Tuombe tuondokane na haya ya Wanasiasa uendawazimu

Tuombe tuondokane na haya ya Wanasiasa uendawazimu

SYLLOGIST!

JF-Expert Member
Joined
Dec 28, 2007
Posts
8,853
Reaction score
8,248
Mwenyekiti wa Chadema Mh. Mbowe Wakati akiwa katika hafla au ufunguzi wa mikutano ya kisiasa, iliyopigwa marufuku kwa takriban miaka sita Nchini Mjini Mwanza, Tanzania. Alimaka.

Wakati wa hotuba yake, alieleza safari yake, ya CHADEMA na Vyama vingine vya siasa ilivyokuwa ndefu na ngumu iliyomfanya kusimamia haki na demokrasia nchini.

Alielezea ujana wake pamoja na historia fupi ya Chadema ambapo alimtaja marehemu Bob Makani (msukuma)🤔 na ambaye alikuwa Katibu Mkuu wa Chadema miaka 30 iliyopita. Aliwataja na Viongozi wengine wengi.

Aliendelea kutoa sababu na shauku ya kutafuta maridhiano, kuundwa kwa tume mpya ya uchaguzi miongoni mwa mengine baada ya kuachiliwa kutoka gerezani/kizuizini na kutaja manufaa mapana ya kutoka kwake kwa nchi yetu na mustakabali wa nchi yetu na kwa nini alimpongeza Mheshimiwa Rais muda mfupi baada ya kuachiwa huru.

Pia, wakati wa hotuba yake ambayo ilikuwa ya kusisimua, kuamsha, yenye shauku, na ya kushangaza wakati fulani, aliweza kueleza, kwa umakini, na busara dhidi ya mgongo wa ucheshi wake, "Cha Arusha"... ambapo umati ulikubaliana na vifijo! Umuhimu wa Maridhiano. Umuhimu wa Haki, Umuhimu wa Kuacha Uhasama Umuhimu wa Katiba Mpya n.k.nk.

Hata hivyo, mahali fulani alianza kuamsha hisia, hasa alipoanza kusema kuna jambo lazima aliongeleee hata kama wengi wata udhika/ kasirika... mdomo wangu ukadondoka mapigo ya moyo yakapanda, moyo wangu ukaanza kudunda, nilidhani leo ndio leo siku ambae atamsulubisha Hayati "J.P.M" ata ukweza umati wa watu ukimsikiliza, kutoka uwanjani na kwingineko, kutoka Australia hadi Zimbabwe yaani dunia nzima. Uwanja ulikuwa kimya kabisa kwa sekunde moja isipokuwa kwa sauti moja ambayo ungeweza kuisikia mara nyingi chinichini akibwabwaja😂 Lakini kwa hatua yake ya mahesabu, na "Udingi" mbele alituliza hofu na matarajio ya wengi nikiwa mmojawapo.

Akatajwa Rais Samia S.H... Uwiii.😥 ilikuwa hatari.

Mshtuko ulififia, nilipata tena ujasiri wa kuendelea kusikiliza, nikijua ataendelea bila uovu au kama alivyoitaja, kwa ufasaha, "propaganda za kitoto".

Fasta fasta... Nilisikia uongo ambao umeambiwa/umeenezwa mara kwa mara, propaganda na uwongo ulioenea kwa nguvu na uhasama ambazo zimesambazwa kwa uangalifu, na umakini mkubwa yaani kupotosha historia, na kudai uongo uliochochewa na wale wanaoifuja bila kuchoka Nchi yetu na Bara letu. Mafisadi, Wazandiki. Kuwa.... Hayati Raisi

"Alikataa uwepo wa Corona Nchini".

...najiuliza...

Kwani kurudia uwongo huo wa "Childish Propaganda" mara kwa mara, sio uwendanaIzimu lakini kabla hata sijamaliza mawazo yangu, alisema "Ni Uwendanazimu" "Nimwendawazimu" Nilibaki najiuliza nani sasa ni Mwendawazimu.??

UwendawaZimu au kwa kimombo Insanity.

Kwa Tafsiri fupi, ni ukichaa ni tusi. Neno hilo au msamiati huo unamaanisha "Kukosekana kwa akili" Kichaa. Mgonjwa wa Akili!

Je Mh. Mbowe Amemtusi Hayati Raisi J.P.M?
Je hayo maridhiano anayotafuta ni kwa mustakabhali wa nchi au ni wa kibinafsi? Bado ana kinyongo?

Kwa kimombo... By any definition it was an ill-advised choice of word, however, ulimi ulisha tema cheche, it was reckless. The words did not fit well, in my view, its counter-intuitive, as it appears, it was a shift from a well-prepared, well-reviewed, well-rehearsed and coerced speech geared towards a true and real Reconciliation cry! A true counter to a well-propagated propaganda "Childish Propaganda" Sweeping the country. There is a saying that doing the same thing over and over again and while hoping for a different result is "Uwendawazimu" :-Kuendelea kusema na kueneza uwongo kuhusu Hayati Magufuli alikataa uwepo wa Corona Nchini ndio Uwendazimu wenyewe. Wewe ndie Mwendawazimu.

Kipi cha ajabu alichokifanya JPM kuitwa Kichaa? Mwendawazimu?
Nawasilisha😥🤔.
 
Naona umeumizwa kwa sababu ya ukweli aliosema, ulitaka awe muongo, au afiche ukweli..

Swali la msingi kwako, Corona ilikuwepo au haikuwepo? kama ilikuwepo, iliua au haikuua? kama iliua, basi kaa utulie.
 
Naona umeumizwa kwa sababu ya ukweli aliosema, ulitaka awe muongo, au afiche ukweli..

Swali la msingi kwako, Corona ilikuwepo au haikuwepo?
Ilikuwepo
kama ilikuwepo, iliua au haikuua?
Iliua
kama iliua, basi kaa utulie.
Unanilazimisha, na Unalazimisha.


Mbowe Amedanganya, Amemtusi. Halafu anataka maridhiano.

Denoj, Ulikuwa huna sababu ya kuja kuniparamia kwa hoja yako hafifu. Dead on arrival.

Nimekujibu niwezavyo, unavyostahili..

Magufuli hakukataa Uwepo au Vifo uliotokana na Corona. Period.
 
Naona umeumizwa kwa sababu ya ukweli aliosema, ulitaka awe muongo, au afiche ukweli..
Uwongo Aliousema ndio umeniuma, haswa. Ukweli anaouficha ndio huo wa kutaka Tume kama ya Desmond Tutu Ili aje waachiwe hata pale ikionekana naye ameficha Ukweli.

Udikteta wake ulionekana pale uwanjani, wazi wazi.
 
Mwenyekiti wa Chadema Mh. Mbowe Wakati akiwa katika hafla au ufunguzi wa mikutano ya kisiasa, iliyopigwa marufuku kwa takriban miaka sita Nchini Mjini Mwanza, Tanzania. Alimaka....

Wakati wa hotuba yake, alieleza safari yake, ya CHADEMA na Vyama vingine vya siasa ilivyokuwa ndefu na ngumu iliyomfanya kusimamia haki na demokrasia nchini.

Alielezea ujana wake pamoja na historia fupi ya Chadema ambapo alimtaja marehemu Bob Makani (msukuma)🤔 na
ambaye alikuwa Katibu Mkuu wa Chadema miaka 30 iliyopita. Aliwataja na Viongozi wengine wengi.

Aliendelea kutoa sababu na shauku ya kutafuta maridhiano, kuundwa kwa tume mpya ya uchaguzi miongoni mwa mengine baada ya kuachiliwa kutoka gerezani/kizuizini.... na kutaja manufaa mapana ya kutoka kwake kwa nchi yetu na mustakabali wa nchi yetu na kwa nini alimpongeza Mheshimiwa Rais muda mfupi baada ya kuachiwa huru.

Pia, wakati wa hotuba yake ambayo ilikuwa ya kusisimua, kuamsha, yenye shauku, na ya kushangaza wakati fulani, aliweza kueleza, kwa umakini, na busara dhidi ya mgongo wa ucheshi wake, "Cha Arusha"... ambapo umati ulikubaliana na vifijo! Umuhimu wa Maridhiano. Umuhimu wa Haki, Umuhimu wa Kuacha Uhasama Umuhimu wa Katiba Mpya n.k.nk.



Hata hivyo, mahali fulani alianza kuamsha hisia, hasa alipoanza kusema kuna jambo lazima aliongeleee hata kama wengi wata udhika/ kasirika..mdomo wangu ukadondoka mapigo ya moyo yakapanda, moyo wangu ukaanza kudunda, nilidhani leo ndio leo siku ambae atamsulubisha Hayati "J.P.M" ata ukweza umati wa watu ukimsikiliza, kutoka uwanjani na kwingineko, kutoka Australia hadi Zimbabwe yaani dunia nzima. Uwanja ulikuwa kimya kabisa kwa sekunde moja isipokuwa kwa sauti moja ambayo ungeweza kuisikia mara nyingi chinichini akibwabwaja😂 Lakini kwa hatua yake ya mahesabu, na "Udingi" mbele alituliza hofu na matarajio ya wengi nikiwa mmojawapo,

Akatajwa Raisi Samia S.H... Uwiii.😥 ilikuwa hatari.


Mshtuko ulififia, nilipata tena ujasiri wa kuendelea kusikiliza, nikijua ataendelea bila uovu au kama alivyoitaja, kwa ufasaha, "propaganda za kitoto".

Fasta fasta....nilisikia uongo ambao umeambiwa/ umeenezwa mara kwa mara, propaganda na uwongo ulioenea kwa nguvu na uhasama ambazo zimesambazwa kwa uangalifu, na umakini mkubwa yaani kupotosha historia, na kudai uongo uliochochewa na wale wanaoifuja bila kuchoka Nchi yetu na Bara letu. Mafisadi, Wazandiki. Kuwa.... Hayati Raisi

"Alikataa uwepo wa Corona Nchini".

...najiuliza...
Kwani kurudia uwongo huo wa "Childish Propaganda" mara kwa mara, sio uwendanaIzimu lakini kabla hata sijamaliza mawazo yangu, alisema "Ni Uwendanazimu" "Nimwendawazimu" Nilibaki najiuliza nani sasa ni Mwendawazimu.??




UwendawaZimu au kwa kimombo Insanity.

Kwa Tafsiri fupi, ni ukichaa ni tusi. Neno hilo au msamiati huo unamaanisha "Kukosekana kwa akili" Kichaa. Mgonjwa wa Akili!

Je Mh. Mbowe Amemtusi Hayati Raisi J.P.M?
Je hayo maridhiano anayotafuta ni kwa mustakabhali wa nchi au ni wa kibinafsi? Bado ana kinyongo?

Kwa kimombo....by any definition it was an ill advised choice of word, however ulimi ulisha tema cheche, it was reckless. The words did not fit well, in my view, its counter intuitive, as it appears, it was a shift from a well prepared, well reviewed, well rehearsed and coerced speech geared towards a true and real Reconciliation cry! A true counter to a well propagated propaganda "Childish Propaganda" Sweeping the country. There is a saying that doing the same thing over and over again and while hoping for a different result is "Uwendawazimu" :-Kuendelea kusema na kueneza uwongo kuhusu Hayati Magufuli alikataa uwepo wa Corona Nchini ndio Uwendazimu wenyewe. Wewe ndie Mwendawazimu.

Kipi cha ajabu alichokifanya JPM kuitwa Kichaa? Mwendawazimu?
Nawasilisha😥🤔.

Huyo bwana aliwahi kusema kateua vichaa wenzake
 
Mtu akishakufa huenda na habari zake...

Kumtaja au kutomtaja JPM hakuwezi msaidia mtu yoyote kwa sasa kama hawa watesi walio hai hatuwezi kuwashinda...

Ujinga, Umasikini na Rushwa.
 
Mwenyekiti wa Chadema Mh. Mbowe Wakati akiwa katika hafla au ufunguzi wa mikutano ya kisiasa, iliyopigwa marufuku kwa takriban miaka sita Nchini Mjini Mwanza, Tanzania. Alimaka....

Wakati wa hotuba yake, alieleza safari yake, ya CHADEMA na Vyama vingine vya siasa ilivyokuwa ndefu na ngumu iliyomfanya kusimamia haki na demokrasia nchini.

Alielezea ujana wake pamoja na historia fupi ya Chadema ambapo alimtaja marehemu Bob Makani (msukuma) na
ambaye alikuwa Katibu Mkuu wa Chadema miaka 30 iliyopita. Aliwataja na Viongozi wengine wengi.

Aliendelea kutoa sababu na shauku ya kutafuta maridhiano, kuundwa kwa tume mpya ya uchaguzi miongoni mwa mengine baada ya kuachiliwa kutoka gerezani/kizuizini.... na kutaja manufaa mapana ya kutoka kwake kwa nchi yetu na mustakabali wa nchi yetu na kwa nini alimpongeza Mheshimiwa Rais muda mfupi baada ya kuachiwa huru.

Pia, wakati wa hotuba yake ambayo ilikuwa ya kusisimua, kuamsha, yenye shauku, na ya kushangaza wakati fulani, aliweza kueleza, kwa umakini, na busara dhidi ya mgongo wa ucheshi wake, "Cha Arusha"... ambapo umati ulikubaliana na vifijo! Umuhimu wa Maridhiano. Umuhimu wa Haki, Umuhimu wa Kuacha Uhasama Umuhimu wa Katiba Mpya n.k.nk.



Hata hivyo, mahali fulani alianza kuamsha hisia, hasa alipoanza kusema kuna jambo lazima aliongeleee hata kama wengi wata udhika/ kasirika..mdomo wangu ukadondoka mapigo ya moyo yakapanda, moyo wangu ukaanza kudunda, nilidhani leo ndio leo siku ambae atamsulubisha Hayati "J.P.M" ata ukweza umati wa watu ukimsikiliza, kutoka uwanjani na kwingineko, kutoka Australia hadi Zimbabwe yaani dunia nzima. Uwanja ulikuwa kimya kabisa kwa sekunde moja isipokuwa kwa sauti moja ambayo ungeweza kuisikia mara nyingi chinichini akibwabwaja Lakini kwa hatua yake ya mahesabu, na "Udingi" mbele alituliza hofu na matarajio ya wengi nikiwa mmojawapo,

Akatajwa Raisi Samia S.H... Uwiii. ilikuwa hatari.


Mshtuko ulififia, nilipata tena ujasiri wa kuendelea kusikiliza, nikijua ataendelea bila uovu au kama alivyoitaja, kwa ufasaha, "propaganda za kitoto".

Fasta fasta....nilisikia uongo ambao umeambiwa/ umeenezwa mara kwa mara, propaganda na uwongo ulioenea kwa nguvu na uhasama ambazo zimesambazwa kwa uangalifu, na umakini mkubwa yaani kupotosha historia, na kudai uongo uliochochewa na wale wanaoifuja bila kuchoka Nchi yetu na Bara letu. Mafisadi, Wazandiki. Kuwa.... Hayati Raisi

"Alikataa uwepo wa Corona Nchini".

...najiuliza...
Kwani kurudia uwongo huo wa "Childish Propaganda" mara kwa mara, sio uwendanaIzimu lakini kabla hata sijamaliza mawazo yangu, alisema "Ni Uwendanazimu" "Nimwendawazimu" Nilibaki najiuliza nani sasa ni Mwendawazimu.??




UwendawaZimu au kwa kimombo Insanity.

Kwa Tafsiri fupi, ni ukichaa ni tusi. Neno hilo au msamiati huo unamaanisha "Kukosekana kwa akili" Kichaa. Mgonjwa wa Akili!

Je Mh. Mbowe Amemtusi Hayati Raisi J.P.M?
Je hayo maridhiano anayotafuta ni kwa mustakabhali wa nchi au ni wa kibinafsi? Bado ana kinyongo?

Kwa kimombo....by any definition it was an ill advised choice of word, however ulimi ulisha tema cheche, it was reckless. The words did not fit well, in my view, its counter intuitive, as it appears, it was a shift from a well prepared, well reviewed, well rehearsed and coerced speech geared towards a true and real Reconciliation cry! A true counter to a well propagated propaganda "Childish Propaganda" Sweeping the country. There is a saying that doing the same thing over and over again and while hoping for a different result is "Uwendawazimu" :-Kuendelea kusema na kueneza uwongo kuhusu Hayati Magufuli alikataa uwepo wa Corona Nchini ndio Uwendazimu wenyewe. Wewe ndie Mwendawazimu.

Kipi cha ajabu alichokifanya JPM kuitwa Kichaa? Mwendawazimu?
Nawasilisha.
Inaumiza sana, tena inasikitisha sana, chama tulichokuwa tunakitegemea, leo ndio kimefunga ndoa ya jinsia moja?
 
Naona umeumizwa kwa sababu ya ukweli aliosema, ulitaka awe muongo, au afiche ukweli..

Swali la msingi kwako, Corona ilikuwepo au haikuwepo? kama ilikuwepo, iliua au haikuua? kama iliua, basi kaa utulie.
Kama kweli alisema hivyo ni mjinga sana

Mambo ya Magufuli kukataa Corona yamepita na haina haja ya kumsakama kwa manufaa ya Chadema wenyewe kisiasa

Mbowe alitakiwa kufanya truce kati yake na wafuasi wa Magufuli ambao wengi walikuwa wafuasi wa Chadema kabla
 
..Ni kichaa kwasababu ya kujaribu kumuua Tundu Lissu.
JokaKuu,

Inawezekana(as per your inference) , je angekuwa hai kujibu shutuma hizo na kudai alikuwa mwendawazimu wakati aki 'Jaribu kumuua' Watanzania tungemuelewa?

Mkuu unanikumbusha yale aliyoyanena Jenerali Ulimwengu. Sintorudia alichonena, ni gumu kumeza na kwa tamaduni zetu, ni tusi.

...kikuu hapa siyo hulka za Hayati, kikuu hapa ni Uwongo alioudai Mh. Mbowe, na kwa lugha yake aliyotumia "childish propaganda" na hapa, hiyo "childish propaganda" ni huo Uwongo ambao umekomaliwa na mebeberu wa Kisiasa...

..Kuwa Hayati J.P.M alikataa katukatu kuwa hakukuwa na Corona Tanzania!

Huo ni uwongo, na kurudia rudia huo uwongo mara kwa mara Akitegemea "anachafua" historia au "anazika legacy" ndio Uwendazimu kwa definition yako(my inference).

Bado ana kinyongo? Manake wakati anasema hayo alionekana wazi wazi kuwa amekereka-Sasa, anawezaje kudai maridhiano wakati bado yeye akiendelea kumchafua, kumbeza na tusi? Mwendawazimu? Atakubali maridhiano kama yeye abakie na "ugaidi" katika CV yake?

Kupata maridhiano lazima kuwe na uwepo wa Kukubali shari hasi au chanya n.k la aina au?

Ndio Nchi anayotaka kuongoza, ya visasi?
 
Duh...!,
P
Kaka yangu Pascal,
Tunajua Hayati amefanya mengi ya ajabu na ya Kijasiri. Sasa unashangaa lipi, Kuwa alikuwa "Mwendawazimu"? Weww ni mwanasheria hivyo basi najua unaweza ongelea Katiba. Ilikuwaje Katiba imruhusu mtu kama huyo Kuendesha Nchi?

Hakika ni suala nje ya Mada, ni suala lililojadiliwa na Wakina Ulimwengu.

Kikuu hapa ni yale anayodai Mh Mbowe, anaasa kusitisha "Childish propaganda' anadai 'Maridhiano' lakini ni dhahiri amejipindisha?, anatulaghai? kwavile amerudia propaganda kuwa Hayati J.P.M alikataa katukatu uwepo wa Corona nchini...
Kwanini aendelee na huwo uwongo? as he puts it "Childish propaganda" huoni huo ndio Uwendanazimu?

Anawezaje kudai maridhiano kwa ajili ya mustakabhali wa nchi wakati hawezi binafsi?au akiwa bado ana kinyongo? na yaliyomtokea? Na kutupa dongo!
 
BrazaJ, Umeacha mwanya mkubwa na ulichabandika. Sijawahi kusikia hao wawili Mh. Mbowe au Hayati J.P.M wameteua "Vichaa" au Mwendawazimu?
Usiogope kumtaja yeyote.

Asante kwa Taarifa lakini.
 
Mtu akishakufa huenda na habari zake...

Kumtaja au kutomtaja JPM hakuwezi msaidia mtu yoyote kwa sasa kama hawa watesi walio hai hatuwezi kuwashinda...

Ujinga, Umasikini na Rushwa.
Watu 8,

Kuhusu , mtu akishakufa huenda na habari zake, kuna ukweli fulani....na inategemea Tamaduni na Jamii yake?

Hayati J.P.M was not an Ordinary man. alikuwa sio mtu wa kawaida.
Binasi sijui Wasukuma wana kanuni gani kuhusu wafu na habari za wafu....
haijalishi...

Lakini upo sahihi na kuhusu haya...
Ujinga(ignorance) aliouonyesha Mh. Mbowe na Umasikini wa Lugha katika kadamnasi ule, ina leta dhana ya kutumika, kwa makusudi au bila kujua....n inaweza fananishwa na rushwa

Vilevile, Katika maridhiano Mh. Mbowe akubali kulikuwa na ujinga fulani, au alikuwa na sababu gani ya kutupa.dongo lile? ati "Mwendawazimu"

Uwongo ule? J.P.M alikataa uwepo wa corona nchini?

Kuna rushwa hapo?

Bado ana kinyongo? au Akubali umasikini wa Lugha, Ulimi uliteleza?

Asante kwa maono yako. na Taarifa.
 
JPM lazima atajwe kwa kuwa ni sehemu ya historia ya taifa la Tanzania.
Mwandambo,
Sio Watanzania wote ambao wanamtaja taja. Sasa hivi kuna wale wanaomtaja kwa makusudi kumchafulia historia yake. Wanampiga madongo kila kukicha, kama walivyomfanyia Iddi Amini M.B.E cha ajabu ukienda kwa jirani yetu, wanamshukuru sana sana, unabaki unajiuliza kisa kilikuwa ni nini?

Kikuu ni huyu Mh. Mbowe, bado ana kinyongo? Wakati J.K anatengeneza watu 'wasiojulikana' na 'wanaojulikana' au wanavyodai kafanya Ikulu "Kariakoo" mbona hakumuita Mwendawazimu? yaani ndio utajua Kinyongo alichokuwa nacho Mh. Mbowe ni cha kibinafsi(inasadikika) baada ya kupoteza Mjengo uliokaliwa na Familia yake Mjini?

Ni uwendawazimu, kurudia kuongea Uwongo ambao umerudiwa mara kwa mara na wanaotaka kuchafua 'Legacy' yake. Ni uwendawazimu kudai 'Maridhiano' wakati bado amejaa hasira, na ilionekana wazi akiwa anatamka 'Ni Uwendanazimu ni Mwendawazimu' . Sasa, kwa maneno yake kuwa ni wakati wa kuacha "childish Propaganda" na yeye kuendelea na propaganda, sio Uwendawazimu huo?

Nafikiri, alijikwaa, simtetei lakini alionyesha Uwendawazimu wa Kisiasa.
 
Inaumiza sana, tena inasikitisha sana, chama tulichokuwa tunakitegemea, leo ndio kimefunga ndoa ya jinsia moja?
Yivgensi primakovu,
Spaasibo Komarade
.
Ndio inaumiza kuona mtu anayedai anataka kuponyesha nchi anaweka pilipili kwenye kidonda kipone. Nakubalina nawe....Inasikitisha.

Ndoa ya CCM na CHADEMA Ndio imekuwa gumzo haswa. Mmoja anadai au atakuja dai amewezesha hilo, na mwingine atakuja dai ni kwa nguvu zake! Lakini ukweli upo wazi na hauhitaji kamisheni ya ukweli kutambua hilo.

Karibu / pazalusta
 
Back
Top Bottom