SENGANITU
Member
- Sep 19, 2012
- 50
- 15
Salamu kwa wana JF wote!!!
Mimi napendekeza aina ya elimu itakayotufaa watanzania kwa wakati huu na kwa miaka mingi ya baadae.
1.Iwe ni ya lazima kuanzia darasa la kwanza hadi kidato cha nne
2.Iwe ni ya kumwezesha mtanzania kujitegemea,kujiajiri na kuwa waajiri (sio kutegemea kuajiriwa tu)
3.Masomo ya mchepuo yawepo pia ya masomo mawili mfano pc,hl...
4.Walimu wawe ni wale waliofaulu na kuthibitishwa kwa ujuzi wao,shule za msingi walimu wawe na diploma ya elimu.
5.Taasisi zote zinazotoa mafunzo ya kiweledi zihusishe kozi zinazohusu watu wenye mahitaji maalum kama vile wasioona,wasiosikia,n.k. na kwamba hizo taasisi zihusishe na watu wenye mahitaji maalum kama wawezeshaji au wasomaji
6.Kwa kuwa elimu ndiyo ngao kubwa ya kumletea mtu mwanga wa kujitegemea na kulisaidia taifa hili,hivyo kipaumbele cha bajeti namba moja miaka yote kiwe elimu
7.Umri wa kuanza darasa la kwanza uwe miaka mitano(5) kutokana na uwezo wa ufahamu wa binadamu kuongezeka,maumbile ya binadamu kukua haraka,na life span(kwa tz) kupungua
8.Somo la mahusiano ya kimataifa lifundishwe kuanzia kidato cha kwanza kwa kuwa sasa dunia inakuja pamoja kwa mitazamo na maendeleo ya kimataifa.
9.Mfumo mzima wa elimu utawaliwe na watu wenye taaluma inayohusu mambo ya kielimu(wanasiasa wasiingilie mambo ya maamuzi ya kielimu)
10.Ada ifutwe kuanzia shule ya msingi hadi kidato cha sita ili watanzania wengi waweze kupata elimu bila kikwazo.
Najua wana jf mna mengi ya kuzungumza kwa hili,karibuni kuchangia mada yetu,nawasilisha kwenu.
Mimi napendekeza aina ya elimu itakayotufaa watanzania kwa wakati huu na kwa miaka mingi ya baadae.
1.Iwe ni ya lazima kuanzia darasa la kwanza hadi kidato cha nne
2.Iwe ni ya kumwezesha mtanzania kujitegemea,kujiajiri na kuwa waajiri (sio kutegemea kuajiriwa tu)
3.Masomo ya mchepuo yawepo pia ya masomo mawili mfano pc,hl...
4.Walimu wawe ni wale waliofaulu na kuthibitishwa kwa ujuzi wao,shule za msingi walimu wawe na diploma ya elimu.
5.Taasisi zote zinazotoa mafunzo ya kiweledi zihusishe kozi zinazohusu watu wenye mahitaji maalum kama vile wasioona,wasiosikia,n.k. na kwamba hizo taasisi zihusishe na watu wenye mahitaji maalum kama wawezeshaji au wasomaji
6.Kwa kuwa elimu ndiyo ngao kubwa ya kumletea mtu mwanga wa kujitegemea na kulisaidia taifa hili,hivyo kipaumbele cha bajeti namba moja miaka yote kiwe elimu
7.Umri wa kuanza darasa la kwanza uwe miaka mitano(5) kutokana na uwezo wa ufahamu wa binadamu kuongezeka,maumbile ya binadamu kukua haraka,na life span(kwa tz) kupungua
8.Somo la mahusiano ya kimataifa lifundishwe kuanzia kidato cha kwanza kwa kuwa sasa dunia inakuja pamoja kwa mitazamo na maendeleo ya kimataifa.
9.Mfumo mzima wa elimu utawaliwe na watu wenye taaluma inayohusu mambo ya kielimu(wanasiasa wasiingilie mambo ya maamuzi ya kielimu)
10.Ada ifutwe kuanzia shule ya msingi hadi kidato cha sita ili watanzania wengi waweze kupata elimu bila kikwazo.
Najua wana jf mna mengi ya kuzungumza kwa hili,karibuni kuchangia mada yetu,nawasilisha kwenu.