Uchaguzi 2020 Tundu Lissu amebadili upepo wa siasa. Watanzania tumuunge mkono

Glenn

JF-Expert Member
May 23, 2015
65,812
156,946
Kwa Watanzania wenye akili timamu mtakubaliana nami kuwa miaka 5 ya awamu hii ya 5, kimekuwa kipindi kigumu sana kilichojaa;

Hofu
Mashaka
Umasikini uliotopea
Ombwe la kiuongozi nk.

Watanzania wengi mioyo yao imejaa mashaka na kutojiamini tena.

Ni enzi za watawala wachache kuneemeka na kufanya walitakalo bila kuwajibishwa na yeyote.

Lakini baada ya Tundu Lissu kuteuliwa kuwa mgombea wa urais na kuanza kitema cheche, naona mioyo ya Watanzania ikihuishwa tena kuingia ulingoni kuipigania Tanzania yenye neema.

Wito wangu, tumuunge mkono huyu shujaa aliyejitoa Sadaka.

Kuthubutu kuyanyooshea kidole mapungufu ya huyu mfalme yahitaji moyo lakini huyu mwamba amedhamiria.

Kwa masikio yangu nimewasikia ccm wengi wakibadili gia angani na kuahidi kumpigia kura Lissu.

Shime Watanzania tuipiganie heshima ya nchi yetu nzuri ya maziwa na asali, upendo na mshikamano

 
Hii ndio Chadema ninayoijua iliyopotea 2015....
Mkuu nimejisikia kuchemka ndani yangu. Pia nimejifunza kitu kuwa hata ujio wa Lowasa kuna wengi waliumia.

Lakini sasa nimeanza kuipna ladha halisi ya upinzani, misimamo ya thabiti na divosheni isiyotia shaka katika kuirejesha Tanzania iliyo bora.
Nilisema ikiwa upinzani utaendelea kupwaya nisingepiga kura tena, lakini sasa nimeanza kuamka upya ndani yangu
 
Nimemsikiliza Tundu Lissu anaongea kama binadamu aliyechanganyikiwa vile ambaye hana matumaini.

Anajaribu kwa kila namna kutafuta huruma ya wananchi na kwa bahati mbaya safari hakuna kura za huruma.

Anafanya uchochezi wa makusudi ili aonekane anaonewa kwa bahati mbaya au nzuri vyombo vya dola vimelitambua hilo na kuamua kumupuiza.

Niwashukuru Chadema kwa kumchagua huyu kupeperusha bendera yenu, maana baada kushindwa vibaya kwenye uchaguzi,uchaguzi wa mwaka 2025 hamtakuwa na propaganda za kitoto.
 
Mkuu kwa sasa watanzania wengi wamesha amua na wapo tayari kumchagua mh Lissu
Kwa Watanzania wenye akili timamu mtakubaliana nami kuwa miaka 5 ya awamu hii ya 5, kimekuwa kipindi kigumu sana kilichojaa;

...Hofu
...Mashaka
...Umasikini uliotopea
...Ombwe la kiuongozi nk.

Watanzania wengi mioyo yao imejaa mashaka
na kutojiamini tena.
Ni enzi za watawala wachache kuneemeka na kufanya walitakalo bila kuwajibishwa na yeyote.

Lakini baada ya Tundu Lisu kuteuliwa kuwa mgombea wa urais na kuanza kitema cheche, naona MIOYO ya Watanzania ikihuishwa tena kuingia ulingoni kuipigania Tanzania yenye neema.

Wito wangu, tumuunge mkono huyu shujaa aliyejitoa sadaka.
Kuthubutu kuyanyooshea kidole mapungufu ya huyu mfalme yahitaji moyo lakini huyu mwamba amedhamiria.
Kwa masikio yangu nimewasikia ccm wengi wakibadili gia angani na kuahidi kumpigia kura Lisu.
Shime Watanzania tuipiganie heshima ya nchi yetu nzuri ya maziwa na asali, upendo na mshikamano

 
Back
Top Bottom