Uchaguzi 2020 Tunapenda Dkt. Wilson Mahera na wenzake wasikie sauti ya Askofu ambayo inawakilisha watetezi wa haki wote nchini

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,789
288,020
Video iliyoambatanishwa hapo chini ni ya Dkt. Wilson Mahera alipokuwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Arusha Mjini alipokuwa akiongea na Makada na Viongozi wa CCM na kusisitiza kuwa yeye [na Wakurugenzi wenzake] hawakuokotwa tu bali walipelekwa kule [katika majukumu ya Ukurugenzi] kikazi zaidi.

Kwa sasa Dkt. Wilson Mahera ndiye Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC). Huyu ndiye anayetakiwa k...uongoza Utendaji ndani ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi inayotarajiwa na kutegemewa kutenda haki kwa kuendesha na kusimamia Uchaguzi ulio Huru na wa Haki. Lakini kauli zake kwenye video hii zinakinzana kabisa na dhana ya Uchaguzi Huru na wa Haki. Kauli zake zinaendana kabisa na kusawiri yanayoendelea sasa katika Majimbo na Kata mbalimbali nchini ambapo idadi kubwa ya Wagombea wa Upinzani wameenguliwa. Huyu ndiye mtu ambaye anashughulikia rufaa zote katika Tume ya Taifa ya Uchaguzi!

Sasa tunapenda Dkt. Wilson Mahera na wenzake wote wasikie sauti ya Askofu ambayo inawakilisha watetezi wa haki wote nchini. Ni sauti inayowakilisha wale wote wanaoporwa haki zao kwa hila, nguvu na ubabe! Kwamba Mungu ndiye aliyetoa afya, uzima na uhai kwa Dkt. Mahera na wenzake. Mungu mwenye haki anatarajia watu wote wenye mamlaka akiwemo Dkt. Wilson Mahera watende haki. Kinyume cha hapo ni kuamsha hasira za Mungu dhidi yao. Dkt. Wilson Mahera na wenzake ndani ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi wanayo nafasi ya kurekebisha makosa yaliyofanywa na Wasaidizi wao (Wasimamizi na Wasimamizi Wasaidizi Wasaidizi) na wao wenyewe. Ujumbe huu pia uwafikie Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar. Kwamba Tume zote mbili ziache kiini macho cha kupitia rufaa za walioenguliwa, bali ziwarejeshe wote katika kinyang'anyiro.

Wasihangaike kumtafuta Askofu bali wahangaike zaidi kutafuta namna ya kurekebisha makosa yaliyofanywa kwa makusudi au kwa kutokukusudia. Njia nyepesi na salama zaidi katika kurekebisha makosa hayo ni kushauri na kushinikiza Tume zote mbili kuwarejesha Wagombea wote walioenguliwa Bara na Visiwani bila masharti ye yote na pasipo kupoteza wakati.

Askofu anatimiza wajibu wake. Ole wake Askofu asipowoanya wanaotenda maovu kwa kufinya na kupora haki za wengine katika nchi (Ezekieli 33:1-20). Sambazeni ujumbe huu hadi katika sebule za watu wote wa Tume, waliowateua, watoto wao, jirani zao, kwa viongozi wao wa kiroho (Makasani na Misikitini), kwa madereva wao, na kwa kila mtu ili ikawe ushahidi juu yao kuwa sauti ya Askofu haikunyamaza juu ya watu hawa na juu ya nchi!
Mwana Kondoo Ameshinda! Tumfuate!

Askofu Mkuu Emmaus Bandekile Mwamakula - Mkuu wa Kanisa la Moravian la Uamsho Tanzania & Afrika Mashariki na Mwenyekiti Mwenza wa Umoja wa Makanisa ya Moravian ya Uamsho Duniani

 
OLE KWA TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI (NEC) NA TUME YA UCHAGUZI ZANZIBAR (ZEC)!

Video iliyoambatanishwa hapo chini ni ya Dkt. Wilson Mahera alipokuwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Arusha Mjini alipokuwa akiongea na Makada na Viongozi wa CCM na kusisitiza kuwa yeye [na Wakurugenzi wenzake] hawakuokotwa tu bali walipelekwa kule [katika majukumu ya Ukurugenzi] kikazi zaidi...
Uwafikie wote wenye mawazo kinzani juu ya ujumbe huu.
 
Wana macho lakini hawaoni, Wana masikio lakini hawasikii.

NEC na ZEC Wana sifa hizo tajwa....mwisho wake siku zote huwa mbaya kama sio wao basi vizazi vyao.
 
Magufuli anataka kubadili katiba kuondoa ukomo wa Rais.

Dalili ndio hizi za kupitisha wabunge wa CCM bila kupingwa.
Kujenga uwanja wa ndege na Ikulu Chato.

Asante Thinktank
Asante PENTAGON
Quote ReplyReport
 
OLE KWA TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI (NEC) NA TUME YA UCHAGUZI ZANZIBAR (ZEC)!

Video iliyoambatanishwa hapo chini ni ya Dkt. Wilson Mahera alipokuwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Arusha Mjini alipokuwa akiongea na Makada na Viongozi wa CCM na kusisitiza kuwa yeye [na Wakurugenzi wenzake] hawakuokotwa tu bali walipelekwa kule [katika majukumu ya Ukurugenzi] kikazi zaidi...
Uchaguzi huu ukivurugika NEC na ZEC lazima wawajibike kwa sababu wameshindwa kusimamia majukumu yao ipasavyo
 
  • Nzuri
Reactions: BAK
Marehemu Mkapa aliona mbali sana alipozungumza hadharani kuhusu umuhimu wa kuwepo Tume Huru na si hii Tume ya wahuni na majizi.

Uchaguzi huu ukivurugika NEC na ZEC lazima wawajibike kwa sababu wameshindwa kusimamia majukumu yao ipasavyo
 
2519249_EJTWRAzWsAAlue5.jpg


Marehemu Mkapa aliona mbali sana alipozungumza hadharani kuhusu umuhimu wa kuwepo Tume Huru na si hii Tume ya wahuni na majizi.
 
Marehemu Mkapa aliona mbali sana alipozungumza hadharani kuhusu umuhimu wa kuwepo Tume Huru na si hii Tume ya wahuni na majizi.
Na sasa ccm nzima imeufyata, hakuna mwenye uthubutu wa kunyanyua kinywa chake kuzungumzia tume huru, mwenye kigoda atakula nao sahani moja

Atlist Mkapa alikua anaweza kukemea na kuzungumza inapobidi, hawa wengine akina mzee wa ruksa kazi yao ni kusifia tuu kwa sababu wanataka watoto wao wapate ulaji
 
Uko sawa kabisa Rafiki ndiyo sababu kuna minong'ono kwamba Mkapa alipewa sumu kwa kuwa alishaonekana ni tishio kwa huu utawala kwa kupinga hadharani huyo anayejiita KICHAA kujiongezea muda madarakani na pia kutaka kuwepo Tume huru kitu ambacho maccm wanakiogopa kama KIFO maana wanajua ndiyo kitakuwa chanzo cha kuzikwa kwao rasmi Nchini na hivyo kupotea milele. Kumbuka pia Rafiki Mangula naye alipinga Membe kufukuzwa ccm akaishia kupewa sumu na hadi hii leo aliyempa hajulikani wakati katika mkutano kulikowepo na wawyu watatu tu naninii, Mangula na Bashiru.

Polisi: Mzee Philip Mangula amekutwa na sumu mwilini, ni baada ya kufanyiwa uchunguzi

Na sasa ccm nzima imeufyata, hakuna mwenye uthubutu wa kunyanyua kinywa chake kuzungumzia tume huru, mwenye kigoda atakula nao sahani moja

Atlist Mkapa alikua anaweza kukemea na kuzungumza inapobidi, hawa wengine akina mzee wa ruksa kazi yao ni kusifia tuu kwa sababu wanataka watoto wao wapate ulaji
 
OLE KWA TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI (NEC) NA TUME YA UCHAGUZI ZANZIBAR (ZEC)!

Video iliyoambatanishwa hapo chini ni ya Dkt. Wilson Mahera alipokuwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Arusha Mjini alipokuwa akiongea na Makada na Viongozi wa CCM na kusisitiza kuwa yeye [na Wakurugenzi wenzake] hawakuokotwa tu bali walipelekwa kule [katika majukumu ya Ukurugenzi] kikazi zaidi...
Safi kabisa baba askofu kwa kusimama upande wa haki . Hawa ndio maaskofu Sasa sio wachumia tumbo , wajasilia dini , Wala kondoo Kama Lile huni la Kawe .Back to point ,Tume haina mamlaka ya kupitisha wagombea eti wamepita bila kupingwa ? Kazi Yao ni kusimamia tu . Wenye mamlaka ya kupitisha au kumkata mgombea ni wananchi peke yake sio tume.
IMG_20200910_181028_8.jpg
 
Uko sawa kabisa Rafiki ndiyo sababu kuna minong'ono kwamba Mkapa alipewa sumu kwa kuwa alishaonekana ni tishio kwa huu utawala kwa kupinga hadharani huyo anayejiita KICHAA kujiongezea muda madarakani na pia kutaka kuwepo Tume huru kitu ambacho maccm wanakiogopa kama KIFO maana wanajua ndiyo kitakuwa chanzo cha kuzikwa kwao rasmi Nchini na hivyo kupotea milele. Kumbuka pia Rafiki Mangula naye alipinga Membe kufukuzwa ccm akaishia kupewa sumu na hadi hii leo aliyempa hajulikani wakati katika mkutano kulikowepo na wawyu watatu tu naninii, Mangula na Bashiru.

Polisi: Mzee Philip Mangula amekutwa na sumu mwilini, ni baada ya kufanyiwa uchunguzi
Very true hata wakati anakaribia kudied aliwaambia walikuwa karibu yake huyu jamaa ananiua , aliyemwekea sumu mangula somebody Magoti ka CCM kipenyo kana nundu mgongoni .
 
Uko sawa kabisa Rafiki ndiyo sababu kuna minong'ono kwamba Mkapa alipewa sumu kwa kuwa alishaonekana ni tishio kwa huu utawala kwa kupinga hadharani huyo anayejiita KICHAA kujiongezea muda madarakani na pia kutaka kuwepo Tume huru kitu ambacho maccm wanakiogopa kama KIFO maana wanajua ndiyo kitakuwa chanzo cha kuzikwa kwao rasmi Nchini na hivyo kupotea milele. Kumbuka pia Rafiki Mangula naye alipinga Membe kufukuzwa ccm akaishia kupewa sumu na hadi hii leo aliyempa hajulikani wakati katika mkutano kulikowepo na wawyu watatu tu naninii, Mangula na Bashiru.

Polisi: Mzee Philip Mangula amekutwa na sumu mwilini, ni baada ya kufanyiwa uchunguzi
Wakati mwingine mimi huwa nawaza ili uwe mwana ccm, your brain must not fuction well, ni aina ya watu wasioweza kureason wala kuchuja mambo, everything is okay with them be it right or wrong
You can imagine the burden we have as a nation, tuna watu wajinga wengi ndio maana ccm inaendelea kutawala

Mimi siamini kama Nkapa alitutoka kihalali, kuna mkono wa hayawani mmoja mnywa damu za watu amemtanguliza mapema kwa ajili ya uchu wake wa madaraka
 
Wakati mwingine mimi huwa nawaza ili uwe mwana ccm, your brain must not fuction well, ni aina ya watu wasioweza kureason wala kuchuja mambo, everything is okay with them be it right or wrong
You can imagine the burden we have as a nation, tuna watu wajinga wengi ndio maana ccm inaendelea kutawala

Mimi siamini kama Nkapa alitutoka kihalali, kuna mkono wa hayawani mmoja mnywa damu za watu amemtanguliza mapema kwa ajili ya uchu wake wa madaraka
Na akaandaa mazishi haraka haraka ili yasichelewe yaka disturb ratiba ya uchaguzi , Hutu noma sana.
 
Back
Top Bottom