fika kuwa kama hakuna demokrasia wala utawala sheria, maana yake ni utawala wa kiimla (Dictatorship).

Kama Magufuli alikuwa na lengo la kujenga taasisi za umma na si kujijenga yeye binafsi ilitakiwa BASATA na jeshi la polisi ndio waseme kuwa wamechunguza kwa makini na kuona kuwa maudhui yaliyomo katika wimbo wa Ney yana ujumbe ambao una manufaa kwa taifa kuliko hasara. Kwamba wimbo huo kwa mtazamo mpana una mafunzo mazuri.

Tukizoea kuamuliwa kila kitu na rais, mwisho wa siku msemaji katika nchi hii atakuwa mtu mmoja, si taasisi za umma wala nini bali Magufuli. Na hapa ndiyo tatizo lilipo.
 
Ujue watu hawashangilii, ishu ni kwamba watu wengi wana grievances moyoni juu ya maamuzi ya kuowanyima watu Uhuru, kuonea wengine na kupendelea wengingine kwa uwazi kabisa.
Wasanii wakamua kuufikisha ujumbe kwa njia ya nyimbo.

In short Ney alijitoa mhanga kati ya wengi ili kutoa ya moyoni. Alijua wazi kuwa atakamatwa. Nani asiyejua hasira za mkulu? "Watch it" sasa mkulu ka respond passively hii ndo kitu kinawapa watu furaha kuwa huenda mkulu kaanza kubadirika.
 
Modes kwa ruhusa maalum, naomba uzi huu ujitegemee kwa kuwa unamadhui mahsusi.

Wale wavuvi wa samaki wanafahamu chambo kinavyotumika kumnasa samaki. Si kitu cha kushangilia hata kidogo kwa rais Magufuli kuruhusu wimbo wa Ney wa Mitego ambao BASATA ilikuwa imeufungia. Naiona ruhusa ya Magufuli kama chambo cha kunasia wananchi. Kuruhusu kwa namna alivyofanya Magufuli kunamjenga na kumwonyesha kama mtu mweye funguo za kufunga na kufungua chochote hapa Tanzania, kitu ambacho si kizuri hata kidogo. Kwa rais kuwa na funguo ya kufunga na kufungua maana yake ni kwamba taasisi zote za umma na zingine zinakosa maana na wala hazitafaya kazi kwa kujiamini. Matokeo yake ni kwamba taasisi na wananchi wanajengwa na kuzoeshwa kisaikolojia kuwa maamuzi katika nchi hii yanafanywa na mtu mmoja, ambaye ni Magufuli. Tafsiri ya hali hii ni kukosekena kwa demokrasia na utawala wa sheria. Na inafahamika fika kuwa kama hakuna demokrasia wala utawala sheria, maana yake ni utawala wa kiimla (Dictatorship).

Kama Magufuli alikuwa na lengo la kujenga taasisi za umma na si kujijenga yeye binafsi ilitakiwa BASATA na jeshi la polisi ndio waseme kuwa wamechunguza kwa makini na kuona kuwa mauadhui yaliyomo katika wimbo wa Ney yana ujumbe ambao unamanufaa kwa taifa kuliko hasara. Kwamba wimbo huo kwa mtazamo mpana una mafunzo mazuri.

Tukizoea kuamuliwa kila kitu na rais, mwisho wa siku msemaji katika nchi hii atakuwa mtu mmoja, si taasisi za umma wala nini bali Magufuli. Na hapa ndiyo tatizo lilipo.
Mtanyoroka tu..
 
Magufuli hataki kuingiliwa, lakini yeye anataka kuingilia vyombo vya sheria, anataka kuingilia mpaka wasanii kwa kuwaambia waimbe nini.

Absurd.

Ney naye kwa kusema atayafanyia kazi mawazo ya rais kajiweka katika mtego wa kuwa mshairi wa rais, hii ni hatua ya kwanza kuelekea kumuandikia rais nyimbo za kampeni ya uchaguzi.

Ametoa sadaka uhuru wake wa kuandika mashairi anavyotaka kwa sababu za kupata urahisi wa kisiasa.
 
Hivi majukumu na mamlaka yake yanaanzia na kuishia wapi? Ni kwamba hajui mipaka ya majukumu yake; which i don't think. Lakini ikumbukwe kwamba Katiba inampa mamlaka makubwa sana hususan kwa mambo yenye maslahi kwa umma. "Maslahi ya umma" ndio yapi?
 
Negative minded people siku zote hua hawajiamini. Hata ukimpa mtaji bure hatafanya kazi, siku zote mda wote atajiuliza kwanini umempa mtaji wa pesa na usingetumia mwenyewe. Watu wa namna hii huwa hawaendelei mara nyingi akiendelea sana ni kuajiriwa na serikali. Na kwa vile ni negative minded siku zote lazima amtukane amlalamikie mwajiri wake. Ndiyo wengi humu.Magufuli hata akiwapa mikate na siagi bure, bado mtalalamika na kuendelea itakuwa kiduchu
 
Rais ni lazima aingilie na aamue jambo lolote sababu mambo yakiwa mazuri au mabaya huwa halaumiwi waziri au mbunge au spika au jaji mkuu..anayelaumiwa ni rais..jk alitoa Uhuru kwa watu aliowapa mamlaka lakini uharibifu wote ulimrudia yeye..pamoja na kuwa ye muda mwingi hakuwa nchini..hatukusikia spika wala jaji mkuu wakiitwa dhaifu au wazembe..magu kajifunza kupitia jk
 
Teh teh.....nahisi kuna maandalizi ya kitu flani. Ila sikijui.
Labda kupotezea habari ya bashite!!! ...au kusema anapenda kukosolewa, watu wanamsingizia tu kuwa hapendi kukosolewa. (Japo maneno yake yanaonyesha hapendi kukosolewa)
Au ndio ile kugombea "front page"........au kwa sabau Ney aliuliza kuhusu uhuru wa kujieleza na akaonekana alichosema "kujikuta selo" kimetimia!!!!?
 
Hiki Ndicho Rais Magufuli ambacho amekifanya kwa Ney aka mabangi man. Wale walio na ufikiri finyu wanaweza kufurahia lkn nyuma ya pazia kunakitu. Furahini kwa Leo lkn ipo siku mtalia na mtanikumbuka na Haya Mawazo yangu.
 
Modes kwa ruhusa maalum, naomba uzi huu ujitegemee kwa kuwa unamadhui mahsusi.

Wale wavuvi wa samaki wanafahamu chambo kinavyotumika kumnasa samaki. Si kitu cha kushangilia hata kidogo kwa rais Magufuli kuruhusu wimbo wa Ney wa Mitego ambao BASATA ilikuwa imeufungia. Naiona ruhusa ya Magufuli kama chambo cha kunasia wananchi. Kuruhusu kwa namna alivyofanya Magufuli kunamjenga na kumwonyesha kama mtu mweye funguo za kufunga na kufungua chochote hapa Tanzania, kitu ambacho si kizuri hata kidogo. Kwa rais kuwa na funguo ya kufunga na kufungua maana yake ni kwamba taasisi zote za umma na zingine zinakosa maana na wala hazitafanya kazi kwa kujiamini. Matokeo yake ni kwamba taasisi na wananchi wanajengwa na kuzoeshwa kisaikolojia kuwa maamuzi katika nchi hii yanafanywa na mtu mmoja, ambaye ni Magufuli. Tafsiri ya hali hii ni kukosekena kwa demokrasia na utawala wa sheria. Na inafahamika fika kuwa kama hakuna demokrasia wala utawala sheria, maana yake ni utawala wa kiimla (Dictatorship).

Kama Magufuli alikuwa na lengo la kujenga taasisi za umma na si kujijenga yeye binafsi ilitakiwa BASATA na jeshi la polisi ndio waseme kuwa wamechunguza kwa makini na kuona kuwa mauadhui yaliyomo katika wimbo wa Ney yana ujumbe ambao unamanufaa kwa taifa kuliko hasara. Kwamba wimbo huo kwa mtazamo mpana una mafunzo mazuri.

Tukizoea kuamuliwa kila kitu na rais, mwisho wa siku msemaji katika nchi hii atakuwa mtu mmoja, si taasisi za umma wala nini bali Magufuli. Na hapa ndiyo tatizo lilipo.
Pasipo kuwa mnafiki, kwa hili nampongeza sana mh rais. Ameona mbali sana na kujua kwamba hata wasanii waimbeje, haimpunguzii kufanikisha kile anachokiamini
 
Inawezekana wanataka nao wawanunue wasanii wao waanze kukashifu maasimu wao. refer bashite na yule mama wa kumdhalilisha bishop Gwaj. Si mnajua mkulu ni mzee wa shilawadu na ubuyu :':):):p
 
Back
Top Bottom