Steve13, mipango ya Mungu ni ili makusudi yake yafanikiwe.
Biblia inasema akina Musa walikufa kwa sababu ya uzee na kwa amani (sina hakika kama nimetumia maneno sahihi)
Kuna nabii mmoja kwenye biblia alitumwa na Mungu akatoe ujumbe kwa mtu fulani, kwa sharti la kutokula kitu chochote. Yule nabii alifikisha ujumbe na mwenyeji wake akamsihi sana ale chakula. Nabii aligomagoma lakini mwisho wa siku alikubali kula.
Mungu alimwambia atakufa na maiti yake italiwa na Mbwa nyikani. ( Nilisoma hiki kisa zamani, inawezekana nimesahau baadhi ya vitu)
Swali langu, kwa wajuzi ni kwanini mtumishi wa Mungu afe kifo cha aibu? ( Kifo cha Yesu kilikuwa tofauti kwa sababu utabiri ulikuwa unasema hivyo, kwa hivyo tusilinganishe)