Tunaibiwa huduma za fedha katika mitandao ya simu

Tunaibiwa huduma za fedha katika mitandao ya simu

hasan124

JF-Expert Member
Joined
Jan 2, 2012
Posts
716
Reaction score
128
tiGO Pesa, M-pesa, Airtel Money ni dizasta, yani wizi nje nje katika huduma za kutuma na kutoa fedha.

Nimestushwa mno na kupanda ghafla kwa gharama hizo, Leo hii nimetuma Tzs. 30,000/= kwa jamaa yangu nashangaa nimekatwa Tzs. 1,850/=, Juzi nilituma laki4 wakanikata Tzs. 6,750/=, Nimejaribu kutuma 1mil. wanakata Tzs. 9,500/=. Je hii ni haki?

Natafakari kuna pesa kiasi gani hawa wanyonyaji wanatukamua sisi walalahoi na Je TRA wanalijua hili ama ndio zile za 10%??!!.

Imenilazimu kuandika mada hii hasa kwa kuwa wengi wetu hivi sasa tunalia na zile bukubuku walizopitisha wahishimiwa sana kule mjengoni, Najiuliza ni wapi Serikali hii ya CCM inapotupeleka?! Je haya ndio yale maisha bora kwa kila mtanzania waliokuwa wanahubiri wakati Adventurer anaomba kura?!

Tafakari chukua hatua 2015 sio mbali tunahitaji kuchukua Maamuzi Magumu Watanzania.

Pamoja Tunaweza kuiondosha CCM Madarakani.
 
hoja nzuri ila imekaa kikachumbari kachumbari sana..iweke vyema ueleweka mkuu.
 
hoja nzuri ila imekaa kikachumbari kachumbari sana..iweke vyema ueleweka mkuu.

Dhamira yangu ilikuwa ni hivyo unavyofikiri sasa, lakini kadri nilivyokua naandika majibu yalikua yanakuja kichwani kwamba ni nani
waliotufikisha hapa tulipo hivi sasa. Hizi 10% ziko maeneo mengi mno hivyo kuona uwezekano wake kuwa kwenye sekta hii ya mawasiliano ni mkubwa mno.Ccm ndio wametufikisha hapa...wizi sasa ni waziwazi...huduma hizi za Mobile Pesa ziko juu kiufanisi kuliko hata financial otitution
 
Ni kweli tunaibiwa na baadhi ya mitandao, kwa mfano mimi nakatwa shs 300, kila wiki kenye mtandao mmoja eti kwa ajili ya nyimbo kubadili nyimbo za mwito, na sasa tumepewa vifurushi vya punguzo la bei eti kwa masaa 25 hii ina maana huyo mtumiaji akitaka kufaidi inambidi awe macho mchana na usiku otherwise hilo punguzo halina mantiki kwani masaa yakiisha huna salio.Mimi nalia na TCRA kwamba kinashirikiana na makampuni haya kuhujumu wananchi kwani kilipasa kufanya ukaguzi wa makampuni hayo
 
tiGO Pesa, M-pesa, Airtel Money ni dizasta, yani wizi nje nje katika huduma za kutuma na kutoa fedha.

Nimestushwa mno na kupanda ghafla kwa gharama hizo, Leo hii nimetuma Tzs. 30,000/= kwa jamaa yangu nashangaa nimekatwa Tzs. 1,850/=, Juzi nilituma laki4 wakanikata Tzs. 6,750/=, Nimejaribu kutuma 1mil. wanakata Tzs. 9,500/=. Je hii ni haki?

Natafakari kuna pesa kiasi gani hawa wanyonyaji wanatukamua sisi walalahoi na Je TRA wanalijua hili ama ndio zile za 10%??!!.

Imenilazimu kuandika mada hii hasa kwa kuwa wengi wetu hivi sasa tunalia na zile bukubuku walizopitisha wahishimiwa sana kule mjengoni, Najiuliza ni wapi Serikali hii ya CCM inapotupeleka?! Je haya ndio yale maisha bora kwa kila mtanzania waliokuwa wanahubiri wakati Adventurer anaomba kura?!

Tafakari chukua hatua 2015 sio mbali tunahitaji kuchukua Maamuzi Magumu Watanzania.

Pamoja Tunaweza kuiondosha CCM Madarakani.[/QUOTE

Bajeti hii ilipitisha kodi kwenye huduma za kutuma pesa ndani na nje ya nchi pia simcard tax. Binafsi sipingi kodi ila napinga matumizi dhalimu ya kodi zetu.
 
Wizi mwingine wa mitandao ya simu ukikopeshwa ukiitoa ile pesa unakatwa,then bado ukuirudisha riba ipo palepale,walau basi wasingekuw wanakata muda wa kutoa,so unajikuta unarudisha almost 50 50,huu si wizi huuu
 
Back
Top Bottom