Habari za asubuhi wana JF,
Ni siku nyingine tena basi tuna kila sababu ya kumshukuru Mwenyezi Mungu endapo amekupa kibali cha kuiona tena siku ya leo.
Nina jambo nahitaji kushirikiana nanyi kwa mawazo katika kukumbushana pia kwani nimeliona mara nyingi kwa watu wa karibu na hata kunikuta mimi binafsi.
Kama utangulizi wa habari hii unavyojieleza juu kabisa kwenye kichwa cha mada hii ni "tusipende kupuuza simu tunazopigiwa" Nimeamua kulileta hili kwenu kwani ninaamini kwa namna moja au nyingine tumeshakutana na mazingira fulani fulani katika utafutaji wa maisha au katika mazingira ya kazi/shughuli zetu za kimaisha za kila siku hutokea wakati mwingine tunapigiwa simu na namba ngeni kupitia simu zetu za mikononi lakini inatokea tunaogopa kupokea simu au kupuuza kabisa nikiwa na maana hata ukikuta missed call huchukui jukumu la kupiga tena ile namba kujua simu ile ilikuwa inahusu nini hasa.
Kwakweli hii tabia sio nzuri sana kwa namna moja au nyingine kwani kuna baadhi ya watu wamejikuta wakipoteza nafasi za kazi au kukosa taarifa fulani za msingi sana ambazo alipaswa kuzipata mapema.
Nishauri pia hata kama imetokea umepoteza mawasiliano yako ya awali ambayo watu wengi na ndugu zako ndio wameyazoea basi unapopata mawasiliano mapya wajulishe ndugu, jamaa, na marafiki maana kuna michongo unaweza kuikosa kwasababu tu ya kutokupatikana kwenye simu.
Sote tunaamini fika ya kuwa kwa dunia ya sasa ilipofikia teknolojia imerahisisha sana baadhi ya shughuli na mfumo mzima wa maisha ya binadamu hivyo kuna baadhi ya vitu kwa asilimia kubwa vinafanyika kimtandao na simu au computer ni mojawapo ya vifaa vya mawasiliano vinavyotumika sana.
Mfano kuanzia unapotafuta kazi tangazo la ajira unalipata kupitia mfumo wa mawasiliano kama simu yako au computer yako mpaka unaomba ajira utatumia vitu hivyo hivyo na inaenda hivyo hivyo mpaka unaitwa kwenye usaili inawezekana ukapigiwa simu au ukatumiwa email sasa usipopatikana kote huko inakuwa ni shida.
Nimetolea mifano hiyo lakini zaidi sana naomba nikazie kwa wale ambao huwa tunaogopa kupokea simu zetu tunapoona tunapigiwa na namba ngeni, hata kama unadaiwa wewe pokea tu hujui ni nani anakutafuta.
Ni haya tu kwa uchache ndugu zangu,
Na ifanyike siku njema kwenu!
🙏
Ni siku nyingine tena basi tuna kila sababu ya kumshukuru Mwenyezi Mungu endapo amekupa kibali cha kuiona tena siku ya leo.
Nina jambo nahitaji kushirikiana nanyi kwa mawazo katika kukumbushana pia kwani nimeliona mara nyingi kwa watu wa karibu na hata kunikuta mimi binafsi.
Kama utangulizi wa habari hii unavyojieleza juu kabisa kwenye kichwa cha mada hii ni "tusipende kupuuza simu tunazopigiwa" Nimeamua kulileta hili kwenu kwani ninaamini kwa namna moja au nyingine tumeshakutana na mazingira fulani fulani katika utafutaji wa maisha au katika mazingira ya kazi/shughuli zetu za kimaisha za kila siku hutokea wakati mwingine tunapigiwa simu na namba ngeni kupitia simu zetu za mikononi lakini inatokea tunaogopa kupokea simu au kupuuza kabisa nikiwa na maana hata ukikuta missed call huchukui jukumu la kupiga tena ile namba kujua simu ile ilikuwa inahusu nini hasa.
Kwakweli hii tabia sio nzuri sana kwa namna moja au nyingine kwani kuna baadhi ya watu wamejikuta wakipoteza nafasi za kazi au kukosa taarifa fulani za msingi sana ambazo alipaswa kuzipata mapema.
Nishauri pia hata kama imetokea umepoteza mawasiliano yako ya awali ambayo watu wengi na ndugu zako ndio wameyazoea basi unapopata mawasiliano mapya wajulishe ndugu, jamaa, na marafiki maana kuna michongo unaweza kuikosa kwasababu tu ya kutokupatikana kwenye simu.
Sote tunaamini fika ya kuwa kwa dunia ya sasa ilipofikia teknolojia imerahisisha sana baadhi ya shughuli na mfumo mzima wa maisha ya binadamu hivyo kuna baadhi ya vitu kwa asilimia kubwa vinafanyika kimtandao na simu au computer ni mojawapo ya vifaa vya mawasiliano vinavyotumika sana.
Mfano kuanzia unapotafuta kazi tangazo la ajira unalipata kupitia mfumo wa mawasiliano kama simu yako au computer yako mpaka unaomba ajira utatumia vitu hivyo hivyo na inaenda hivyo hivyo mpaka unaitwa kwenye usaili inawezekana ukapigiwa simu au ukatumiwa email sasa usipopatikana kote huko inakuwa ni shida.
Nimetolea mifano hiyo lakini zaidi sana naomba nikazie kwa wale ambao huwa tunaogopa kupokea simu zetu tunapoona tunapigiwa na namba ngeni, hata kama unadaiwa wewe pokea tu hujui ni nani anakutafuta.
Ni haya tu kwa uchache ndugu zangu,
Na ifanyike siku njema kwenu!
🙏