Tunawezaje kutofautisha nyuzi za Britanicca na stori za vijiwe vya kahawa ?

Tunawezaje kutofautisha nyuzi za Britanicca na stori za vijiwe vya kahawa ?

adriz

JF-Expert Member
Joined
Sep 2, 2017
Posts
15,479
Reaction score
33,510
Moja kwa moja.

Mimi ni muumini wa ushahidi, habari zozote bila ushahidi wa uhakika na wa kuamika huwa nazikataa moja kwa Moja au naiweka katika kundi la tetesi na kuzifanyia uchunguzi ili kujua ukweli na uhalisia wa habari yenyewe kwa uhakika.

Siku za karibuni kumekuwa na wimbi la watu wengine ni kama wakosoaji wa serikali na wengine kama wafuaji wa yale ya ndani yaliyojificha yaliyotokea na yanayoendelea , sasa tukija kwenye Mada husika binafsi nimesoma nyuzi kadhaa za Britanicca haswa hizi episode mbili za jana ila sikuona solid evidence katika nyuzi zake zote zaidi kujikita katika masimulizi na tuhuma tu.

Swala la ushahidi nalitilia umakini mkubwa sababu katika ulimwengu huu mtu ni rahisi sana kupelekwa na upepo wa propaganda au kusuka vizuri habari ya uwongo na ikaonekana ukweli au kutia chumvi kwenye ukweli wenyewe kutoka na uadui , chuki , maslahi nk #EvidenceIsAPower

Sasa kama ushahidi wa kuaminika katika habari na tuhuma ukawa unapuuzwa tunaweza kutenganisha vipi habari tuzazoziamini zinazoletwa na watu na zile stori maarufu za kutunga na soga za vijiwe vya kahawa ? tukipuuza Hilo na tusihoji mtu yeyote anaweza kuwa source of information akaamka na habari yeyote anayoiona ya sawa na tukamuamini pia.

Nyongeza ;
Mhusika ana historia ya kutoa tabiri feki na mikeka yake mingine kuchanika vibaya . Pamoja na hiyo baadhi ya members wamekuwa wakimtuhumu kutoa taarifa za uongo na kukurupuka katika majambo , hapo inatia mashaka kidogo kumuamini Moja kwa moja.

Hii Screenshot nimetoa katika comment ya uzi wake mmoja wa codes ambao umefeli vilevile kuleta matokeo tarajiwa.
IMG_20250829_194631.jpg
 
Si ndio hata Mimi nashangaa mtu anasema kikwete kamuua magufuli
How?
Picha?

Bora kidogo hata mange Yule kama Leo kazungumzia magari ya kifahari waliyo nayo watoto wa vigogo na kweli Kaweka na picha zake hayo magari kidogo unaamini...

Sio eti uamini kila habari kisa mtu anakaa Russia

Polepole na ye yuko vzr maana anaongea kitu na mifano kabisa kwamba alishauri hiki akamfuata mzee Fulani n.k vitu ambavyo hata hao wanaotajwa hawakatai means NI ukweli.. sometimes tuacheni unyumbu
 
Moja kwa moja.

Mimi ni muumini wa ushahidi, habari zozote bila ushahidi wa uhakika na wa kuamika huwa nazikataa moja kwa Moja au naiweka katika kundi la tetesi na kuzifanyia uchunguzi ili kujua ukweli na uhalisia wa habari yenyewe kwa uhakika.

Siku za karibuni kumekuwa na wimbi la watu wengine ni kama wakosoaji wa serikali na wengine kama wafuaji wa yale ya ndani yaliyojificha yaliyotokea na yanayoendelea , sasa tukija kwenye Mada husika binafsi nimesoma nyuzi kadhaa za Britanicca haswa hizi episode mbili za jana ila sikuona solid evidence katika nyuzi zake zote zaidi kujikita katika masimulizi na tuhuma tu.

Swala la ushahidi nalitilia umakini mkubwa sababu katika ulimwengu huu mtu ni rahisi sana kupelekwa na upepo wa propaganda au kusuka vizuri habari ya uwongo na ikaonekana ukweli au kutia chumvi kwenye ukweli wenyewe kutoka na uadui , chuki , maslahi nk #EvidenceIsAPower

Sasa kama ushahidi wa kuaminika katika habari na tuhuma ukawa unapuuzwa tunaweza kutenganisha vipi habari tuzazoziamini zinazoletwa na watu na zile stori maarufu za kutunga na soga za vijiwe vya kahawa ? tukipuuza Hilo na tusihoji mtu yeyote anaweza kuwa source of information akaamka na habari yeyote anayoiona ya sawa na tukamuamini pia.
Mimi tangu alipokuja na hekaya eti kuna mtu yuko kwenye friji huko Uturuki nikasema kweli huyu mtu ni hamnazo. Lakini lakushangaza wala hakomi..na kuna watu na akili zao kabisa wanaona kama ni mtu reliable kabisa. Kumbe ni mavi ya kuku.
 
Ukiona chakula hauwezi kukila,singizia una mzio/allergy nacho.Lakini,umekula sahani nne zilizojaa tele halafu ujidai tu mpishi hakuuzungusha upawa vizuri wakati anakupakulia mboga ndiyo maana haujashiba,huo ni zaidi ya upambaff!
 
Hakuna Utofauti..Sasa Wewe Unadhani Hao Unao Onana Nao Huko Vijiweni Na Ulimwenguni Kiujumla Ni Watu Tofauti Na Huku Mitandaoni...??
 
Ndo wale watu wakimuona mtu ni chizi mtaani wanamuita usalama wa taifa , ukimwambia thibitisha hana jibu zaidi ya kukwambia "Kama huamini we haya"
Inasikitisha sana..
 
Back
Top Bottom