Tupunguze kuwashirikisha marafiki zetu madhaifu ya wenza wetu

miss chagga

JF-Expert Member
Jun 7, 2013
57,821
48,976
Habari za asubuhi wapendwa ..
Kuna kesi nimeletewa ni wiki sasa natafakari na kuamua kuwafundisha baadhi yetu wenye tabia kama hizo..

Kesi yenyewe kwa ufupi tu ni kuna wana ndoa wapo kwenye kutoelewana kwa muda sasa kisa mume anatabia ya kuchepuka , ila mke ana rafiki yake wa kike ambaye yeye hajaolewa na ndiyo rafiki yake mkubwa kiasi kwamba hawa wanandoa kama vile wanamtumia katika kusuluhisha matatizo yao... lakini aliyeanzisha ni mwanamke kumtuma rafiki yake kwa mume wake kitu ambacho si kibaya....

Sasa kumbe mume kashaacha madanga yote au kaamua kubeba yote pamoja shoga yake mkubwa, Sasa mke analia haamini kinachoendelea na wala hataki kusikia mume wala rafiki. Nipo naye mtu kamleta kwangu nimsaidie ila naona ana kiu ya pombe anataka kulewa sasa tumekunywa weweee jana akaniambia kiu imeisha sasa tujenge au tubomoe. Nimeshayajenga kwake sasa nikaona nije niwajenge na baadhi yenu humu....

Kuna makosa tunayoyafanya wanawake/wanaume katika kutafuta suluuu. Kutumia rafiki kama njia ya mawasiliano yako.... Unajua unapokuja kwangu kunieleza mambo ya mwenza wako na ukanipa nafasi ya mimi kuonana nae kukujadili automatic sababu umesema mabaya yake kwangu na yeye atasema ubaya wako zaidi na anaweza kutengeneza mazingira ya kuonewa huruma na kitakachotokea ni rehema za Mungu tu.......

Huwa wanasema wewe unamwona wa nini wenzio wanasema watakipata lini? Hujui yupi anayemtamani mkeo au mumeo okey akimaliza kusuluhisha unadhani mawasiliano yanaisha ooh no yanaendelea na watakuwa wameshakukatia A.K.A........sababu adui ukishamjua ni nusu ya ushindi...

Tupunguze kutoa madhaifu ya wake au waume zetu kwa marafiki.. Jamani binadamu tunataka kusikia ubaya zaidi kuliko mazuri ndiyo maana baya moja hufuta mazuri elfu..

Unamwambia mshikaji wako ooh mke wangu ooh mume wangu hivi na vile jamani humo humo kwenye weakness ndiyo tunapochezea .. na ndiyo maana ndoa nyingi wanasalitiwa na watu wa karibu hasa wanaojiita washauri wetu kuweni makini..

NB: Ni bora ukaja huku jf au sehemu yeyote ile ukaomba ushauri usiyemjua akakushauri ukasepa kuliko hao mnawaita mashoga .. pia si marafiki wote wabaya
okey weekeend njema .. Nipo tayari kujibu maswali ...
 
Miss chaga ye anaangaliaga pesa tu hahaaaa

Ukimsimulia madhaifu ya mume wako mradi akiwa na hela utakiona cha moto.....anabeba jumla teh teh

Ila ushauri murua dada. Wafundishe vijana ila hii mara nyingi nimeisikia kwa wanaume kutumia marafiki zaidi huwa tukiamini katika bro code.

Ya mkewangu amtume rafiki yake wa kike kusuluhisha ni kutafutana ubaya tu.....
Easy Friday...
 
huyo shosti yako kakwambia mumewe ana tabia ya kuchepuka hata na shemeji zake


swali: je na wewe utaenda kuchepuka na huyo shemeji yako ?
 
huyo shosti yako kakwambia mumewe ana tabia ya kuchepuka hata na shemeji zake


swali: je na wewe utaenda kuchepuka na huyo shemeji yako ?
huyu siyo rafiki yangu aliyemleta kwangu ndiyo rafiki yangu.. me sichepuki na wanaume wanawaliza wake zao
 
Miss chaga ye anaangaliaga pesa tu hahaaaa

Ukimsimulia madhaifu ya mume wako mradi akiwa na hela utakiona cha moto.....anabeba jumla teh teh

Ila ushauri murua dada. Wafundishe vijana ila hii mara nyingi nimeisikia kwa wanaume kutumia marafiki zaidi huwa tukiamini katika bro code.

Ya mkewangu amtume rafiki yake wa kike kusuluhisha ni kutafutana ubaya tu.....
Easy Friday...
kweli kabisa sema ndiyo hivyo tena .. akiwa na pesa mmmh nilikataa kukaa na namba za masheji zangu na wakinipa nawablock in advance
 
Dah unanizungumzia mm kabisa teh teh.... nikisuluhishaga misunderstanding za jamaa zangu na wapenzi wao huwa inatokea wapenzi wao wananing'ang'ania, sijui kwann
inatokea automatic sababu jamaa zako wanapokueleza matatizo yako akaja kueleza mpenzi wake basi unajua gape lipo wapi katika kusuluhisha huko demu anakuona bonge la mjanja
 
sasa mtu atakushauri nini cha maana .mume wako akichepuka unaomba ushauri? hapo utashauriwa nini? unashindwa kujua ufanye nini mume/mke akichepuka ? kweli mtu mzima kabisa unakosa la kufanya ?
 
habari za asubuhi wapendwa ..

kuna kesi nimeletewa ni wiki sasa natafakari na kuamua kuwafundisha baadhi yetu wenye tabia kama hizo.. kesi yenyewe kwa ufupi tu ni kuna wana ndoa wapo kwenye kutoelewana kwa muda sasa kisa mume anatabia ya kuchepuka , ila mke anarafiki yake wa kike ambaye yeye hajaolewa na ndiyo rafiki yake mkubwa kiasi kwamba hawa wanandoa kama vile wanamtumia katika kusuluhisha matatizo yao... lakini aliyeanzisha ni mwanamke kumtuma rafiki yake kwa mume wake kitu ambacho si kibaya....

sasa kumbe mume kashaacha madanga yote au kaamua kubeba yote pamoja shoga yake mkubwa, sasa mke analia aamini kinachoendelea na wala hataki kusikia mume wala rafiki nipo naye mtu kamleta kwangu nimsaidie ila naona anakiu ya pombe ana anataka kulewa sasa tumekunywa weweee jana akaniambia kiu imeisha sasa tujenge au tubomoe. nimeshayajenga kwake sasa nikaona nije niwajenge na baadhi yenu humu....

kuna makosa tunayoyafanya wanawake/wanaume katika kutafuta suluuu.
kutumia rafiki kama njia ya mawasiliano yako.... unajua unapokuja kwangu kunieleza mambo ya mwenza wako na ukanipa nafasi ya mimi kuonana nae kukujadili automatic sababu umesema mabaya yake kwake na yeye atasema ubaya wako zaidi na anweza tengeneza mazingira ya kuonewa huruma na kitakachotokea ni rehema za mungu tu....... huwa wanasema we unamwona wa nini wenzio wansema watakipata lini? hujui yupi anayemtamani mekeo au mumeo okey akimaliza kusuluhisha unadhani mawasiliano yanisha ooh no yanaendelea na watakuwa wamesha kukatia A.K.A........sababu adui ukishamjua ni nusu ya ushindi...

tupunguze kutoa madhaifu ya wake au waume zetu kwa marafiki.. jamani binadamu tunataka kusikia ubaya zaidi kuliko mazuri ndiyo maana baya moja hufuta uzuri elfu.. unamwambia mshikaji wako ooh mke wangu ooh mume wangu hivi na vile jamani humo humo kwenye weakness ndiyo tunapochezea .. na ndiyo maana ndoa nyingi wanacheat na watu wa karibu hasa wanao jiita washauri wetu kuweni makini..
NB: ni bora ukaja huku jf au sehemu yeyote ile ukaomba ushauri usiyemjua akakushauri ukasepa kuliko hao mnawaita mashoga .. pia si marafiki wote wabaya
okey weekeend njema .. nipo tayari kujibu maswali ...okey


Aisee mimi nimeshakutwa na hili Demu wangu alinimwaga kwa sababu rafiki yake hakunimind, hilo tu likatosha kunimwaga, Mademu noma sana, lkn ninejifunza ukiwa Demu ujue uko na Mashoga zake pia!
 
sasa mtu atakushauri nini cha maana .mume wako akichepuka unaomba ushauri? hapo utashauriwa nini? unashindwa kujua ufanye nini mume/mke akichepuka ? kweli mtu mzima kabisa unakosa la kufanya ?
kuna watu wakikutana na tatizo wanapanic na kushindwa kufikiri vyema ambao wengi ni wanawake ... na tunatabia ya kuongea hapo ndiyo tatizo lilipo
 
Back
Top Bottom