kt the irreplaceable
JF-Expert Member
- Oct 12, 2017
- 2,363
- 4,851
Wakuu kwema?
Ukitizima kwa jicho la kiufundi hii timu yetu ya Simba ni timu dhaifu, kweli tutasema tumefuzu hatua ya makundi Klabu Bingwa Africa lakini tumekutana na timu gani? Huwezi kujisifu kwa kupigana na mlevi.
Tazama mechi ya Azam, Singida na Yanga, Simba yetu ikikutana na timu iliyo 'compact' hatutoboi, ukweli usemwe. Tuna wachezaji ambao ni wa kawaida sana, mtu kama Kibu ataifikisha wapi timu?
Aya twende kwenye uongozi, huku ndiyo ujanja ujanja, walikuwa wanajificha kwenye kivuli cha Yanga kufungwa kimataifa. Mpaka sasa kocha mkuu Mgunda hana mkataba, hawajui kama wamuongezee au watafute kocha mpya.
Mpaka sasa anayejiita mwekezaji hajaweka ile pesa shilingi bilioni 20 kama thamani ya hisa ya asilimia 49. Timu inasajili wachezaji wa laki 5 kama akina Kibu itafika wapi? Angalia Yanga wamecheza michezo pungufu ila ndiyo wanaongoza ligi. Halafu kuna mbumbumbu wanasema tutachukua kombe, labda kombe la kahawa.
Mo Dewj tuachie timu yetu, ondoka na huyo dada yako Barbra, wanachama tunataka 20b, hatuwezi kuendelea kuwa mambumbumbu kiasi hiki.
Ukitizima kwa jicho la kiufundi hii timu yetu ya Simba ni timu dhaifu, kweli tutasema tumefuzu hatua ya makundi Klabu Bingwa Africa lakini tumekutana na timu gani? Huwezi kujisifu kwa kupigana na mlevi.
Tazama mechi ya Azam, Singida na Yanga, Simba yetu ikikutana na timu iliyo 'compact' hatutoboi, ukweli usemwe. Tuna wachezaji ambao ni wa kawaida sana, mtu kama Kibu ataifikisha wapi timu?
Aya twende kwenye uongozi, huku ndiyo ujanja ujanja, walikuwa wanajificha kwenye kivuli cha Yanga kufungwa kimataifa. Mpaka sasa kocha mkuu Mgunda hana mkataba, hawajui kama wamuongezee au watafute kocha mpya.
Mpaka sasa anayejiita mwekezaji hajaweka ile pesa shilingi bilioni 20 kama thamani ya hisa ya asilimia 49. Timu inasajili wachezaji wa laki 5 kama akina Kibu itafika wapi? Angalia Yanga wamecheza michezo pungufu ila ndiyo wanaongoza ligi. Halafu kuna mbumbumbu wanasema tutachukua kombe, labda kombe la kahawa.
Mo Dewj tuachie timu yetu, ondoka na huyo dada yako Barbra, wanachama tunataka 20b, hatuwezi kuendelea kuwa mambumbumbu kiasi hiki.