meningitis
JF-Expert Member
- Nov 17, 2010
- 8,464
- 4,829
Hili ni swali kwa wote UKAWA ASILIA na UKAWA Mabadiliko.
UKAWA ilianza kama muungano usio rasmi wa wananchi wanaotaka rasimu ya katiba ya judge Warioba.
Hapa UKAWA ilikuwa hot kweli kweli na ilikuwa serious.
Ukawa hii ilijumuisha watu mbalimbali kutokea kwenye vyama vya siasa na asasi za kiraia.
Baadae tukaona mchujo wa kimyakimya ukianza kushika kasi na hatimaye tukafika hatua ya kubaki na viongozi wa vyama vinne vya kisiasa.Baadaye zaidi tukaona ajenda ya katiba mpya inatulizwa pembeni na kukawekwa makubaliano ya Kusimamisha mgombea urais kupitia UKAWA.
UKAWA ukatoka kuwa umoja wa katiba ya wananchi na kuwa umoja wa vyama vinne.
Hapa tukaanza kusikia Badiliko la kwanza la Salamu yaani badala ya salamu moja ya Peoplez(kumbuka koti hili la UKAWA lilikuwa na rangi ya kakh) tukapata salamu nne...yaani peoplezz,Nccr,Haki na Motomoto.
Hata kwenye ufunguzi wa kampeni za urais tulizisikia.
Muda haukupita Salamu tatu zikaanza kufifia huku ile ya peoplezz ikirudi kwenye chati kabla ya mwenyekiti kuja na salamu mpya yaani mabadiliko yote yataitwa lowassa.
Kampeni zikashika kasi lakini kukawa na ukakasi wa watu kuikubali au kuizoea hii salamu ya mabadiliko ...sasa leo naona ile salamu ya asili imerejeshwa tena yaani peoplezzz!!
Sasa mimi najiuliza je mabadiliko ni salamu au?
Watanzania wanajiuliza mabadiliko ni salamu?
Wale wa vyama vitatu yaani CUF,NCCR na NLD wanajiuliza mabadiliko ni kwenye salamu tu?
Tunaendelea kukumbushwa kuwa hatuendi kuchagua Genge la kishikaji kuingia ikulu bali taasisi yenye ukamilifu wa kimaono,kimipango,kirasilimali,kimiongozo na yenye kila sifa ya kuitwa taasisi.
Tunaenda kuchagua taasisi yenye utambulisho kutokana na muundo wake,sera zake na misimamo yake.
Mimi siamini katika mabadiliko ya salamu hata kidogo kwani siko tayari kubadilishiwa salamu baada ya kupiga kura.
TUPINGANE KWA HOJA!
UKAWA ilianza kama muungano usio rasmi wa wananchi wanaotaka rasimu ya katiba ya judge Warioba.
Hapa UKAWA ilikuwa hot kweli kweli na ilikuwa serious.
Ukawa hii ilijumuisha watu mbalimbali kutokea kwenye vyama vya siasa na asasi za kiraia.
Baadae tukaona mchujo wa kimyakimya ukianza kushika kasi na hatimaye tukafika hatua ya kubaki na viongozi wa vyama vinne vya kisiasa.Baadaye zaidi tukaona ajenda ya katiba mpya inatulizwa pembeni na kukawekwa makubaliano ya Kusimamisha mgombea urais kupitia UKAWA.
UKAWA ukatoka kuwa umoja wa katiba ya wananchi na kuwa umoja wa vyama vinne.
Hapa tukaanza kusikia Badiliko la kwanza la Salamu yaani badala ya salamu moja ya Peoplez(kumbuka koti hili la UKAWA lilikuwa na rangi ya kakh) tukapata salamu nne...yaani peoplezz,Nccr,Haki na Motomoto.
Hata kwenye ufunguzi wa kampeni za urais tulizisikia.
Muda haukupita Salamu tatu zikaanza kufifia huku ile ya peoplezz ikirudi kwenye chati kabla ya mwenyekiti kuja na salamu mpya yaani mabadiliko yote yataitwa lowassa.
Kampeni zikashika kasi lakini kukawa na ukakasi wa watu kuikubali au kuizoea hii salamu ya mabadiliko ...sasa leo naona ile salamu ya asili imerejeshwa tena yaani peoplezzz!!
Sasa mimi najiuliza je mabadiliko ni salamu au?
Watanzania wanajiuliza mabadiliko ni salamu?
Wale wa vyama vitatu yaani CUF,NCCR na NLD wanajiuliza mabadiliko ni kwenye salamu tu?
Tunaendelea kukumbushwa kuwa hatuendi kuchagua Genge la kishikaji kuingia ikulu bali taasisi yenye ukamilifu wa kimaono,kimipango,kirasilimali,kimiongozo na yenye kila sifa ya kuitwa taasisi.
Tunaenda kuchagua taasisi yenye utambulisho kutokana na muundo wake,sera zake na misimamo yake.
Mimi siamini katika mabadiliko ya salamu hata kidogo kwani siko tayari kubadilishiwa salamu baada ya kupiga kura.
TUPINGANE KWA HOJA!