Tunahitaji Reforms; Je Reforms zipi na Tunachotaka Kitapitishwa ?

Tunahitaji Reforms; Je Reforms zipi na Tunachotaka Kitapitishwa ?

Logikos

JF-Expert Member
Joined
Feb 26, 2014
Posts
17,572
Reaction score
27,314
Wizi..., Wizi..., Wizi na Rushwa... hilo limekuwa janga tangu enzi na enzi hata walipokuwa hawaibi kulikuwa hakuna sababu ya kuiba; kwahio cha kujiuliza moja..., Je tunachotaka kitapita tukikaa kwenye majadiliano ?

Meza ya Majadiliano
  • Kuna pande zaidi ya tatu zinataka mabadiliko tofauti tofauti mengine yakiwa ni hadaa tupu.., Je tuna uhakika kile tunachotaka kitapita, sababu wengine ukiwauliza watakwambia reforms zimefanyika na walikaa kwa kutumia kodi zetu lukuki kupitisha walichopitisha hata kama kilichopita ni hadaa
Hata tukipata baadhi ya tunachotaka, je kitakomesha wizi na rushwa ? (TUME inaweza ikawa huru kutokuchaguliwa / teuliwa LAKINI ni huru kupokea Rushwa / Intimidation au hata Bias
  • Kila mtu anataka TUME HURU na hata ukiwauliza waliopo watasema waliopo ni HURU, lakini je hata akiajiliwa mtu au watu wa kudumu kwa utamaduni huu wa watu kupokea Rupia na kutoa Rupia na baadhi ya watu wenye uwezo wa kutoa Rupia ambayo ni life changing je wizi hautatokea ?
  • Kuna mianya mingi sana ya kuiba je vyama vyote vina uwezo wa kusimamia na kuhakikisha hakuna faulo sababu hata kinachotokea sasa sio legal lakini kinatokea

PENDEKEZO (Transparency UWAZI...) kila KURA iwe accountable kutokea kila KITUO kusiwe na Upenyo wa KUIBA wala KUTEGEMEA HISANI YA TUME au TAASISI
Tatizo ni WIZI na watu ni Corrupt penye UDHIA, RUPIA itapenyezwa na aliye HURU atakuwa HURU mpaka tu pale atapopewa kitu kidogo, kuwa intimidated au vyovyote vile, kwa ushauri ingawa karne hii ya automation tungeweza kabisa kufahamu ni KURA gani imepigwa na nani na wapi (ELECTRONICALLY) bado kungekuwa na uwezekano wa kucheza na MFUMO...; sasa basi kwanini lifuatalo lisifanyika kwa kutumia Teknolojia ambayo ipo tangia enzi na enzi; au hata hio electronically iwe backed up na Uhalisia unaotokea kila KITUO kwa UHAKIKI kufanyika kila KITUO
  • Kwenye kila Kituo cha kupigia KURA, KURA zihesabiwa hapo hapo na watu wala wasilazimishwe kwenda majumbani Wakae hata mita kadhaa ili waweze kutally kwamba kuna watu mia mbili wamepita kupiga KURA (Hivyo tusishangae wapigaji wakabadilka baadae na kuwa 2000)
  • Mwisho wa kupiga KURA zihesabiwa kwa mawakala na baadhi ya watu kuangalia kila kura inatolewa kwenye Boksi na kuonyeshwa na kuhesabiwa
  • Matokeo hayo ndio yawe halisi ya kupeleka kwenye Hesabu KUU hakuna sababu ya Mkurugenzi kuhesabu tena wala kusafirisha maboksi tusiyojua yana HESABU kiasi gani
  • Mwisho wa siku huko mbele ni kufanya confirmation tu lakini mchezo mzima kuishia kwenye KITUO ambapo hata mtu aliyepiga baada ya wiki akisikia KITUO chetu walipiga watu elfu hamsini wakati walihesabu watu MIA TANO aweze kuhoji
Ni hayo tu WIZI; RUSHWA, INTIMIDATION na NJAA hata tunaodhani watakuwa HURU huenda wasiwe HURU na hata wasipoteuliwa sidhani kama wataacha kuchukua MLUNGULA kwa nchi iliyogubikwa na wachukua MILUNGULA

NB: Reforms hizo zisisahau Mgombea HURU sababu kwa kulazimisha mgombea awe mwanachama wa CHAMA ni kumfanya awe kondoo wa CHAMA Husika...
 
Back
Top Bottom