Hao uliowataja hawakuwa na reference popote. Walianza wenyewe hadi kufika hapo, ikiwa ni pamoja na kuturubuni na kutuibia rasilimali zetu. Leo si lazima kuanza kama kina marekani enzi za miaka ya 1770. Tuna uwezo wa kuiba, kununua na kuunda teknilijia na sera zetu za kiuchumi, kisiasa na kiteknolijia. Tunasimesha na tunahitimisha wasomi kila mwaka.Kichwa cha Yohana kwanza kinatakiwa kwenye huo upinzani ambao unatakiwa ndio uwe rejea mbadala ya Taifa.
Huwezi kutaka mambo makubwa wakati huna maono ya kuyafanikisha mambo hayo.
Wewe huwezi kuona umuhimu wa standard gauge leo hii, lakini itakapokamilika treni ya umeme kutoka Dar mpaka Burundi, hao wanaoishi kando kando yake watawasimulia wajukuu au watoto zako juu ya umuhimu wa usafiri huo.
Flyover zinao umuhimu ambao wakati huu wa ujenzi huwezi kuuona. Hayo mataifa makubwa ambayo waafrika tunaona fahari kwenda kuishi, hayakujengwa ndani ya miaka 56 ya uhuru wao.
Ujerumani ilianza kujengwa upya baada ya vita kuu ya pili. Japan ilipigwa bomu zito pale Hiroshima. Marekani mwaka jana imefikisha miaka 240 ya uhuru.
Hatuhitaji kichwa cha Yohana, kwa sababu hakuna short cut ya kutufikisha kwenye nchi ya ahadi.
Kuifikia nchi hiyo ni mchakato wa miaka mingi, pengine sisi wa kizazi cha sasa turidhike tu na ule ukweli kwamba watakaokuja kuiona Tanzania yenye neema ni wale watakaoishi miaka mingi kutoka leo hii.
Mkuu kunachofanywa na awamu ya tano kwa kiasi kikubwa sana kina lengo la kwenda huko huko walipo hao kina tiger countries. Nimetumia mfano wa Marekani kuonyesha tu kwamba sio safari ndogo ya kuyafikia maendeleo.Hao uliowataja hawakuwa na reference popote. Walianza wenyewe hadi kufika hapo, ikiwa ni pamoja na kuturubuni na kutuibia rasilimali zetu. Leo si lazima kuanza kama kina marekani enzi za miaka ya 1770. Tuna uwezo wa kuiba, kununua na kuunda teknilijia na sera zetu za kiuchumi, kisiasa na kiteknolijia. Tunasimesha na tunahitimisha wasomi kila mwaka.
Pia kuna tiger countries za pale south asia. Kina Malaysia, Thailand, Singapore, Taiwan, n.k. Hizi inasemekana wakati wa uhuru miaka ya 1960 tulikuwa nao sawa kiuchumi. Leo si wenzetu. Wako dunia ya pili. Hivyo leo kuzungumzia kuwa taifa lina miaka 56 si hoja tena
Hivi umeelewa uzi huu kweli ? Heshima gani ya kuvunja katiba ?Mkuu kunachofanywa na awamu ya tano kwa kiasi kikubwa sana kina lengo la kwenda huko huko walipo hao kina tiger countries. Nimetumia mfano wa Marekani kuonyesha tu kwamba sio safari ndogo ya kuyafikia maendeleo.
La muhimu pia ni kujifunza kuangalia mambo katika mtazamo chanya. Kuna wasomi wengi wanaosomeshwa huko nje na humu ndani, je wanaelewa maana ya kutanguliza nchi yao kwanza?.
Hao wasomi wanapopewa nafasi za kuongoza nchi, wanatambua kuwa kuna wengi walio na umasikini wenye kuhitaji sana huo ubunifu wao uliopatikana shuleni?.
Rais JPM ana heshimu sana wasomi vijana, ambao wanaingia kazini wakiwa na mtazamo mpya wenye kuendana na matakwa ya dunia ya sasa, natumaini wale ambao wanao uwezo wa kutazama vitu katika jicho chanya watakuwa wanajionea ukweli wa mambo.
Pengine kuliko wewe.Hivi umeelewa uzi huu kweli ? Heshima gani ya kuvunja katiba ?
Sidhani .Pengine kuliko wewe.
I second youAsante kwa story, lakini hakuna relevance yeyote baina ya biblia na serikali husika
Watakaokuelewa ni wachache mno.!Kwa wale wasomaji na wafuatiliaji wa maandiko matakatifu watajua kisa cha Yohana mbatizaji, yule aliyetumwa kuandaa njia katika kusubiri ujio wa Masiha, yani Yesu Kristo.
Herode alikuwa mfalme wakati huo. Naye alitokea kumpenda mke wa ndugu yake, akamfunga nduguye na kumchukua mkewe aliyeitwa Herodia. Herodia alikuwa na binti mdogo mrembo.
Wakati ule wa Herode, Yohana akijua kuwa mfalme hakutenda sawa, alichukua fursa hiyo kumsema mfalme kuwa kitendo alichofanya cha kumchukua mke wa nduguye si chema machoni pa Mungu na wanadamu. Mfalme pamoja na Herodia hawakuwa wakipendezwa na mambo aliyokuwa alisema Yohana juu mfalme. Herode aliamua kumfunga jela.
Turudi kwa Herode na Herodia. Ikawa mfalme aliandaa karamu kubwa na kuwaalika watu wengi mashuburi. Katika karamu yule bintti mdogo wa Herode alipewa fursa ya kuwaburudisha wageni. Naye alicheza mbele ya wageni kwa umahiri mkubwa. Ndipo mfalme alipohamasika sana na kumuahidi binti yake kuwa chochote atakachoomba, hata kama ni nusu ya ufalme wake atampa.
Binti alitoka akaenda kwa mama yake kuomba ushauri. Herodia kwa kuwa alikuwa na chuki na Yohana akaona ndio sehemu pekee ya kumkomoa. Basi akamwambia bintie amwambie baba yake ampatie kichwa cha Yohana kwenye sinia.
Mfalme alifadhaika sana. Hakutegemea hilo. Kwa kuwa alishaahidi kuwa atatoa chochote, hakuwa na jinsi. Walitumwa askari kule gerezani wakamkata Yohana kichwa kisha kikaletwa mbele ya mfalme na binti akakabidhiwa...
Turudi kwetu Tz. Rais amekuwa anafanya mengi. Kweli tunayaona. Mazuri kwa mabaya. Rais anajua anaongoza taifa ambalo lina itikadi tofauti kwa wananchi wake. Alipata dhamana ya kuongoza kwa kuwa ilotokea tu ikawa hivyo. Taifa lilipofikia lilihitaji mwokozi. Taifa linahitaji uratubu mpya wa mfumo. Mfumo uliopo tunasema umeshafikia maturity stage. Lazima ufe! Hakuna kuvua gamba maana gamba linaishia kiunoni tu.
Rais anajaribu ku dilute mfumo kwa kuteua watu wasio wa chama chake kwenye mfumo wa chama tawala. Tunajua uwezo wa vyama vilivyopewa mbeleko na rais. Ni kama hadaa. Watanzania hawataki hivi vitu rahisi kiasi hiki. Wanataka mapinduzi. Wanataka maamuzi magumu, japo wanayafanya ila zinatokea songombingo.
Wananchi wanataka Bunge huru. Wanataka uhuru wa vyama. Wanataka tume huru ya uchaguzi. WANATAKA KATIBA MPYA. Wanataka kichwa cha Yohana. Kinyume na hapo ni sawa na kujitekenya na kucheka mwenyewe. Hayo mambo manne ndio msingi wa Taifa lijalo. Utakumbukwa kwa hayo. Hutakumbukwa kwa flyovers wala standard gauge.
Wako wanaosema kuwa Nyerere alituletea uhuru wa kisiasa, na wewe unatuletea uhuru wa kiuchumi. Kupambana na makinikia si huo uhuru. Kukamua wananchi kodi hadi macho kutoka pima si huo uhuru. Kaa nao hao wawekezaji chemba, tena tumia wataalamu wako wafanye hizo kazi. Si kuna think tank nchini? Si ni ile tume ya mipango? Wape uhuru watu hao. Wape uhuru wapinzani wakueleze mambo mazuri. Waruhusu wakukosoe. All in all... Kichwa cha Yohana, mzee.
Maendeleo hayapimwi kwa vitu pekee,watu ndo msingi. Kama uhai,ustawi wa watu mmoja mmoja na hatimae jamii pana ni duni miundo mbinu hiyo haina tija.Kichwa cha Yohana kwanza kinatakiwa kwenye huo upinzani ambao unatakiwa ndio uwe rejea mbadala ya Taifa.
Huwezi kutaka mambo makubwa wakati huna maono ya kuyafanikisha mambo hayo.
Wewe huwezi kuona umuhimu wa standard gauge leo hii, lakini itakapokamilika treni ya umeme kutoka Dar mpaka Burundi, hao wanaoishi kando kando yake watawasimulia wajukuu au watoto zako juu ya umuhimu wa usafiri huo.
Flyover zinao umuhimu ambao wakati huu wa ujenzi huwezi kuuona. Hayo mataifa makubwa ambayo waafrika tunaona fahari kwenda kuishi, hayakujengwa ndani ya miaka 56 ya uhuru wao.
Ujerumani ilianza kujengwa upya baada ya vita kuu ya pili. Japan ilipigwa bomu zito pale Hiroshima. Marekani mwaka jana imefikisha miaka 240 ya uhuru.
Hatuhitaji kichwa cha Yohana, kwa sababu hakuna short cut ya kutufikisha kwenye nchi ya ahadi.
Kuifikia nchi hiyo ni mchakato wa miaka mingi, pengine sisi wa kizazi cha sasa turidhike tu na ule ukweli kwamba watakaokuja kuiona Tanzania yenye neema ni wale watakaoishi miaka mingi kutoka leo hii.
Mkuu Erythrocyte, nchi haihitaji kumtoa mtu kafara. Siku zote kafara huambatana na laana mbaya sana, iwapo lengo la kafara haliwezi kuwa na baraka kwa Muumba wetu.Sidhani .
Kutopimwa kwa maendeleo kupitia kwa mabadiliko ya maisha ya watu hakumaanishi kwamba hakuna kinachoendelea katika uhalisia wa kuifanya Tanzania kuwa ni nchi yenye tofauti kati ya jana, kesho na kesho kutwa.Maendeleo hayapimwi kwa vitu pekee,watu ndo msingi. Kama uhai,ustawi wa watu mmoja mmoja na hatimae jamii pana ni duni miundo mbinu hiyo haina tija.
Tunaiangalia Tanzania na si mtu fulani. Kama huyo mtu ataweza kuivusha nchi na kuipeleka kule tunakotaka basi ni heri. Lakini hao wananchi wanataka nini? Kiongozi wa nchi anapoamini kuwa hawezi kufanya kazi kwenye kelele za upinzani ni udhaifu mkubwa. Ndani ya kelele hizo kuna majibu kwa watz. Waache watu waseme na watazame ili siku ikifika uwathibitishie kuwa hawakuwa sahihi. Hakuna sababu ya kuzima wengine ili tuone kuwa wewe ni mtendaji bora.Mkuu kunachofanywa na awamu ya tano kwa kiasi kikubwa sana kina lengo la kwenda huko huko walipo hao kina tiger countries. Nimetumia mfano wa Marekani kuonyesha tu kwamba sio safari ndogo ya kuyafikia maendeleo.
La muhimu pia ni kujifunza kuangalia mambo katika mtazamo chanya. Kuna wasomi wengi wanaosomeshwa huko nje na humu ndani, je wanaelewa maana ya kutanguliza nchi yao kwanza?.
Hao wasomi wanapopewa nafasi za kuongoza nchi, wanatambua kuwa kuna wengi walio na umasikini wenye kuhitaji sana huo ubunifu wao uliopatikana shuleni?.
Rais JPM ana heshimu sana wasomi vijana, ambao wanaingia kazini wakiwa na mtazamo mpya wenye kuendana na matakwa ya dunia ya sasa, natumaini wale ambao wanao uwezo wa kutazama vitu katika jicho chanya watakuwa wanajionea ukweli wa mambo.