Tunahitaji msaada wako Mh Lukuvi

Tunahitaji msaada wako Mh Lukuvi

Kamongo

JF-Expert Member
Joined
Mar 20, 2009
Posts
2,361
Reaction score
2,718
Sisi ni watoto yatima wa marehemu mzee Rajabu tuko watoto 9,tuna eneo letu la ekari tatu maeneo ya GOBA karibu na petrol station ya oil link,kuna mama anaitwa Lilian Kileo ametupora eneo letu kwa kushirikiana na mtendaji wa kata ya Goba bwana Mzaganya,tumefuatilia haki yetu baraza la ardhi la kata bila mafanikio,watendaji wa kata wamekuwa wakihongwa pesa na mama lilian kileo ili kutunyima haki yetu,hivyo tunaomba msaada wako,huyu mama ni tapeli maarufu wa viwanja hapa mjini,
 
Sisi ni watoto yatima wa marehemu mzee Rajabu tuko watoto 9,tuna eneo letu la ekari tatu maeneo ya GOBA karibu na petrol station ya oil link,kuna mama anaitwa Lilian Kileo ametupora eneo letu kwa kushirikiana na mtendaji wa kata ya Goba bwana Mzaganya,tumefuatilia haki yetu baraza la ardhi la kata bila mafanikio,watendaji wa kata wamekuwa wakihongwa pesa na mama lilian kileo ili kutunyima haki yetu,hivyo tunaomba msaada wako,huyu mama ni tapeli maarufu wa viwanja hapa mjini,
Pole sana huko ni balaa. Hata sisi tuko mapinga kuna mwanamke anaitwa Mwanahamisi ni tapeli wa mashamba ile mbaya. Cha kushangaza anatumia majina matatu tofauti katika utapeli wake na watendaji wanamkubalia katika mikataba ya kitapeli. Ukienda polisi utakuta ana kesi tofauti na majina tofauti lakini wamemkubalia kufungua hizo kesi. Na ukifuatilia kuhusu eneo ambalo yeye kavamia unawekwa ndani wewe mwenye eneo lako na unapelekwa mahakama ya kibaha kwa kuharibu mali. Ukifika huko anasema huyu naomba afungwe miezi sita. Waweza fungwa na yeye anaendelea kujenga kwenye kiwanja chako. Ameinunua serikali ya kijiji cha mapinga yote mpaka kituo cha polisi. Ukienda kuomba RB yake hapo kituoni hawakupi, na wakikupa hawamkamati. Ila yeye akisema kamkamate fulani, mara unakamatwa. kuna wenzetu walikamatwa na huyo mama kisa yeye huyo mama ndio kapokonya ardhi ya wenzie na akaweka walinzi. wale kujitetea kawageuzia kuwa wamebomoa sehemu ni yake. Yaani hupewi muda ukajieleza. Na anafahamika serikali yote ya kijiji lkn wanamtetea.

Hivyo kama Mh. Lukuvi yupo humu, na kuna watu wa TAKUKURU wakifuatilie hiki kituo na ofisi ya kata ya Mapinga kwa kweli watakuta malalamiko ni mengi sana kuhusu huyu mama na si kwa hao wenzetu tu hata ya watu wengine.
 
Pole sana huko ni balaa. Hata sisi tuko mapinga kuna mwanamke anaitwa Mwanahamisi ni tapeli wa mashamba ile mbaya. Cha kushangaza anatumia majina matatu tofauti katika utapeli wake na watendaji wanamkubalia katika mikataba ya kitapeli. Ukienda polisi utakuta ana kesi tofauti na majina tofauti lakini wamemkubalia kufungua hizo kesi. Na ukifuatilia kuhusu eneo ambalo yeye kavamia unawekwa ndani wewe mwenye eneo lako na unapelekwa mahakama ya kibaha kwa kuharibu mali. Ukifika huko anasema huyu naomba afungwe miezi sita. Waweza fungwa na yeye anaendelea kujenga kwenye kiwanja chako. Ameinunua serikali ya kijiji cha mapinga yote mpaka kituo cha polisi. Ukienda kuomba RB yake hapo kituoni hawakupi, na wakikupa hawamkamati. Ila yeye akisema kamkamate fulani, mara unakamatwa. kuna wenzetu walikamatwa na huyo mama kisa yeye huyo mama ndio kapokonya ardhi ya wenzie na akaweka walinzi. wale kujitetea kawageuzia kuwa wamebomoa sehemu ni yake. Yaani hupewi muda ukajieleza. Na anafahamika serikali yote ya kijiji lkn wanamtetea.

Hivyo kama Mh. Lukuvi yupo humu, na kuna watu wa TAKUKURU wakifuatilie hiki kituo na ofisi ya kata ya Mapinga kwa kweli watakuta malalamiko ni mengi sana kuhusu huyu mama na si kwa hao wenzetu tu hata ya watu wengine.
Huyu mama ametengeneza hati fake kwa kushirikiana na mtendaji kata anaitwa mzaganya,mtendaji amehongwa tsh 40M iliapindishe sheria,kwa sasa huyu mama ameleta walinzi wa kampuni binafsi walinde,pia anajenga ukuta wakati mahakama imemzuia,pia anawatumia polisi wa kituo cha kawe kututishia,mwezi uliopita walimweka ndani kaka yangu mkubwa
 
Huyu mama ametengeneza hati fake kwa kushirikiana na mtendaji kata anaitwa mzaganya,mtendaji amehongwa tsh 40M iliapindishe sheria,kwa sasa huyu mama ameleta walinzi wa kampuni binafsi walinde,pia anajenga ukuta wakati mahakama imemzuia,pia anawatumia polisi wa kituo cha kawe kututishia,mwezi uliopita walimweka ndani kaka yangu mkubwa


Una uwakika ni eneo lenu na documents zote unazo zinazoonyesha ni sehemu yebu na nyinyi mnakaa wapi kwa sasa na hilo eneo mnalo kwa mda gani??hebu nijibu naweza kukusaidia kwa chochote au mawazo na toka alivamie ni mda gani??na huyo mtendaji wa kata yupo ofisini kwa mda gani??je hilo eneo kuna wale wazee wa kijiji wanao fahamy kama eneo lenu??na una karatasi yoyote ya hilo eneo??
 
Eneo ni letu tangu mwaka 1975,na document zote tunazo,huyo mama amevamia miaka 8 iliyopita,mtendaji kata ana miaka 4 kwenye ofisi,wazee wa kijiji wapo wanatutambua kama sisi ndio wamiliki halali,
 
Kaka nenda ofisin kwa lukuvi pale wizarani,jamaa msikivu na hak yenu mtaipata.humu utachukua muda kupata msada
 
Liliani Kileo ni tapeli namba moja wa viwanja. huku kimbiji ni shida.
 
Lukuvi ana mapungufu yake kama sisi wote lakini kwa kipindi alichokaa kama waziri wa ardhi wa serikali ya Magufuli amefanya mambo makubwa ambayo mimi ni shahidi kwa vitendo. Kuna hati ya viwanja vyangu ambavyo mimi na familia yangu tulilipia toka mwaka 2010 na muda wote huo tulikuwa tunazungushwa; muda mrefu sikuwepo nchini lakini juzi juzi niliporudi na kuzungumza na rafiki yangu akanishauri nifuatilie hizo hati wizarani, nimekwenda pale wizarani sikuamini jinsi nilivyoshuhulikiwa na wafanyakazi na kuzipata hati zile chini ya saa moja!!! Hongera sana Lukuvi endeleza mwendo huo huo!!

Juu ya hayo mimi ni mkazi wa Jangwani Beach; huku kuna jirani yetu ambaye amejenga na kutuzibia njia kiasi kwamba mvua zikinyesha maji yanajaa kwenye viwanja vyetu kwani hakuna njia ya hayo maji kupita!! Ramani ya mipango miji inaonesha kuwa hiyo barabara ipo lakini malalamiko yetu huko halmashauri ya Kinondoni na wizarani hatujafanikiwa kuvunja ukuta ulioziba hiyo barabara kwani wahusika wamewahonga pesa nyingi maofisa wa ardhi. Tunaomba ushauri tufanye nini kwani ramani ya mipango miji iko wazi kuwa sehemu hiyo ni ya barabara!!
 
Sasa hivi ukiwa na shida nenda moja kwa moja kwa waziri. Kwani wanapatikana ki rahisi na sio shida kama zamani.
 
Back
Top Bottom