Tupige vita kuwanyanyapaa waliopata div zero mashuleni

Tupige vita kuwanyanyapaa waliopata div zero mashuleni

Ni kwa muda sasa umekuwepo unyanyapaaji mkubwa kwa watu wanaoshindwa masomo ya sekondari maarufu kama ''div zero''

wanaitwa kila majina ya hovyo kama wamezungusha vilaza na mambo ya ajabu ajabu.

Kwanza sio kweli wanaofeli sekondari basi hawawezi chochote maishani kana kwamba ni ndondocha au mataahira.

Wapo waliofeli kwa kukosa maandalizi mazuri ikiwemo upungufu wa madarasa walimu na vifaa vya kufundishia kama maabara etc.

Sasa kusema fulani kazungusha kana kamba katenda jinai hapana ifike wakati sasa tukatae namna hii ya unyanyapaa na ifike sehemu watoto wakifeli wazazi wawashitaki walimu na wadai fidia. Ni jukumu la mwalimu kumfdundisha mtoto nani dhamana yake.
Umeshawahi ona aliyepata division one akiomba kutumia cheti cha mtu mwingine..?? Tatizo la kutumia vyeti vya watu wengine linaanzia kwenye kuzungusha.... LAZIMA TUKEMEE UZUNGUSHAJI

Kudeal na utumiaji wa vyeti vya watu wengine ni kushughurika na matokeo pekee... tuhusishe source pia...
 
Ungekua mwanangu ninge kunywea supu ita ukoo wako mkapige iyo vita bashite we[emoji57][emoji57][emoji57]
 
hapana sikubaliani na wewe, jiulize mwaka jana azania ilishika mkia wakati shule inawalimu zaidi ya wale wanaohitajika kitaalamu inakila nyenzo tena iko mita chache kutoka makao makuu ya wizara hapo walimu na maafisa elimu lazima wabebe lawama za kufeli kwa watoto.
Soma tena nilichoandika utanielewa. Niliandika "Lakini kushitaki walimu ni ngumu sana labda kama darasa zima limepata 0 na umewapa walimu environment nzuri ya kufundishia pamoja na vijana wazuri". Kwa mfano uliotoa inamaana shule (mazingira na walimu) iko safi. Je walimu wako walikuwa na motisha ya kufundisha? Wanafunzi je? Kushika mkia sio issue kama bado wanafunzi wamefanya vizuri kwani lazima shule moja au zaidi zishike mkia. Ufaulu wao ulikuaje na umesambaa vipi (distribution). Kama unahakika walimu walikuwa wakutosha, wanavigezo vinavyotakiwa na hawana tatizo la motisha na wanafunzi wamefanya vibaya (in absolute terms) ndio utakuwa na haki ya kuwawajibisha.
 
Unajua hiyo division zero inashangaza wengi!!! Ata mimi nashangaa mtu atapataje F zote? Ila nimekuja kuelewa kua viwango vya uelewa tumepishana na kama umepata division one haimaanishi kumnyanyapaa aliepata zero kwani kuna sehemu nae ni bora kuliko wewe. Wengi tu ajilinganisha na wengine, hii si sahihi!!! Hujui maisha mwenzako alioishi na anayoishi, hujui kilichopo moyoni mwake... Ufaulu wa mtu ni zaidi ya kuhudhuria vipindi darasani, kuna vichocheo vingi sana.

Sister wangu akiwa form 2 aliwaambia kabisa wazazi kua mimi shule haipandi, naomba nisome ujuzi fulani. Kasoma, kapata kazi nzuri na ana heshima zake saivi. Ukiona ishu za darasani uko vibaya, nenda pale unapoona utakua vizuri.
 
Ni kwa muda sasa umekuwepo unyanyapaaji mkubwa kwa watu wanaoshindwa masomo ya sekondari maarufu kama ''div zero''

wanaitwa kila majina ya hovyo kama wamezungusha vilaza na mambo ya ajabu ajabu.

Kwanza sio kweli wanaofeli sekondari basi hawawezi chochote maishani kana kwamba ni ndondocha au mataahira.

Wapo waliofeli kwa kukosa maandalizi mazuri ikiwemo upungufu wa madarasa walimu na vifaa vya kufundishia kama maabara etc.

Sasa kusema fulani kazungusha kana kamba katenda jinai hapana ifike wakati sasa tukatae namna hii ya unyanyapaa na ifike sehemu watoto wakifeli wazazi wawashitaki walimu na wadai fidia. Ni jukumu la mwalimu kumfdundisha mtoto nani dhamana yake.
na akitumia jina la mtu pia tusi mnyanyapae?
 
Hakuna anayewanyanyapaa, kinachotakiwa wakae katika nafasi zinazoendana na elimu zao.
 
Ila nduguyanguuu kuna watu tumesoma mazingira magumu sana na misuli yatima na kumuomba mungu tukapata angalauuu si haba sasa unataka kuwafunza nini wadogo zetu usitetee ujinga msingi wa kupata zero uliujenga mwenyewe
Kama Mwenyekiti wako
 
Mtu amepata Divsion 0 anapigana akipenya anasoma DIPLOMA, hii diploma inampeleka mpaka chuo kikuu tena akiwa kisu, core science. sasa hapa tatizo ni waalimu wa Seco, wajinga sana wale watu, siyo sec, zoote but some of them wanapoteza future ya watoto,

wakati mwingine wazazi wanachangia wattoto kutofanya vizuri, mfano mzazi kufokafoka hovyo mpaka mate yanaruka, pale mtoto akikosea kidogo kana kwamba wao wazazi wanawaonea wivu watoto wao. hasa mdingi akiwa na li mama la kambo pembeni akitaka sifa utasoma number zote za matusi,

Utasikia ''kwanza toto hili halikushinda kwa akili zake'' linatafuta chuo hivi vyuo ni aghali sana ntapoteza hela zangu tu, unaoondoka Mungu saidia unapata chuo kilekile agahli unapasua na Distinction juu bila yeye kujua, siku unarudi na gamba hata hongera hakupi, unapiga kimya na wewe! atakuskia tu!
 
Back
Top Bottom