Tusaidiane kulilinda taifa

Tusaidiane kulilinda taifa

Kiwalani finest

Senior Member
Joined
Jul 6, 2024
Posts
116
Reaction score
85
Tusaidieni kulilinda taifa ninyi vyombo vya dola kwa kujizibuwa na kuwachukulia hatua baadhi ya viongozi waliomkufuru mungu na sisi raia kwa kuapa na kisha kuishi maisha ya kikafir wakikufuru mchana kweupe.

Nikiwa nimevagaliwa na jini tambuzi huko usingizini, nikawa naropokwa tukisoma kitabu cha sunnah za mtume kiitwacho muntakhab ahadith uk 775. Kinatufunza:

Ali (r.a) amesimulia kuwa rasulullah (s.a.w) amesema:

"hakuna utiifu kwa kumuasi allah. Utiifu ni katika mema tu."

Mwisho wa kunukuu.

Shekhe walidi alhad omar kawambwa, shekhe wa mkoa wa dar es salaamu, nakumbuka tarehe 18/03/2025 alisema:

"huyu mtu aliyesema maneno hayo hadanganyi. Mtume (s.a.w) hajaongopa hata siku moja. Na kabla hajakuwa mtume alikuwa anaitwa aswaadikhum masulukhu. Neno lake halijaanguka."

Mwisho wa kunukuu.

Baadhi ya viongozi wameapa kuhifadhi, kulinda na kutetea katiba na sheria za nchi. Ila baada ya kuapa wako kinyume na viapo, wakilazimisha ubatili kuwa haki, na haki zilizo ndani ya katiba, kanuni, miongozo na taratibu za kisheria wanazifanya batili kwa msaada wa michawa ilayo ubwabwa bila kutosheka.

Katika viapo walimuahidi mwenyezi mungu kutenda haki kwa kufuata maandiko ya kimfumo na ya kidini. Na ndiyo maana halisi ya kushika vitabu vya dini. Ndani ya vitabu vya kimfumo, wametakiwa kuwa wanyenyekevu, kujiepusha na ubaguzi na upendeleo, kuwa watu wa haki kwa wenye nacho na wasio nacho.

Yote haya hawayafanyi. Akijitokeza anayewakumbusha wamfanya adui, na michawa ikisherehesha ubatili na kuiponda ponda haki, utaona viongozi hao waliomkufuri mungu wakiipongeza michawa na kuitia moyo izidishe uchawi ili jamii izidi kupotea.

Vyombo vya dola, ninyi ni watanzania namba moja wa kuwafanya watu wengine kuiga uadilifu na uaminifu kwenu. Isaidieni nchi kupitia:

  • Ibara 26(1)(2)
  • Ibara 09(a)(b)
  • Ilani ya CCM 2020 uk 01 ibara 04
  • Kusimamia kila mtanzania kuitii ibara hiyo kwa mazingatio ya ibara ya 10 na 11 ya ilani
  • Katiba ya jamhuri ya muungano wa tanzania 1977 toleo 2005:
    • Ibara 12(1)(2)
    • Ibara 13(1)(4)(5)
    • Ibara 29(1)(2)
    • Ibara 152(1)(2)(3)
    • Uk 14 ibara 01 na 02(1)
    • Uk 13 paragraph ya kwanza ya katiba
Nayasema haya nikiwa naonyeshwa baadhi ya viongozi kutokuwa na utu wala huruma ya kushughulikia malalamiko ya watu wanyonge. Baadhi ya viongozi hao wamekuwa manunda kwa sababu ya kumiliki uraia pacha, kunawafanya kudharau hata viapo walivyomuahidi mwenyezi mungu.

Wako tayari hata kusaini mikataba ya hovyo kuwanufaisha wasio watanzania huku watanzania wakipiga miayo. Viongozi hao hawana utii kwa kauli za viongozi wetu wakuu wa kitaifa. Wanauza maeneo nyeti yenye utajiri ili siku fukara akizinduka ajikute ni manamba kwenye nchi iliyojaaliwa maziwa na asali.

Viongozi hao wanaamini uzalendo ni kwa ajiri ya mtu asiyekuwa nacho. Huu ndiyo uzao wa nyoka, uzao wa shetani wenye kjjitamkisha neno mwenyezi mungu huku wakimaanisha ushetani kimoyo moyo. Ndiyo maana wakimsikia mwenzao hasomi mapato na matumizi wanamlinda na kumuandaa aendelee kuwa kiongozi ili wazidi kuifaidi rushwa waitamkayo kama vile hawaipendi, huku nyuma ya pazia wakiibusu na kuisujudia rushwa.

Tusaidieni ninyi vyombo vya dola ili mulinde maslahi ya vizazi vya sasa na vile vijavyo. Tusome:

  • Katiba ya jamhuri ya muungano wa tanzania 1977 toleo 2005 uk 121 ibara 147
  • Ilani ya ccm 2020 uk 09 ibara 14(a)
  • Uk 156-157 ibara 105(c)(k)
Nikashtuka ndotoni nikitokwa jasho kama mgonjwa wa buradi pureshaa, huku nikijisemea: twendeni tu.

Watu kila kukicha wanazidi kukuza uelewa ila wako kimya...

Kidumu chama cha mapinduzi

Mathias mugerwa kahinga
 
Back
Top Bottom