Tusaidiane kumshauri; Ameamua kuokoka mke anadai talaka

sepema

JF-Expert Member
Jun 13, 2019
591
1,000
Tuungane tena kwenye kuliangalia hili.

Jamaa yangu ni chapombe,bangi na mwasherati aliyekubuhu.Mara kadhaa amekuwa analewa nakulala nje(harudi nyumbani).Tarehe zamshahara haonekani nyumban hadi juhudi zakumtafuta zifanyike.

Mwezi ulopita alinieleza jambo ambalo binafsi nililichukulia Kama sehemu ya mauzauza ya bangi mbichi anazovuta. Alikuja kwangu nakunieleza kuwa marehemu mama yake kamtokea kwenye ndoto na kumsihi aache hizo tabia zaulevi vinginevyo atakufa hivi karibuni.

Baada yakumsikiliza kwa muda nikagundua kuwa jamaa yupo serious. Jamaa anadai kwenye kuota huko aliambiwa na mamayake aokoke kwa maana ya kufuata misingi ya Mungu kupitia dhehebu flani la kikristo.

Jamaa anaishi na mkewe mwaka wa9 saivi na Wana watoto wao wawili.
Mwanzo wa mwezi huu jamaa amekuja kwangu anadai amemshirikisha mkewe juu ya nia yake yakuokoka nakumrudia Mungu Ila mke amekuwa mbogo hataki kusikia jambo Kama hilo.Jamaa na mkewe ni wakatoliki japo tangu alipofunga ndoa hakurudi tena kanisani.

Alivyoamua kuacha hayo Mambo aliamua abadili dhehebu kitu ambacho mkewe hakubaliani nachi na kudai bora jamaa abaki Kwenye tabia zake za awali kuliko kuhama dhehebu.
Mke amesema Kama jamaa atabadili dhehebu basi ndo mwisho wa wao kuishi pamoja.

Jamaa anadai ana wiki3 hajui pombe Wala sigara(bangi)Ila Cha kushangaza haoni furaha ya mkewe zaidi ya visirani vya hapa napale.

Wakuu, mwanamke aliyeteseka miaka mingi kwa tabia mbaya zamumewe anaweza kweli kutaman mumewe aendelee na Mambo maovu kuliko kubadili dhehebu?(sio dini)

Kwangu naona mwanamke alitakiwa kufurahia maamuzi ya mumewe kuacha tabia mbaya kuliko kutizama anaelekea dhehebu gani

Kwa mtazamo wangu wa haraka nahisi huyu mwanamke Kuna namna alikuwa anafaidika kutokana na tabia za ulevi za jamaa.
Je,mnadhani nini kipo nyuma ya msimamo wa huyu mwanamke dhidi ya kuokoka kwa mumewe.

Wasalaam!
 
Sikumbuki vizuri mstari lakini kuna mahali kwenye biblia Yesu anasema "Sikuja kuleta amani bali uadui kati ya binti na mkwewe, kijana na babake,...ADUI WA MTU NI YULE WA NYUMBANI MWAKE...kumfuata Yesu si lelemama utakataliwa na watu wako wa karibu,dharau.kutukanwa,kebehi lakini songa mbele
 
Kuna mawili.

Mke kashakuwa addicted na tabia za mumewe sasa anaona anaishi na mtu mpya.

Au kuna namna alikuwa anafaidika kwa mumewe kuwa mlevi.

Hata hivyo mambo yao tuwaachie wenyewe.

Nakazia
 
Tuungane tena kwenye kuliangalia hili.

Jamaa yangu ni chapombe,bangi na mwasherati aliyekubuhu.Mara kadhaa amekuwa analewa nakulala nje(harudi nyumbani).Tarehe zamshahara haonekani nyumban hadi juhudi zakumtafuta zifanyike.

Malaika ni watu na mashetani ni watu

Mwanamke ana roho ya dada zake Lucifer huyo, yawezekana jamaa alikua anafikia mwisho wa uhai wake kupitia ulevi na huo ndio ulikua mipango wa mkewe

MWANZO 6:1-7​

Ikawa wanadamu walipoanza kuzidi usoni pa nchi na wana wa kike walizaliwa kwao, wana wa Mungu waliwaona hao binti za wanadamu ya kuwa ni wazuri; wakajitwalia wake wo wote waliowachagua.

Bwana akasema, Roho yangu haitashindana na mwanadamu milele, kwa kuwa yeye naye ni nyama; basi siku zake zitakuwa miaka mia na ishirini.

Nao Wanefili walikuwako duniani siku zile;tena ,baada ya hayo ,wana wa Mungu walipoingia kwa binti za binadamu,wakazaa nao wana;hao ndiyo waliokuwa watu hodari zamani ,watu wenye sifa.

Bwana akaona ya kuwa maovu ya mwanadamu ni makubwa duniani na kwamba kila kusudi analowaza moyoni mwake ni baya tu sikuzote.

Bwana akaghairi kwa kuwa amemfanya mwanadamu duniani, akahuzunika moyo.

Bwana akasema, Nitamfutilia mbali mwanadamu niliyemwumba usoni pa nchi; mwanadamu na mnyama, na kitambaacho na ndege wa angani; kwa maana naghairi ya kwamba nimewafanya.
 
Sikumbuki vizuri mstari lakini kuna mahali kwenye biblia Yesu anasema "Sikuja kuleta amani bali uadui kati ya binti na mkwewe, kijana na babake,...ADUI WA MTU NI YULE WA NYUMBANI MWAKE...kumfuata Yesu si lelemama utakataliwa na watu wako wa karibu,dharau.kutukanwa,kebehi lakini songa mbele
Ni mathayo 10:34-39 ndio inazungumza kuwa Yesu hakuja kuleta amani bali upanga. Kama ulivyosema ni kuwa suala la wokovu linaweza kukufarakanisha na ndugu, jamaa, wazazi nk na Yesu alijua na kuonya mapema kuwa asiyeweza kujikana na kuuchukua msalaba wake na kuachana na jamaa yake huyo hamfai.

Pia jambo hili limekuwa addressed na mtume Paulo katika kitabu cha wakorinto. Baada ya Paulo kupita huko akahubiri na watu wakaamini na kumpokea Yesu, baadhi ya walio amini walikuwa ni wanandoa. Basi kati yao palitokea mwingine mke akaamini na mume asiamini na wengine mume akaamini bali mke hajaamini bado.

Basi taarifa ikamfikia Paulo huko alikokuwa na pamoja na mambo mengine aliandika waraka wa kwanza kwa wakorinto kutoa maelekezo juu ya yaliyojiri na kwa upande wa ndoa biblia inasema hivi;

1 Corinthians 7:12-14
12 Lakini watu wengine nawaambia mimi, wala si Bwana, ya kwamba iwapo ndugu mmoja ana mke asiyeamini, na mke huyo anakubali kukaa naye asimwache.
13 Na mwanamke, ambaye ana mume asiyeamini, na mume huyo anakubali kukaa naye, asimwache mumewe.
14 Kwa maana yule mume asiyeamini hutakaswa katika mkewe; na yule mke asiyeamini hutakaswa katika mumewe; kama isingekuwa hivyo, watoto wenu wangekuwa si safi; bali sasa ni watakatifu.

Kwa maana hiyo kama mmoja ameamini na mwenza wake hajaamini na hataki kuishi naye kwa sababu amepokea wokovu anaweza kuachana naye na hatakuwa na hatia juu ya hilo ukisoma mstari wa 15 unasema hvo.

15 Lakini yule asiyeamini akiondoka, na aondoke. Hapo huyo ndugu mume au ndugu mke hafungiki. Lakini Mungu ametuita katika amani.

Kwa hiyo ushauri ni kuwa, jamaa aendelee na wokovu kama mke akiamua kuondoka sababu ya wokovu wake, amuache aende kwa amani.
 
Mwanamke yupo sahihi sana.

kwanza kitendo cha mwanaume kubadili dini ni udhaifu mkubwa sana mbele ya Mungu na jamii,

Kama mwamaume anakosa msimamo wa kidini anashindwa kuiamini dini yake ambayo mpaka amefungia ndoa, anakuja ukubwani kashapigwa na maisha anataka kuokoka huu ni udhaifu mkubwa sana, hana msimamo na maisha yatamuendesha sana akiwa kama baba ambaye hana msimamo anatetereka kiimani

Akiona ulokole hakuna issue tena ataenda kwa waganga, maana hana misimamo.

Swala la msingi ni kwamba kulikuwa na haja gani ya yeye kubadili dini, hiyo dini yake ya kikatoliki inahusikaje na bangi, pombe na uzinzi? Au ndo alkuwa tayari ashakula msuba anamskiliza rose mhando akaona hapa dili ni kuokoka?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni mathayo 10:34-39 ndio inazungumza kuwa Yesu hakuja kuleta amani bali upanga. Kama ulivyosema ni kuwa suala la wokovu linaweza kukufarakanisha na ndugu, jamaa, wazazi nk na Yesu alijua na kuonya mapema kuwa asiyeweza kujikana na kuuchukua msalaba wake na kuachana na jamaa yake huyo hamfai.
Mm nashindwaga kuwaelewa nyie walokole, hivi nini maana ya ulokole na kwann katika kutoa majibu ya maswali madogo ni mpaka mtafute vifungu vya biblia, hamuwezi kuumiza ubongo wenu na kutoa majibu yaliyonyooka?
 
Malaika ni watu na mashetani ni watu

Mwanamke ana roho ya dada zake Lucifer huyo, yawezekana jamaa alikua anafikia mwisho wa uhai wake kupitia ulevi na huo ndio ulikua mipango wa mkewe
mama D, amani ya bwana iwe pamoja nawe!!

Don't cross the line please, usimregard huyo wife wa jamaa km binti wa lucifer. Nadhani wengi tulianzia huko haikuwa rahisi kumpokea Yesu.

Inawezekana baadaye kupitia mmewe huyu mke akampokea Yesu pia, nimetoa maelekezo ya kibiblia hapo juu kuhusu ni nini kinafanyika katika mazingira hayo.

However, nikupe pongezi kwa kupenda kushiriki na kutoa ufafanuzi katika mijadala ihusuyo mambo ya imani, bless you!!
 
Mm nashindwaga kuwaelewa nyie walokole, hivi nini maana ya ulokole na kwann katika kutoa majibu ya maswali madogo ni mpaka mtafute vifungu vya biblia, hamuwezi kuumiza ubongo wenu na kutoa majibu yaliyonyooka?

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu, hata unacho kijibu wewe pia kinapata msingi kutoka kwenye maarifa ya aina flani ambayo wewe unayaamini na kuona yanakufaa kama muongozo.

Kama wewe ulivyoona inafaa, nasi pia kwa kutumia maarifa yetu ya kiimani toka kwenye biblia tumetoa mchango wetu, muhusika anaomba ushauri, kwa nini unahisi ushauri wako toka kwenye vyanzo vyako vya maarifa ni sahihi kuliko wengine?

Nadhani tumuachie muhusika ataona mwenyewe mchele ni upi na pumba ni zipi, mwisho wa yote atachukua kimfaacho, ahsante.
 
Sikumbuki vizuri mstari lakini kuna mahali kwenye biblia Yesu anasema "Sikuja kuleta amani bali uadui kati ya binti na mkwewe, kijana na babake,...ADUI WA MTU NI YULE WA NYUMBANI MWAKE...kumfuata Yesu si lelemama utakataliwa na watu wako wa karibu,dharau.kutukanwa,kebehi lakini songa mbele
Sawa mkuu lakini nashauri huu mstari uungalie tena vizuri.
 
Malaika ni watu na mashetani ni watu

Mwanamke ana roho ya dada zake Lucifer huyo, yawezekana jamaa alikua anafikia mwisho wa uhai wake kupitia ulevi na huo ndio ulikua mipango wa mkewe

MWANZO 6:1-7​

Ikawa wanadamu walipoanza kuzidi usoni pa nchi na wana wa kike walizaliwa kwao, wana wa Mungu waliwaona hao binti za wanadamu ya kuwa ni wazuri; wakajitwalia wake wo wote waliowachagua.

Bwana akasema, Roho yangu haitashindana na mwanadamu milele, kwa kuwa yeye naye ni nyama; basi siku zake zitakuwa miaka mia na ishirini.

Nao Wanefili walikuwako duniani siku zile;tena ,baada ya hayo ,wana wa Mungu walipoingia kwa binti za binadamu,wakazaa nao wana;hao ndiyo waliokuwa watu hodari zamani ,watu wenye sifa.

Bwana akaona ya kuwa maovu ya mwanadamu ni makubwa duniani na kwamba kila kusudi analowaza moyoni mwake ni baya tu sikuzote.

Bwana akaghairi kwa kuwa amemfanya mwanadamu duniani, akahuzunika moyo.

Bwana akasema, Nitamfutilia mbali mwanadamu niliyemwumba usoni pa nchi; mwanadamu na mnyama, na kitambaacho na ndege wa angani; kwa maana naghairi ya kwamba nimewafanya.
Daaah! Imebidi nicheke kwa nguvu. Yaani watu humu mnaongea kwa rejea hadi raha.
Kila lakheri mamaD
 
Mwanamke yupo sahihi sana.

kwanza kitendo cha mwanaume kubadili dini ni udhaifu mkubwa sana mbele ya Mungu na jamii,

Kama mwamaume anakosa msimamo wa kidini anashindwa kuiamini dini yake ambayo mpaka amefungia ndoa, anakuja ukubwani kashapigwa na maisha anataka kuokoka huu ni udhaifu mkubwa sana, hana msimamo na maisha yatamuendesha sana akiwa kama baba ambaye hana msimamo anatetereka kiimani

Akiona ulokole hakuna issue tena ataenda kwa waganga, maana hana misimamo.

Swala la msingi ni kwamba kulikuwa na haja gani ya yeye kubadili dini, hiyo dini yake ya kikatoliki inahusikaje na bangi, pombe na uzinzi? Au ndo alkuwa tayari ashakula msuba anamskiliza rose mhando akaona hapa dili ni kuokoka?

Sent using Jamii Forums mobile app
Lakini bado kubadili dhehebu nahisi ilikuwa muhimu kuliko kuendelea na zile tabia za awali
 
Back
Top Bottom